<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:admin="http://webns.net/mvcb/"
	xmlns:rdf="http://www.w3.org/1999/02/22-rdf-syntax-ns#"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/">

	<channel>
	
	<title>Media Centre</title>
	<link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media</link>
	<description></description>
	<dc:language>en</dc:language>
	<dc:creator>info@ikuluzanzibar.go.tz</dc:creator>
	<dc:rights>Copyright 2026</dc:rights>
	<dc:date>2026-05-14T11:29:00+00:00</dc:date>
	<admin:generatorAgent rdf:resource="https://www.ikuluzanzibar.go.tz/index.php/" />
	<item>
	  <title>Vision and Mission</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/vision-and-mission</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/vision-and-mission#When:09:02:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Vision &amp;amp; Mission ,</dc:subject>
	  <dc:date>2014-02-12T09:02:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Overview of the President’s Office and Chairman of the Revolutionary Council</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/overview-of-the-presidents-office-and-chairman-of-the-revolutionary-council</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/overview-of-the-presidents-office-and-chairman-of-the-revolutionary-council#When:09:08:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[The President’s Office and the Chairman of the Revolutionary Council (POCRC) is one among sixteen Ministries established in the Seventh Phase of the Revolutionary Government of Zanzibar. The Office plays a central role that lies in overseeing development programmes and activities aiming at reduction and ultimately alleviation of poverty among Zanzibari’s as well as strengthening Good Governance and Human Rights]]></description> 
	  <dc:subject>Overview,</dc:subject>
	  <dc:date>2014-02-12T09:08:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>President&#8217;s Office Contact Details</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/presidents-office-contact-details</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/about/presidents-office-contact-details#When:09:36:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Contact Details,</dc:subject>
	  <dc:date>2011-11-25T09:36:00+00:00</dc:date>
	</item>
 	<item>
	  <title>H.E. Dr. Hussein Ali Mwinyi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-dr-hussein-ali-mwinyi-3</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-dr-hussein-ali-mwinyi-3#When:15:20:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Office of the President, President,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:20:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon:.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/nd</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/nd#When:15:19:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Chief,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:19:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Nd.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/ambassador-eng-zena-ahmed-said</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/ambassador-eng-zena-ahmed-said#When:15:19:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Office of the President, Secretary,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:19:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>H.E.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-othman-mosoud-othman</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-othman-mosoud-othman#When:15:19:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Vice President,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:19:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>H.E. Hemed Suleiman Abdullah</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-hemed-suleiman-abdullah</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/h.e-hemed-suleiman-abdullah#When:15:18:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Vice President,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:18:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon. Saada Mkuya Salum</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-ali-suleiman-ameir-mrembo</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-ali-suleiman-ameir-mrembo#When:15:18:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Minister,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:18:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon. Shariff Ali Shariff</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-shariff-ali-shariff</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-shariff-ali-shariff#When:15:17:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Minister,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:17:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon. Idrissa Kitwana Mustafa</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-masoud-ali-mohammed</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-masoud-ali-mohammed#When:15:17:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Minister,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:17:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon. Haroun Ali Suleiman</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-haroun-ali-suleiman</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-haroun-ali-suleiman#When:15:17:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Minister,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:17:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hon.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-harusi-said-suleiman</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/administration/view/hon-harusi-said-suleiman#When:15:16:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Revolutionary Council, Minister,</dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-20T15:16:00+00:00</dc:date>
	</item>

	<item>
	  <title>THE ZANZIBAR PLANNING  COMMISSION ACT,NO.3 OF 2012</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/the-zanzibar-planning-commission-actno.3-of-2012</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/the-zanzibar-planning-commission-actno.3-of-2012#When:06:46:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Laws,</dc:subject>
	  <dc:date>2014-06-26T06:46:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>THE POLITICAL LEADERS RETIREMENT BENEFITS ACT,NO.2 OF 2012</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/the-political-leaders-retirement-benefits-actno.2-of-2012</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/the-political-leaders-retirement-benefits-actno.2-of-2012#When:06:42:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Laws,</dc:subject>
	  <dc:date>2014-06-26T06:42:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>PRESIDENTIAL  AFFAIRS ACT NO 5 1993</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/presidential-affairs-act-no-5-1993</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/zanzibar/view/presidential-affairs-act-no-5-1993#When:06:40:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject>Laws,</dc:subject>
	  <dc:date>2014-06-26T06:40:00+00:00</dc:date>
	</item>

	<item>
	  <title>Dk. Mwinyi ameishukuru Serikali ya India kwa kuendeleza ushirikiano na misaada yake kwa Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendeleo, kijamii na kiuchumi.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dk-mwinyi-ameishukuru-serikali-ya-india-kwa-kuendeleza-ushirikiano-na-misaada-yake-kwa-zanzibar-katika-sekta-mbalimbali-za-maendeleo-kijamii-na-kiuchumi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dk-mwinyi-ameishukuru-serikali-ya-india-kwa-kuendeleza-ushirikiano-na-misaada-yake-kwa-zanzibar-katika-sekta-mbalimbali-za-maendeleo-kijamii-na-kiuchumi#When:11:29:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru India kwa kuendeleza ushirikiano na misaada yake kwa Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendeleo, kijamii na kiuchumi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 14 Mei 2026, alipokutana na Balozi Mdogo wa India aliyepo Zanzibar, Balozi Kumar Praveen, aliyefika Ikulu kwa ajili ya kuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-14T11:29:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Serikali inakusudia kutoa Kibali cha Ajira Mpya katika Mwaka Mpya wa Fedha katika sekta  ya Afya na Kada nyengine ili kukabiliana na Tatizo la  Uhaba wa Wauguzi hapa Nchini.