Rais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi amesafiri kuelekea Nchini Msumbiji Kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Sadc
07 Apr 2021
375
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi akisalimiana na Wakuu
wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Zanzibar,Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Abeid Amani Karume akiondoka Zanzibar kuelekea Nchini Msumbiji
kumuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu
Hassan, katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za SADC unaofanyika Jijini Maputo
Msumbiji.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman,Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe Idrisa Mustafa Kitwana, akielekea Nchini Msumbiji kuhudhuria
Mkutano wa Wakuu wa Nchi za SADC, akimuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,unaofanyeka Jijini Maputo Msumbuji.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na kuagana na Meya wa Jiji la Zanzibar Mhe. Mahmoud Mohammed Mussa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said,Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akielekea
Nchini Msumbiji kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za SADC, kumuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.