State House Blog

Ufunguzi wa Msikiti wa Ijumaa Chuini Zanzibar.

  • Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa nne kulia) akijumuika na Viongozi na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika sala ya Ijuma mara baada ya Kufungua Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair uliopo Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja, uliojengwa kupitia Wafadhili na Waislamu mbali mbali, ambapo sala ilioongozwa na Sheikh Rashid Salim (mbele).
  • Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akitoa nasaha zake kwa waumini wa dini ya Kiislamu baada ya ufunguzi wa Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair, Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja, uliojengwa kupitia Wafadhili na michango ya Waislamu mbali mbali.
  • Waumini wa Dini ya Kiislamu wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha zake kwa waumini hao baada ya sala ya Ijumaa na ufunguzi wa Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair, Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja, uliojengwa kupitia Wafadhili na michango ya Waislamu mbali mbali.
  • Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili leo katika Ufunguzi wa Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair uliopo Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja.
  • Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) akifungua pazia kuashiria Ufunguzi wa Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair uliopo Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja, uliojengwa kupitia Wafadhili na Waislamu mbali mbali.
  • Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akikata utepe kama ishara ya ufunguzi wa Masjid Muhammed Bin Ahmed Al Jofair uliopo Chuini Wilaya ya Magharibi A Unguja, uliojengwa kupitia Wafadhili na Waislamu mbali mbali.