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-inakusudia-kutoa-kibali-cha-ajira-mpya-katika-mwaka-mpya-wa-fedha-katika-sekta-ya-afya-na-kada-nyengine-ili-kukabiliana-na-tatizo-la-uhaba-wa-wauguzi-hapa-nchini</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-inakusudia-kutoa-kibali-cha-ajira-mpya-katika-mwaka-mpya-wa-fedha-katika-sekta-ya-afya-na-kada-nyengine-ili-kukabiliana-na-tatizo-la-uhaba-wa-wauguzi-hapa-nchini#When:15:30:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali inakusudia kutoa Kibali cha Ajira Mpya katika Mwaka Mpya wa Fedha katika sekta  ya Afya na Kada nyengine ili kukabiliana na Tatizo la  Uhaba wa Wauguzi hapa Nchini. Rais Dķt, Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 12 Mei 2026 katika Kongamno  kwanza la Kisayansi la Wauguzi  lilioambatana na  Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, hafla iliofanyika  Hoteli  Verde ,Mkoa wa Mjini Magharibi. ]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-12T15:30:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Serikali itachukua hatua kuhakikisha watu waliolipwa fidia zisizostahiki katika maeneo yaliyopitishwa miradi ya maendeleo wanazirejesha fedha hizo Serikalini.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-itachukua-hatua-kuhakikisha-watu-waliolipwa-fidia-zisizostahiki-katika-maeneo-yaliyopitishwa-miradi-ya-maendeleo-wanazirejesha-fedha-hizo-serikalini</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-itachukua-hatua-kuhakikisha-watu-waliolipwa-fidia-zisizostahiki-katika-maeneo-yaliyopitishwa-miradi-ya-maendeleo-wanazirejesha-fedha-hizo-serikalini#When:07:21:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itachukua hatua kuhakikisha watu waliolipwa fidia zisizostahiki katika maeneo yaliyopitishwa miradi ya maendeleo wanazirejesha fedha hizo Serikalini. Dkt. Mwinyi amefahamisha kuwa ripoti iliyowasilishwa na Tume ya Tathmini ya Masuala ya Fidia kwa Wananchi Waliopisha Miradi ya Maendeleo imeonesha kuwa wapo baadhi ya wananchi waliolipwa fidia ili kupisha miradi lakini hawakuondoka katika maeneo hayo, huku wengine wakiendelea na ujenzi licha ya kulipwa fidia zao.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-10T07:21:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Mwinyi amesema SMZ kuongeza kasi ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-amesema-smz-kuongeza-kasi-ya-ujenzi-wa-miradi-ya-maendeleo</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-amesema-smz-kuongeza-kasi-ya-ujenzi-wa-miradi-ya-maendeleo#When:15:55:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaongeza kasi ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara za kisasa kwa lengo la kuibadilisha Zanzibar kuwa nchi ya kisasa.  Dkt. Mwinyi amesema hayo leo tarehe 09 Mei 2026 alipokutana na viongozi na wanachama wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama katika mkutano maalum wa kutoa shukrani baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 uliofanyika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Amani, Mkoa wa Mjini Magharibi.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-09T15:55:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt.Mwinyi amesema CCM ipo tayari kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amesema-ccm-ipo-tayari-kuunda-serikali-ya-umoja-wa-kitaifa-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amesema-ccm-ipo-tayari-kuunda-serikali-ya-umoja-wa-kitaifa-zanzibar#When:08:35:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema mazungumzo ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa kati ya CCM na ACT-Wazalendo yanaendelea vizuri huku CCM ikiwa tayari kushiriki katika kuunda Serikali hiyo kwa maslahi ya Taifa na wananchi.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-09T08:35:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hotuba ya Waziri wa Nchi Afisi ya Rais &#45; Ikulu &amp;nbsp; Mheshimiwa Dkt. Saada Mkuya Salum (MBM) kuhusu makadirio ya mapato na matumizi &amp;nbsp; kwa mwaka wa Fedha 2026/2027.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-kwa-mwaka-wa-fedha-2026-2027</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-kwa-mwaka-wa-fedha-2026-2027#When:12:20:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[YALIYOMO ORODHA YA VIAMBATANISHO .......................................................iv <br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO ................................................................vi <br />
<br />
UTANGULIZI .........................................................................................1 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YARAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ..............................................7 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU A01). ....................................................................................7 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Kusimamia na Kuratibu Shughuli na Huduma za Mheshimiwa Rais na Kuimarisha Mawasiliano Ikulu. ........8 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Kuratibu Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. .............11<br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Afisi ya Rais – Ikulu. ...............................................................................14 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MIRADI YA MAENDELEO .............17 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU A02) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. .....................18 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Majukumu ya Kikatiba na Kisheria ya BLM. ......................................................................19 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utumishi na Uendeshaji wa Ofisi ya Baraza la Mapinduzi .............................................................20 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI ZANZIBAR (FUNGU A09) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ……………………….....20 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA ZPDB (FUNGU A09) .........21<br />
<br />
 i. Programu Kuu ya Usimamizi na Uratibu wa Huduma za Serikali .......................................................................................21 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Mipango ya Miradi ya Kipaumbele na Uendeshaji. ............................................................................23 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAENDELEO KWA FUNGU A09 ……………......24 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU ZANZIBAR (FUNGU A10) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ....................................25 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027<br />
<br />
ii i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Nyaraka na Kumbukumbu kwa matumizi ya Serikali na Umma. ............25<br />
<br />
 ii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu. ..............................................27 <br />
<br />
MWELEKEO WA BAJETI YA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ......................................................................27.<br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO NA MAKISIO YA FEDHA ZINAZOHITAJIKA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ...............29 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU 001) .................................................................................................30 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Shughuli za Mheshimiwa Rais na Uimarishaji wa Mawasiliano. ...................................30 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Uratibu wa Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. ................31 <br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji. ...........................32 <br />
<br />
MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOTEKELEZWA NA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ..................................33 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU 040). ...................................................................................34<br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Majukumu ya Kikatiba na Kisheria ya BLM. ................................................................34 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utumishi na Uendeshaji wa Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi. ..............................................................35 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU (FUNGU 057) ..........................................................36 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Nyaraka na Kumbukumbu kwa Matumizi ya Serikali na Umma. .....................................36 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji .........................37 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI (FUNGU 058) …….....38 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi na Uratibu wa Miradi ya Serikali. ..................................................................................................38 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 iii ii. Programu Kuu ya Mipango ya Miradi ya Kipaumbele na Uendeshaji. ..............................................................................39 <br />
<br />
MAOMBI YA FEDHA YA KAZI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027. .....................................................40 <br />
<br />
HITIMISHO ........................................................................................40 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
iv ORODHA YA VIAMBATANISHO KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
01. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU 001) ..44 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
02. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU 040) ....................................................................................47 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.<br />
<br />
03. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI (FUNGU 058) ...............48 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 04. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI - MACHI) KWA 2025 – 2026 KWA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU (FUNGU 057) ....................................................................................49 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 05. ORODHA YA ZIARA ZA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO. ........................................50 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 06. ORODHA YA ZIARA ZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO. ........................................51 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 07. ORODHA YA MIKUTANO YA KIKANDA NA KIMATAIFA AMBAYO RAIS WA ZANZIBAR AMESHIRIKI......................53 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
08. ORODHA YA VIKAO VYA MHESHIMIWA RAIS WIZARA ZA KISEKTA ZA SERIKALI ...................54 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
09. ORODHA YA MABALOZI NA WAGENI MASHUHURI WA NCHI ZA NJE WALIOMTEMBELEA MHESHIMIWA RAIS....................................................56 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
10. ORODHA YA IDADI YA SHEHIA ZILZOTEMBELEWA NA WANANCHI WALIOFIKIWA KATIKA MAFUNZO YA SNR..................................................... 58 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
11. USHIRIKI WA IDARA KATIKA MIKUTANO NA VIKAO ZA JUMUIYA ZA KIKANDA NA KIMATAIFA………………60 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.<br />
<br />
12. ORODHA YA MIKUTANO NA VIKAO YA URATIBU WA SHUGHULI ZA DIASPORA ZANZBAR. ......63 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.13. <br />
<br />
ORODHA YA WATUMISHI WALIOPATIWA MAFUNZO. ............................................................. 64 <br />
<br />
v HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO <br />
<br />
AfCFTA BLM CAN CCM EAC ECDP GSO ITV IORA NTBs PAC RAMIS SADC SNR TADIO TBC TOKTEN UAE UNDP UNFPA ZASO ZBC ZCTV ZNCC ZPDB Eneo huru la Biashara Barani Afrika Baraza la Mapinduzi Climate Action Network Tanzania Chama cha Mapinduzi Jumuiya ya Afrika Mashariki Early Childhood Development Programme Afisi ya Usalama wa Serikali Independent Television Indian Ocean Rim Association Non-Tariff Barriers Kamati ya Bajeti, na Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Hesabu za Serikali Mfumo wa kielektroniki wa uhifadhi na matumizi ya nyaraka na kumbumbuku Jumiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika Sema na Rais Mwinyi Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Oman Shirika la Utangazaji la Tanzania Transfer of knowlegde through expartriete Nationals Umoja wa Falme za Kiarabu United Nations Development Programme United Nations Population Fund Zanzibar Association of Sports Officers Shirika la Utangazaji la Zanzibar Zanzibar Cable Television Zanzibar National Chamber of Commerce Taasisi ya Afisi ya Rais ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini Zanzibar. <br />
<br />
vi HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 UTANGULIZI 1. 2. 3. 4. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Naomba kutoa hoja kwamba Baraza lako lipokee na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Afisi ya Rais - Ikulu na Taasisi zake kwa Mwaka 2025/2026 na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Afisi ya Rais - Ikulu (Fungu A01), Baraza la Mapinduzi (Fungu A02), Taasisi ya Afisi ya Rais ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa utendaji Serikalini (Fungu A09), na Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu (Fungu A10) kwa mwaka 2025/2026. Mheshimiwa Spika, Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima, siha njema, amani na utulivu vinavyotuwezesha kuendelea kutekeleza majukumu yetu yanayochangia kuleta maendeleo na kujenga ustawi wa Taifa. <br />
<br />
Pia, tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana katika kipindi hiki cha Mkutano wa 03 wa Baraza la 11 kwa ajili ya kupokea utekelezaji wa Afisi ya Rais - Ikulu pamoja na kutafakari mipango ijayo katika kufikia malengo ya Nchi. Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imetekeleza jukumu lake la kikatiba kwa kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Napenda kuwapongeza wananchi wote wa Zanzibar kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo muhimu la kidemokrasia, wakitumia haki yao ya msingi kwa amani na utulivu. Vilevile, napenda kuvipongeza vyama vyote vya siasa vilivyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu, jambo linaloonesha kuimarika kwa misingi ya demokrasia nchini na ukomavu wa kisiasa miongoni mwa Watanzania. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kipekee napenda kutumia fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa imani yake kwangu na kuendelea kunipa dhamana ya kusimamia Afisi ya Rais - Ikulu, yenye jukumu kubwa la kusimamia na kuratibu utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali, kuhakikisha nidhamu na utendaji bora wa watumishi wa umma na kukuza maendeleo endelevu ya kijamii, kiuchumi 1 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 na kiutawala kwa wananchi na hatimae kuwa na Serikali yenye ufanisi na uwajibikaji kwa ustawi wa Taifa. 5. 6. 7. 8. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kwa heshima na adhama ya kipekee, napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kufuatia ushindi wa kishindo alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa Vyama Vingi uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025. Ushindi huu ni kielelezo cha imani kubwa ya wananchi kwake, pamoja na uimara wa mikakati ya kisiasa iliyosimamiwa kwa umakini na maono ya muda mrefu. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kampeni za Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi zilijengwa juu ya msingi unaogusa uhalisia wa maisha ya wananchi, kuimarisha umoja wa kitaifa, kuchochea mageuzi ya kiuchumi na kudumisha misingi ya utawala bora. Ujumbe huu uliwasilishwa kwa utulivu, umakini na mwelekeo ulioeleweka kwa urahisi, hali iliyochangia kuimarisha uungwaji mkono kutoka kwa sekta mbalimbali za jamii. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Katika kipindi chote cha kampeni, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi aliendelea kujijengea taswira ya kuwa kiongozi makini, mwenye dira iliyo wazi na anayethamini maoni ya wananchi. Uwezo wake wa kusikiliza, kuelewa na kujibu changamoto za wananchi kwa vitendo uliimarisha zaidi uhusiano wa kuaminiana kati ya uongozi na jamii. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Ushindi wake katika uchaguzi huo na hatimaye kuapishwa kwake rasmi tarehe 02 Novemba 2025, ni matokeo ya mchakato uliotekelezwa kwa nidhamu na ufanisi, ukihusisha mikakati madhubuti ya kisiasa, mawasiliano yenye ushawishi chanya, pamoja na mshikamano wa dhati kati ya chama na wananchi. Kwa ujumla, kampeni za Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi zilionesha kiwango cha juu cha ubora wa kisiasa na kimkakati. Ziliweka msingi imara wa ushindi huo na kuendelea kipindi cha pili cha awamu ya uongozi wake unaolenga kuharakisha maendeleo 2 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 endelevu ya Zanzibar, kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na mustakabali wa taifa kwa ujumla.<br />
<br />
9. Mheshimiwa Spika, Natoa wito kwa wananchi na wadau wote kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha juhudi za maendeleo ya taifa letu. Aidha, ninawakumbusha viongozi wote waliochaguliwa kuendelea kuweka mbele maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, uwazi na kujituma katika kila nafasi waliyopewa. <br />
<br />
10. Mheshimiwa Spika, Mwaka mmoja ni kipindi kirefu katika maisha ya binadamu na mara nyingi huambatana na matukio na changamoto za maisha. Napenda kuwapa pole wananchi wote walioathiriwa na majanga yaliyotokea katika kipindi cha harakati zao za kujitafutia kipato na maisha. <br />
<br />
11. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuwa karibu na wananchi hao na itaendelea kushirikiana nao katika kukabiliana na changamoto hizo, kwa lengo la kuhakikisha wanapata msaada unaostahiki na kurejesha hali ya ustawi katika maisha yao. <br />
<br />
12. Mheshimiwa Spika, Naomba kuliahidi Baraza lako Tukufu na wananchi wote kuwa nitaendelea kutekeleza majukumu yangu kwa uadilifu, bidii na weledi mkubwa, ili kuendeleza mafanikio yaliyofikiwa na kuhakikisha kwamba Bajeti hii inasimamiwa kwa ufanisi na kutekelezwa ipasavyo. Hakika, mafanikio makuu yaliyopatikana Zanzibar yametokana na maono ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, katika kuwaletea Wazanzibari maendeleo endelevu. <br />
<br />
Tunajivunia na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kiongozi mwenye maono chanya kwa mustakabali wa Taifa letu. Naomba tuendelee kumuombea Mwenyezi Mungu amjalie afya njema, hekima, busara, na ustahimilivu katika kuliongoza Taifa letu. <br />
<br />
3 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
13. Mheshimiwa Spika, Nalikumbusha Baraza lako Tukufu kuwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameweka wazi mwelekeo mpya wa Serikali katika kipindi chake cha pili, ukiangazia mageuzi ya kiuchumi na ustawi wa wananchi. Katika hotuba yake ya uzinduzi wa Baraza la kumi na moja la Wawakilishi tarehe 10 Novemba 2025, Mheshimiwa Rais alisisitiza kuwa Serikali itajikita katika kukuza ukuaji wa uchumi kwa kutumia nguvu za uzalishaji, kuongeza uwekezaji, na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika biashara na viwanda. <br />
<br />
14. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais Mwinyi pia alibainisha umuhimu wa kuimarisha utendaji wa sekta zinazochangia ukuaji wa uchumi, kuimarisha mazingira ya kupata mtaji, na kuendeleza fursa za uwekezaji zinazovutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Mwelekeo huu mpya unalenga kuhakikisha maendeleo yanayojumuisha kila kona ya jamii; wakulima, wafanyabiashara wadogo na wakubwa, na vijana katika masuala ya ajira na ubunifu. <br />
<br />
15. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amesisitiza usalama, amani, umoja wa kitaifa, na nidhamu ya kitaalamu kama misingi ya utekelezaji wa sera za uchumi na maendeleo endelevu katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake. Serikali inalenga kujenga uchumi imara, wa kisasa, na wenye mshikamano, utakaowawezesha Wazanzibari kushindana vyema katika mazingira ya kimataifa ya kibiashara na kupata faida za moja kwa moja. <br />
<br />
16. Mheshimiwa Spika, Napenda kutoa shukrani zangu za dhati na pongezi kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake madhubuti na wa kimkakati. Ameongoza jitihada za kukuza uchumi na kuimarisha maisha ya Watanzania, akiwahusisha wakulima, wafanyabiashara, na vijana katika maendeleo. Uongozi wake umeimarisha mazingira ya uwekezaji, kuimarisha miundombinu, na kuendeleza mshikamano wa kitaifa. Aidha, juhudi za Serikali zimepanua fursa za mikopo 4 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 kwa wakulima, wavuvi, na wafugaji, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa kipato kwa wananchi. Mwelekeo huu unaonesha dhamira ya kujenga uchumi imara, wa kisasa, na unaotoa faida kwa kila mwananchi. <br />
<br />
17. Mheshimiwa Spika, Kwa moyo wa dhati napenda kumshukuru Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, kwa juhudi zake kubwa katika kuhakikisha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatekeleza majukumu yake kwa umakini. Ushirikiano wake na Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi umeimarisha ufanisi wa Serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kutoa huduma bora kwa wananchi. <br />
<br />
18. Mheshimiwa Spika, Naomba nikupongeze wewe binafsi pamoja na Naibu Spika kwa kuliongoza Baraza letu Tukufu kwa umahiri mkubwa uliodhihirika katika kufikia maamuzi yenye manufaa kwa ustawi wa wananchi, hakika mmesimama imara kuongoza Muhimili huu muhimu kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya Taifa na Mwenyezi Mungu aendelee kuwatia nguvu zaidi. Niwapongeze pia Wenyeviti wa Baraza kwa kukusaidia wewe kuongoza vyema vikao vya Baraza letu, ni dhahiri kuwa muhimili huu umetoa mchango mkubwa kwenye maamuzi ya nchi yetu. <br />
<br />
19. Mheshimiwa Spika, Nichukue nafasi hii pia kuwapongeza Mawaziri wenzangu wote wa Serikali ya Awamu ya Nane kwa kuendelea kupewa dhamana ya kuwatumikia Wazanzibari na kwa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025/2030 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050. <br />
<br />
20. Mheshimiwa Spika, Nikiwa miongoni mwa watekelezaji wa Ilani ya CCM nichukue fursa hii kuwapongeza viongozi wote walioteuliwa kushika nafasi za kumsaidia Mwenyekiti kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM. Tuendelee kushirikiana kutekeleza Ilani na miongozo mingine ya kitaifa ili kujenga Taifa letu. 5 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
21. Mheshimiwa Spika, Napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa Balozi Mhandisi Zena Ahmed Said, aliyekuwa Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha utendaji wa Serikali na kuhakikisha malengo yanafikiwa kwa ufanisi. Uongozi wake mahiri katika kusimamia watendaji wa Serikali umeacha alama muhimu ya mafanikio tunayojivunia leo. Aidha, tunampongeza kwa kuteuliwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Saudi Arabia na tunamtakia kila la kheri katika kuendelea kulitumikia Taifa katika nafasi hiyo mpya. <br />
<br />
22. Mheshimiwa Spika, Vile vile, nawashukuru kwa dhati Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi, hususan Kamati ya Kusimamia Afisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Machano Othman Said, Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini na Makamu wake Mheshimiwa Azza Januari Joseph, Mwakilishi wa Kuteuliwa kupitia nafasi Maalum za Wanawake pamoja na wajumbe wa kamati kwa ushirikiano, maelekezo na ushauri mzuri wanaotupatia ambao umetuwezesha kufanikisha utendaji wa kazi zetu. Aidha, nazishukuru Kamati ya Bajeti na Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Hesabu za Serikali (PAC), Ushirikiano, busara na maelekezo yao yamekuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha utendaji wa Serikali. <br />
<br />
23. Mheshimiwa Spika, Nichukue fursa adhimu ya kumshukuru na kumpongeza Ndugu Raya Issa Mselem, Katibu wa Baraza la Wawakilishi kwa Utendaji wake bora na mashirikiano anayonipa yeye binafsi na watendaji wengine wote wa Baraza la Wawakilishi. <br />
<br />
24. Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa kila mmoja wetu kuendelea kuiunga mkono Serikali, kudumisha mshikamano wa kitaifa, na kushiriki kikamilifu katika juhudi za kujenga Zanzibar imara yenye maendeleo jumuishi kwa ustawi wa wananchi. Ushirikiano huu ni nguzo muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo na kuhakikisha kuwa 6 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 rasilimali za taifa zinatumika kwa ufanisi na kwa manufaa ya wananchi wote. <br />
<br />
25. Mheshimiwa Spika, Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 Afisi ya Rais - Ikulu iliwasilisha mbele ya Baraza lako Tukufu, Mpango na Bajeti ya Afisi na kuomba fedha ili kutekeleza majukumu yake. Ninayo heshima kusimama tena mbele ya Baraza lako Tukufu ili niweze kutoa taarifa ya utekelezaji wa Mpango ulioombewa fedha kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 na kuwasilisha Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. <br />
<br />
26. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais - Ikulu, kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 ilijipangia kutekeleza Programu Kuu tisa (09) zenye Programu ndogo kumi na tano (15). Kiambatanisho nambari 01, 02, 03 na 04 vina maelezo ya ziada kuhusu Programu Kuu na Programu Ndogo. UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGUA01). <br />
<br />
27. Mheshimiwa Spika, Fungu A01 limejumuisha Programu Kuu tatu na Programu Ndogo nane. Kwa kipindi cha Julai, 2025 hadi Machi 2026, fungu hili limetumia TZS. 7.94.Bilioni sawa na asilimia 51.87 ya makadirio ya TZS.15.30 Bilioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 39.52 ya makadirio ya kutumia TZS. 20.09 Bilioni kwa mwaka. Mchanganuo wa matumizi hayo ni kama ifuatavyo: a) Malipo ya Mishahara TZS. 5.06 Bilioni sawa na asilimia 98.78 ya makadirio ya TZS, 5.12 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. b) Matumizi Mengineyo TZS. 1.51 Bilioni sawa na asilimia 43.34 ya makadirio ya TZS. 3.49 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. 7 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 c) Matumizi ya Mradi wa Maendeleo TZS.1.37 Bilioni sawa na asilimia 20.46 ya makadirio ya TZS. 6.70 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
28. Mheshimiwa Spika, Fedha hizo zimetumika kutekeleza programu kuu zifuatazo: i. Programu Kuu ya Kusimamia na Kuratibu Shughuli na Huduma za Mheshimiwa Rais na Kuimarisha Mawasiliano Ikulu. <br />
<br />
29. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 3.88 Bilioni sawa na asilimia 85.67 ya makadirio ya TZS. 4.53 Bilioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 64.81 ya makadirio ya TZS. 5.99 Bilioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo mbili zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu wa Huduma za Mheshimiwa Rais imetumia TZS. 3.39 Bilioni sawa na asilimia 91.60 ya makadirio ya kutumia TZS.3.70 Bilioni kwa kipindi cha tathmini; na b) Programu ndogo ya Kuimarisha Mawasiliano baina ya Serikali na Wananchi imetumia TZS. 492.89 Milioni sawa na asilimia 59.27 ya makadirio ya kutumia TZS. 831.63 Milioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
30. Mheshimiwa Spika, kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: i. Kutoa ushauri kwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika masuala ya siasa, uchumi, jamii, sheria, diplomasia, mawasiliano na habari, pamoja na uhusiano wa kikanda na kimataifa, na masuala mengine muhimu. <br />
<br />
ii. Kusimamia ratiba ya kila siku ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kuhakikisha kwamba shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa mipango iliyowekwa na kwa ufanisi unaotarajiwa. 8 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
iii. Ziara nane (08) za ukaguzi wa miradi ya maendeleo ndani ya visiwa vya Zanzibar zimefanyika. Ziara hizi zimehusu ukaguzi wa miradi katika sekta ya elimu, afya, michezo, maji, miundombinu na kilimo, kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji wake unakidhi viwango vinavyotarajiwa, kutumia rasilimali kwa ufanisi na kutoa mapendekezo ya kuimarisha miradi hii ili kufanikisha maendeleo endelevu kwa wananchi. Kiambatanisho nambari 05 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
iv. Kuratibu uzinduzi wa miradi kumi na nane (18) mikubwa, miradi ambayo ina faida za moja kwa moja kwa wananchi katika sekta ya elimu, afya, maji, nishati na miundombinu. Miradi hii inalenga kuimarisha huduma za jamii, kuongeza fursa za kiuchumi, na kuhakikisha maendeleo endelevu yanayogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Kiambatanisho nambari 06 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
v. Kuratibu ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika mikutano minne (04) ya kikanda na kimataifa yenye lengo la kukuza ushirikiano wa kibiashara, uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi. Mikutano hii imejumuisha Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika, Mkutano wa Usajili Barani Afrika na Mkutano wa Uhakiki wa Rasimu ya Mkakati wa kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji. Ushiriki huu umehusisha mazungumzo na wadau mbalimbali, kutafuta fursa za uwekezaji, kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kushirikiana katika miradi ya maendeleo, ili kuhakikisha Zanzibar inapata faida za kiuchumi na kimaendeleo. Kiambatanisho nambari 07 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
vi. Kuratibu na kuendesha vikao 22 vya kiserikali. Vikao hivi vilitumika kutoa maelekezo ya kiutendaji kwa wizara na taasisi 17 za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kupitia vikao hivi, Mheshimiwa Rais amesisitiza uwajibikaji na nidhamu katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali. Kiambatanisho nambari 08 kina taarifa zaidi. 9 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 vii.Kuratibu na kufanikisha shughuli ya kutunuku Nishani ya Mapinduzi na Nishani ya Utumishi Uliotukuka kwa viongozi na wananchi 18 wenye sifa maalum, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika historia, maendeleo na ustawi wa Zanzibar. viii.Kuratibu hafla ya utiaji saini wa mikataba ya miradi mitatu mikubwa ya kimkakati iliyofanyika Ikulu Zanzibar, ikiwemo mradi wa Mfumo Jumuishi wa Usimamizi na Usajili wa Huduma za Ardhi, Mradi wa Usambazaji Maji Kusini Unguja na ujenzi wa Kituo cha Huduma za Saratani Binguni. Miradi hii inalenga kutatua changamoto za muda mrefu katika sekta za ardhi, maji na afya pamoja na kuimarisha upatikanaji wa huduma muhimu kwa wananchi. <br />
<br />
ix. Kuratibu na kutekeleza itifaki ya mikutano ya Mheshimiwa Rais na mabalozi na wajumbe kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Marekani, Saudi Arabia, Ufaransa, Oman, Canada, India na Brazil, kwa lengo la kukuza ushirikiano wa kimkakati na kuvutia uwekezaji. Katika mikutano hii, majadiliano yamelenga sekta za kipaumbele zikiwemo miundombinu, utalii, afya, elimu, uchumi wa buluu na biashara. Majadiliano hayo yalisisitiza upatikanaji wa fursa za uwekezaji, misaada ya maendeleo na uhamishaji wa teknolojia. Aidha, mikutano hiyo imeimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kuongeza imani ya washirika wa kimataifa na kufungua fursa mpya za maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa Zanzibar. Kiambatanisho nambari 09 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
x. Kusimamia utayarishaji, urushaji na utangazaji wa shughuli za kila siku zinazotekelezwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi kupitia vyombo vya habari vikiwemo ZBC TV na Redio, Channel Ten, ITV, TBC Taifa, ZCTV na Azam TV. 10 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 xi. Kuimarisha mawasiliano kati ya Mheshimiwa Rais na wananchi kupitia mitandao ya kijamii iliyofikia maelfu ya watembeleaji “Followers” (Facebook yenye watembeleaji 114,063, Instagram 378,000 na Whatsapp 47,467). <br />
<br />
xii. Kupitia Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR), Afisi imepokea malalamiko 5,266 kati ya hayo, malalamiko 4,593 sawa na asilimia 87.2 yamepatiwa ufumbuzi, na malalamiko 673 sawa na asilimia 12.8 yakiendelea kufuatiliwa kwa kushirikiana na taasisi husika ili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. xiii. Kuandaa na kurusha hewani vipindi 36 kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar kwa lengo la kuonesha ushuhuda wa utatuzi wa changamoto za wananchi zinazowasilishwa kupitia Mfumo wa Sema na Rais, jambo lililoshajihisha wananchi kutumia mfumo huo. <br />
<br />
xiv.Kutoa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa SNR kwa wananchi 2,518 kutoka shehia 44 za Unguja na Pemba. Kiambatanisho nambari 10 kina taarifa zaidi. ii. Programu Kuu ya Kuratibu Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. <br />
<br />
31. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 307.02 Milioni sawa na asilimia 47.81 ya makadirio ya TZS. 642.19 Milioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 37.22 ya makadirio ya TZS. 824.88 Milioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo mbili zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kikanda na kimataifa imetumia TZS. 275.52 Milioni sawa na asilimia 53.59 ya makadirio ya kutumia TZS. 514.15 Milioni kwa kipindi cha tathmini; na b) Programu ndogo ya Uratibu Shughuli za Wazanzibari wanaoishi nje ya nchi imetumia TZS. 31.50 Milioni sawa na 11 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 asilimia 24.60 ya makadirio ya kutumia TZS.128.04 Milioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
32. Mheshimiwa Spika, Kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: <br />
<br />
i. Kuratibu ushiriki wa Zanzibar katika Mikutano ya Jumuiya za Kikanda (EAC, SADC, AfCFTA, IORA) na ushirikiano wa Kimataifa kwa ajili ya utatuzi wa changamoto na upatikanaji wa fursa kwa Zanzibar. <br />
<br />
ii. Afisi imeshiriki Vikao na Mikutano 17 ya Jumuiya za Kikanda za EAC, SADC na AfCFTA ndani na nje ya nchi. Lengo la vikao na mikutano hiyo ni upatikanaji wa fursa na kuwajengea uwezo wadau katika kukuza sekta muhimu za Uchumi ikiwemo Uchumi wa buluu, uwekezaji, Biashara na Ujasiriamali Kiambatanisho nambari 11 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
iii. Afisi imetoa mafunzo ya Vikwazo Visivyo vya Kodi (NTBs) kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa wataalamu 32 kutoka Kamati ya NTBs ya Zanzibar, Wafanya Biashara na watendaji kutoka Jumuiya ya Wafanya Biashara Zanzibar. Mafunzo hayo yalilenga kuimarisha uelewa kuhusu dhana na athari za Vikwazo Visivyo vya Kodi katika biashara na kujenga uwezo wa washiriki katika kutambua na kushughulikia vikwazo hivyo kwa ufanisi. iv. Kuratibu shughuli 128 za Itifaki ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na kuratibu safari saba za Viongozi Wakuu wastaafu nje ya nchi. <br />
<br />
v. Kushiriki mikutano mitano (5) inayohusiana na masuala ya Diaspora ikiwemo mikutano ya taarifa za wahamaji (Data Migration), ubidhaishwaji wa lugha ya Kiswahili pamoja na vikao vya mashirikiano baina ya Afisi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kiambatanisho nambari 12 kinataarifa zaidi. 12 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 vi. Uzinduzi wa Mfumo rasmi wa Usajili wa Diaspora wa Zanzibar (mwezi Januari 2026), unaoiwezesha Serikali kupata takwimu halisi za Diaspora wa Zanzibar ikiwemo nchi wanazoishi, taaluma na ujuzi, biashara na uwekezaji kwa lengo la kushirikiana katika maswala ya Uchumi, fursa na maendeleo. Hadi kufikia mwezi Machi, 2026, Afisi imesajili Diaspora 1,360 kutoka mataifa mbali mbali duniani. Aidha, kwa kipindi hicho Disapora 423 Wameshapatiwa vitambulisho vyao (Wanaume 257 na Wanawake 166). <br />
<br />
vii. Afisi imeratibu maombi 17 ya vibali vya kazi na maombi 22 ya vibali vya ukaazi kwa Diaspora ambao wanahitaji kukaa nchini na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi. <br />
<br />
viii. Afisi kwa kushirikiana na Jumuiya ya Diaspora Al Amana Foundation kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), imeratibu utoaji wa sadaka ya futari kwa familia zaidi ya 1200 yenye thamani TZS.100.00 Milioni na kuwalipia faini na fidia yenye thamani ya TZS. 18.4 Milioni kwa Wanafunzi 18 walioachiwa huru na kutoa msaada wa magodoro 170 kwa ajili ya Chuo cha Mafunzo. <br />
<br />
ix. Afisi kwa kushirikiana na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Zanzibar na Chuo cha Mafunzo imeratibu mafunzo ya imani kwa Wanafunzi 18 wa Chuo cha Mafunzo walioachiwa huru. <br />
<br />
x. Afisi iliratibu na kushiriki katika zoezi la utoaji wa misaada ya kijamii kwa familia 600 yenye thamani ya zaidi ya TZS. 43.75 Milioni kisiwani Pemba. Misaada hiyo ilitolewa na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Oman (TADIO), Al Wadood Charitable Group na Taasisi ya Diaspora Charity Organization za nchini Oman. <br />
<br />
xi. Afisi kwa kushirikiana na Afisi ya Mufti wa Zanzibar imeratibu uingizwaji wa kontena la sadaka liloletwa na Jumuiya ya Diaspora Ifraj Zanzibar Foundation iliyopo Umoja wa 13 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 Falme za Kiarabu (UAE). Sadaka hio iliwanufaisha familia (668 - Unguja na 5,350 – Pemba) na yenye thamani ya TZS. 377.16 Milioni. <br />
<br />
xii. Afisi ilifanikiwa kukusanya TZS. 13.15 Milioni kutoka Diaspora wa Zanzibar Duniani kwa ajili ya utoaji wa Sadaka katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Sadaka hio walipatiwa watoto 382 ikiwemo mayatima na wenye mahitaji maalum kwa Unguja na Pemba. xiii. Afisi imeratibu programu ya TOKTEN (Tranfer of Knowlegde Through Expatriate Nationals) kwa Wizara na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Wataalam wawili (02) kutoka jamii ya Diaspora (Uingereza na Afrika Kusini) walibadilishana ujuzi na uzoefu kwa Wizara na Taasisi za Serikali katika masuala ya ubunifu, Akili Mnemba pamoja na usimamizi wa huduma za maji safi na salama kwa jamii. <br />
<br />
xiv. Afisi imefanya vikao viwili (02) vya majadiliano na Diaspora, vikao hivyo vilikutanisha wanadiaspora na taasisi husika zinazotoa huduma kwa Diaspora ambapo wanadiaspora walipata fursa ya kueleza changamoto zao na kutatuliwa. Lengo la vikao hivyo ni kuweka mfumo endelevu wa mawasiliano na kuimarisha uhusiano wa Diaspora na nchi yao ya asili. <br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Afisi ya Rais – Ikulu. 33. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 3.75 Bilioni sawa na asilimia 37.00 ya makadirio ya TZS. 10.13 Bilioni Kwa kipindi cha tathmini na asilimia 28.24 ya makadirio ya TZS. 13.27 Bilioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo nne zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu na Usimamizi wa Afisi ya Rais Ikulu imetumia TZS.1.31 Bilioni sawa na asilimia 76.92 ya makadirio ya kutumia TZS. 1.697 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. 14 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
b) Programu ndogo ya Uratibu wa shughuli za Mipango, Sera na Utafiti imetumia TZS.1.59 Bilioni sawa na asilimia 22.80 ya makadirio ya kutumia TZS. 6.98 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
c) Programu ndogo ya Uratibu na Usimamizi wa Afisi ya Rais Ikulu Pemba imetumia TZS. 733.81 Milioni sawa na asilimia 64.68 ya makadirio ya kutumia TZS. 1.13 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
d) Programu ndogo ya Usimamizi wa Usalama wa Serikali imetumia TZS. 117.00 Milioni sawa na asilimia 36.84 ya makadirio ya kutumia TZS. 317.61 Milioni kwa kipindi cha tathmini. 34. Mheshimiwa Spika, kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: <br />
<br />
i. Kuandaa Kanuni za Utoaji wa Tunzo (Nishani) 2025 chini ya Sheria ya mambo ya Rais. Nam. 3 ya mwaka 2020. <br />
<br />
ii. Kuratibu na kusimamia utoaji wa stahiki kwa watumishi kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma kwa lengo la kuongeza hamasa katika utekelezaji wa majukumu ya kazi. <br />
<br />
iii. Kufanya ukaguzi wa kipindi cha robo ya nne ya Mwaka wa Fedha 2024/2025, sambamba na ukaguzi wa robo ya kwanza, ya pili na ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, kwa lengo la kutathmini utekelezaji wa shughuli, ufanisi wa matumizi ya rasilimali, pamoja na kuainisha na kushauri maeneo yanayohitaji kuimarishwa kwa kuzingatia viwango na miongozo ya ukaguzi wa ndani. <br />
<br />
iv. Kuwajengea uwezo watumishi 42 kwa kuwapatia mafunzo ya muda mrefu katika ngazi na fani zinazohitajika za elimu, pamoja na mafunzo ya muda mfupi ikiwemo Programu za kuwajengea ujuzi kazini na maandalizi ya kustaafu utumishi wa umma kwa lengo la kuimarisha 15 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 utendaji kazi. Kiambatanisho nambari 13 kinataarifa zaidi. v. Kuhakiki mali za Afisi ya Rais - Ikulu kwa kuzitambua, kuziweka thamani stahiki na kuzisajili katika Mfumo wa Usimamizi wa Mali wa Serikali. <br />
<br />
vi. Kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Afisi kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 hadi 2025/2026, kwa lengo la kupima kiwango cha utekelezaji wa malengo yaliyowekwa, kubaini mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza, na kuainisha hatua stahiki za kuimarisha utendaji. <br />
<br />
vii. Kufanya tathmini ya utendaji wa Afisi ya Usalama wa Serikali pamoja na hali halisi ya usalama katika Ofisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. viii. Kufanya upekuzi wa kiusalama wa awali na endelevu kwa watumishi 1,739. Hatua hii imeimarisha uadilifu na uaminifu miongoni mwa watumishi wa umma, hususan katika nafasi nyeti, na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa vihatarishi vya kiusalama vinavyoweza kujitokeza. <br />
<br />
ix. Kufanya ukaguzi wa miundombinu na majengo ya Serikali kumi na moja (11), pamoja na mifumo ya TEHAMA katika taasisi tatu (3) za Serikali. Ukaguzi huu umewezesha kutathmini hali ya usalama wa nyaraka, taarifa, maeneo ya kazi na ufanisi wa mifumo ya utoaji huduma. <br />
<br />
x. Kutoa mafunzo maalum ya kiusalama kwa wateule 78. Mafunzo yalilenga kuongeza uelewa wao wa kiusalama, kuimarisha utendaji katika majukumu yao na kudumisha nidhamu. <br />
<br />
xi. Kutoa mafunzo maalumu ya kiusalama katika mifumo ya TEHAMA na vifaa vya kielektroniki kwa taasisi tatu (03) za Serikali, mafunzo yalilenga kuimarisha uelewa 16 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 wa watumishi, utendaji wao na kuhakikisha usalama wa matumizi ya mifumo muhimu ya kiserikali. <br />
<br />
xii. Kutoa mafunzo kwa watumishi wa umma kwa taasisi 32. Mafunzo haya yalilenga kuimarisha uelewa wa watumishi juu dhana ya usalama serikalini. xiii. Kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na uratibu kwa waajiriwa wapya na wateule wa Rais. Shughuli hizi zinaweka msingi mzuri wa kudhibiti rasilimali watu na kuimarisha usalama, huku zikiwa na lengo la kuongeza ufanisi wa GSO katika kipindi kijacho. <br />
<br />
xiv. Kufuatilia ahadi za Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika miradi ya maendeleo kwa upande wa Pemba. Ahadi hizo zimejumuisha Miradi ya Maendeleo ya Ujenzi wa Barabara ya Ukutini – Mtangani, Finya – Kicha, Chuo cha Mwalimu Nyerere Tawi la Pemba, Dahalia ya Skuli ya Sekondari ya Kiwani na Fidel Castro. <br />
<br />
xv. Kutoa mafunzo ya Sera na Sheria ya Diaspora kwa masheha 32 wa Wilaya ya Chake Chake Pemba. Lengo la mafunzo hayo ni kujenga uelewa kwa masheha juu ya namna kufahamu fursa na huduma wanazopewa Diaspora na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. <br />
<br />
xvi. Kuandaa na kurusha vipindi vinne (4) vinavyoonesha uwajibikaji wa Serikali ya awamu ya nane kwa jamii kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii Pemba. UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MIRADI YA MAENDELEO <br />
<br />
35. Mheshimiwa Spika, Kwa kipindi cha miezi tisa, Afisi ya Rais - Ikulu ilipangiwa TZS. 6.70 Bilioni kwa utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Miradi hiyo ni Mradi wa Uimarishaji wa majengo ya Ikulu, Mradi wa Uimarishaji Mawasiliano ya Mfumo wa Sema na Rais na Mradi wa Uimarishaji wa 17 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 Mfumo wa Ulinzi na Usalama katika Majengo ya Ikulu na Makaazi ya Mheshimiwa Rais. Hadi kufikia Machi 2026, Afisi imeingiziwa TZS. 1.37 Bilioni sawa na asilimia 20.46. 36. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kupitia shughuli za miradi ya maendeleo, Afisi imetekeleza yafuatayo: i. Kufanya ukarabati wa majengo ya Ikulu Ndogo ya Dodoma na Ikulu Ndogo ya Laibon Dar es salaam ikiwemo uwekaji wa paving stone na curb stone mpya katika maeneo ya ndani ya Ikulu. <br />
<br />
ii. Kuimarisha mifumo ya ulinzi katika Ikulu Ndogo ya Pagali kwa kuweka kamera za uangalizi (CCTV), pamoja na uzio wa umeme, kwa lengo la kuongeza kiwango cha usalama na ulinzi wa eneo hilo. <br />
kuu wa Serikali, kwa lengo la kuimarisha ufanisi, hadhi na weledi katika utekelezaji wa majukumu ya kiutawala<br />
iii. Kuweka lifti katika Ikulu ya Mnazi Mmoja ili kuimarisha upatikanaji wa huduma na kurahisisha ufikiaji wa maeneo ya ofisi, hususan kwa wageni wanaofika kushiriki vikao na mikutano na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hatua inayochangia kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutawala na hadhi ya mazingira ya kikazi. <br />
<br />
iv. Kununua vitendea kazi vinavyohitajika katika kutoa huduma kwa Uongozi, ikiwemo vifaa vya kisasa vya uendeshaji wa mikutano, mifumo ya sauti (PA system), vifaa vya TEHAMA, mifumo ya mawasiliano ya ndani, pamoja na vifaa maalum vya mapokezi na mikutano ya viongozi wa]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-08T12:20:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi ameshiriki Dua ya kumuombea Sheikh Abuubakar Al&#45;Abassy, na kutoa pole kwa Familia ya Waziri Nadir Al&#45;Wardi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-ameshiriki-dua-ya-kumuombea-sheikh-abuubakar-al-abassy-na-kutoa-pole-kwa-familia-ya-waziri-nadir-al-wardi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-ameshiriki-dua-ya-kumuombea-sheikh-abuubakar-al-abassy-na-kutoa-pole-kwa-familia-ya-waziri-nadir-al-wardi#When:15:43:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika dua maalum ya kumuombea marehemu Sheikh Abuubakar bin Said Al-Abassy. Dua hiyo imesomwa leo, tarehe 02 Mei 2026, katika Ukumbi wa Majid uliopo Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-02T15:43:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt Hussein Ali Mwinyi  ameyakaribisha Makampuni na Wawekezaji wa Uturuki  kuwekeza Nchini hususan  katika Maeneo ya Biashara, Nishati na  Miundombinu</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-ameyakaribisha-makampuni-na-wawekezaji-wa-uturuki-kuwekeza-nchini-hususan-katika-maeneo-ya-biashara-nishati-na-miundombinu</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-ameyakaribisha-makampuni-na-wawekezaji-wa-uturuki-kuwekeza-nchini-hususan-katika-maeneo-ya-biashara-nishati-na-miundombinu#When:15:24:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi  ameyakaribisha Makampuni na Wawekezaji wa Uturuki  kuwekeza Nchini hususan  katika Maeneo ya Biashara ,Nishati na  Miundombinu.Rais Dķt,  ameyasema hayo leo tarehe 2 Mei 2026 alipokutana na  Mkurugenzi Mkuu wa anayeshughulikia Masuala ya Afrika Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo Balozi Volkan Isikci akiamabatana na Balozi wa Uturuki Tanzania  Balozi Bekir Geze waliofika Ikulu, Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-02T15:24:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Mwinyi Atangaza ongezeko la Mshahara kima cha Chini  ni Sh. 500,000</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-atangaza-ongezeko-la-mshahara-kima-cha-chini-ni-sh-500000</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-atangaza-ongezeko-la-mshahara-kima-cha-chini-ni-sh-500000#When:12:52:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka shilingi 300,000 hadi shilingi 500,000 kwa mwezi. Rais Dkt. Mwinyi ametangaza ongezeko hilo la mshahara leo, tarehe 01 Mei 2026, katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Maonesho ya Kilimo Kizimbani, Mkoa wa Mjini Magharibi.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-01T12:52:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Mwinyi amepokea Ripoti ya CAG Zanzibar ya mwaka 2024 &#45; 2025.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-amepokea-ripoti-ya-cag-zanzibar-ya-mwaka-2024-2025</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-mwinyi-amepokea-ripoti-ya-cag-zanzibar-ya-mwaka-2024-2025#When:14:44:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar (CAG) ya mwaka 2024–2025. Ripoti hiyo imewasilishwa leo, tarehe 30 Aprili 2026, na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar, Dkt. Othman Abbas Ali, katika hafla iliyofanyika Ikulu, Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-30T14:44:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt.Mwinyi amesema Zanzibar itaendelea kushirikiana na Ireland.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amesema-zanzibar-itaendelea-kushirikiana-na-ireland</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amesema-zanzibar-itaendelea-kushirikiana-na-ireland#When:14:41:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu na Ireland, hususan katika sekta za uwekezaji, biashara, uchumi wa buluu, utalii na ustawi wa jamii.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-30T14:41:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt.Mwinyi amekabidhi Kombe la Muungano 2026 kwa timu ya Simba Sport Club ya Dar es Salaam</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amekabidhi-kombe-la-muungano-2026-kwa-timu-ya-simba-sport-club-ya-dar-es-salaam</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amekabidhi-kombe-la-muungano-2026-kwa-timu-ya-simba-sport-club-ya-dar-es-salaam#When:20:22:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza maelfu ya mashabiki wa soka kushuhudia mchezo wa fainali wa Ligi ya Muungano kati ya Simba na Yanga, uliochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 29 Aprili 2026. Timu ya Simba imefanikiwa kulitwaa kombe la michuano hiyo baada ya kuilaza Yanga kwa bao moja kwa sifuri, lililofungwa na mchezaji Selemani Mwalimu katika dakika ya 120 ya mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, kufuatia sare ya bila kufungana katika dakika 90 za kawaida.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-29T20:22:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Serikali zote Mbili za SMZ na SMT zitaendeleza na kuweka &amp;nbsp; Mkazo maalum wa kumaliza Changamoto za Muungano ambazo bado hazijapatiwa Ufumbuzi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-zote-mbili-za-smz-na-smt-zitaendeleza-na-kuweka-mkazo-maalum-wa-kumaliza-changamoto-za-muungano-ambazo-bado-hazijapatiwa-ufumbuzi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/serikali-zote-mbili-za-smz-na-smt-zitaendeleza-na-kuweka-mkazo-maalum-wa-kumaliza-changamoto-za-muungano-ambazo-bado-hazijapatiwa-ufumbuzi#When:13:16:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali zote Mbili za SMZ na SMT zitaendeleza na kuweka   Mkazo maalum wa kumaliza Changamoto za Muungano ambazo bado hazijapatiwa Ufumbuzi. Amesema Serikali zitaendelea kuendeleza Vikao na Majadiliano  kwa lengo la kuzipatia Ufumbuzi Changamoto  ambazo bado ni Kikwazo kwa Muungano aliouelezea kuwa wa kipekee Duniani.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-26T13:16:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewahimiza waumini wa dini ya Kiislamu kuitumia vema misikiti kwa ajili ya kujadiliana na kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizopo katika jamii</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/alhaj-dkt-hussein-ali-mwinyi-amewahimiza-waumini-wa-dini-ya-kiislamu-kuitumia-vema-misikiti-kwa-ajili-ya-kujadiliana-na-kuzipatia-ufumbuzi-changamoto-zilizopo-katika-jamii</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/alhaj-dkt-hussein-ali-mwinyi-amewahimiza-waumini-wa-dini-ya-kiislamu-kuitumia-vema-misikiti-kwa-ajili-ya-kujadiliana-na-kuzipatia-ufumbuzi-changamoto-zilizopo-katika-jamii#When:13:58:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewahimiza waumini wa dini ya Kiislamu kuitumia vema misikiti kwa ajili ya kujadiliana na kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizopo katika jamii. Alhaj. Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 24 Aprili 2026, alipojumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa iliyoambatana na ufunguzi wa Msikiti Mpya wa Jamaa Nour uliopo Boshowa, Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-24T13:58:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza uboreshaji wa Mfumo wa Viza Kidigitali pamoja na uimarishaji wa Usalama Nchini</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amesisitiza-uboreshaji-wa-mfumo-wa-viza-kidigitali-pamoja-na-uimarishaji-wa-usalama-nchini</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amesisitiza-uboreshaji-wa-mfumo-wa-viza-kidigitali-pamoja-na-uimarishaji-wa-usalama-nchini#When:11:22:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishauri Wizara ya Mambo ya Ndani kuimarisha mfumo wa utoaji wa viza kwa njia ya kidigitali ili huduma hiyo ipatikane kwa haraka kwa wageni wanaoingia nchini. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 24 Aprili 2026, alipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Patrobas Katambi, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-24T11:22:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshiriki hafla ya uwasilishaji wa Ripoti ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-ameshiriki-hafla-ya-uwasilishaji-wa-ripoti-ya-uchunguzi-wa-matukio-ya-uvunjifu-wa-amani-yaliyotokea-wakati-na-baada-ya-uchaguzi-mkuu-wa-oktoba-2025</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-ameshiriki-hafla-ya-uwasilishaji-wa-ripoti-ya-uchunguzi-wa-matukio-ya-uvunjifu-wa-amani-yaliyotokea-wakati-na-baada-ya-uchaguzi-mkuu-wa-oktoba-2025#When:14:00:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshiriki hafla ya uwasilishaji wa Ripoti ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, hafla iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-23T14:00:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt.Mwinyi amesisitiza SMZ kuimarisha huduma na Elimu kuhusu Usonji</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amesisitiza-smz-kuimarisha-huduma-na-elimu-kuhusu-usonji</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amesisitiza-smz-kuimarisha-huduma-na-elimu-kuhusu-usonji#When:12:44:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Usonji kwa watoto ni changamoto kubwa ya kijamii inayohitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na wadau mbalimbali katika kuwatambua na kuwasaidia watoto wanaoathirika. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 20 Aprili 2026, alipokutana na viongozi wa Lukiza Autism Foundation waliomtembelea Ikulu Zanzibar kwa lengo la kujitambulisha na kueleza shughuli za taasisi yao. Amesema changamoto ya Usonji inachangiwa na uelewa mdogo wa jamii pamoja na uhaba wa wataalamu wa fani hiyo, hivyo Serikali inaendelea kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha wataalamu wanapatikana na elimu inaongezwa kwa wananchi.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-20T12:44:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Giuseppe Sean Coppola Ikulu Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amekutana-na-balozi-wa-italia-nchini-tanzania-mhe-giuseppe-sean-coppola-ikulu-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amekutana-na-balozi-wa-italia-nchini-tanzania-mhe-giuseppe-sean-coppola-ikulu-zanzibar#When:11:00:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amemshukuru Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Giuseppe Sean Coppola, kwa kuendelea kuimarisha uhusiano wa kihistoria na kidiplomasia kati ya Zanzibar na Italia, hususan katika sekta ya utalii na utamaduni. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Balozi huyo Ikulu Zanzibar, akiwa na Balozi Mdogo wa Heshima wa Italia Zanzibar, Stephano Totisco.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-20T11:00:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt.Mwinyi amekutana na Uongozi wa EcoBank.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amekutana-na-uongozi-wa-ecobank</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt.mwinyi-amekutana-na-uongozi-wa-ecobank#When:10:03:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na uongozi wa Benki ya Ecobank, ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Biashara na Uwekezaji kutoka makao makuu ya benki hiyo nchini Togo, Bw. Michael Larbie, aliyefuatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Ecobank Tanzania, Ndugu Charles Asiedu, leo tarehe 15 Aprili 2026, Ikulu Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-15T10:03:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi amekagua Mradi wa Mji wa Afcon Fumba na kuangalia maendeleo ya Uwanja.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amekagua-mradi-wa-mji-wa-afcon-fumba-na-kuangalia-maendeleo-ya-uwanja</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amekagua-mradi-wa-mji-wa-afcon-fumba-na-kuangalia-maendeleo-ya-uwanja#When:09:33:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameutembelea mradi wa Mji wa AFCON Fumba uliopo Mkoa wa Mjini Magharibi. Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 14 Aprili 2026, akiambatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembe Juma, pamoja na wadau wa mradi wa AFCON Fumba Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-14T09:33:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt.Mwinyi amewaapisha wakuu wa Wilaya wapya aliowateuwa hivi karibuni.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amewaapisha-wakuu-wa-wilaya-wapya-aliowateuwa-hivi-karibuni</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amewaapisha-wakuu-wa-wilaya-wapya-aliowateuwa-hivi-karibuni#When:10:14:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaapisha Wakuu wa Wilaya aliowateua hivi karibuni. Hafla hiyo ya uapisho imefanyika leo tarehe 13 Aprili 2026, Ikulu Zanzibar, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama pamoja na wanafamilia wa Wakuu wa Wilaya walioapishwa.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-13T10:14:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) ili kuhakikisha mafanikio zaidi yanapatikana katika kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-zanzibar-itaendelea-kushirikiana-na-shirika-la-afya-duniani-who-ili-kuhakikisha-mafanikio-zaidi-yanapatikana-katika-kuimarisha-utoaji-wa-huduma-za-afya-nchini</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-zanzibar-itaendelea-kushirikiana-na-shirika-la-afya-duniani-who-ili-kuhakikisha-mafanikio-zaidi-yanapatikana-katika-kuimarisha-utoaji-wa-huduma-za-afya-nchini#When:12:01:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) ili kuhakikisha mafanikio zaidi yanapatikana katika kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 09 Aprili 2026 alipokutana na ujumbe wa wataalamu kutoka Shirika la Afya Duniani, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Shirika hilo Kanda ya Afrika, Profesa. Mohamed Yakub Janabi, waliowasili Ikulu Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-09T12:01:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekihakikishia Chama cha Mawakili Zanzibar kuwa Serikali inathamini na kuunga mkono kazi nzuri inayofanywa na taasisi hiyo ya kuwasaidia wananchi katika masuala ya kisheria.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amekihakikishia-chama-cha-mawakili-zanzibar-kuwa-serikali-inathamini-na-kuunga-mkono-kazi-nzuri-inayofanywa-na-taasisi-hiyo-ya-kuwasaidia-wananchi-katika-masuala-ya-kisheria</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amekihakikishia-chama-cha-mawakili-zanzibar-kuwa-serikali-inathamini-na-kuunga-mkono-kazi-nzuri-inayofanywa-na-taasisi-hiyo-ya-kuwasaidia-wananchi-katika-masuala-ya-kisheria#When:09:34:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekihakikishia Chama cha Mawakili Zanzibar kuwa Serikali inathamini na kuunga mkono kazi nzuri inayofanywa na taasisi hiyo ya kuwasaidia wananchi katika masuala ya kisheria. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 09 Aprili 2026, alipokutana na uongozi wa Chama cha Mawakili Zanzibar ulioongozwa na Rais wa chama hicho, Wakili Joseph Shaban Magazi, waliofika Ikulu, Zanzibar.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-09T09:34:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi amewasisitiza Mabalozi kukuza Diplomasia ya Uchumi Kimataifa.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amewasisitiza-mabalozi-kukuza-diplomasia-ya-uchumi-kimataifa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-amewasisitiza-mabalozi-kukuza-diplomasia-ya-uchumi-kimataifa#When:11:49:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasisitiza mabalozi wanaoenda kuiwakilisha Tanzania katika mataifa mbalimbali kuweka kipaumbele katika kuzingatia diplomasia ya kiuchumi kwa kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini.Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 08 Aprili 2026, alipokutana na mabalozi hao waliofika Ikulu, Zanzibar, kumuaga kabla ya kwenda katika vituo vyao vya kazi.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-08T11:49:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi ameongoza Dua ya kumuenzi Hayati Karume.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-ameongoza-dua-ya-kumuenzi-hayati-karume</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-ameongoza-dua-ya-kumuenzi-hayati-karume#When:11:53:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza viongozi wa kitaifa, wanafamilia na wananchi mbalimbali katika dua maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.Du a hiyo imefanyika leo, tarehe 07 Aprili 2026, katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar, Mkoa wa Mjini Magharibi, ambapo pia imehudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba,  Mama Fatma Karume na familia yake, Viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-07T11:53:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Alhaj Dkt.Hussein Mwinyi,amejumuika na wanafamilia, Viongozi wa Serikali katika dua maalum ya kumuombea Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/alhaj-dkt.hussein-mwinyiamejumuika-na-wanafamilia-viongozi-wa-serikali-katika-dua-maalum-ya-kumuombea-rais-wa-awamu-ya-pili-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-hayati-mzee-ali-hassan-mwinyi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/alhaj-dkt.hussein-mwinyiamejumuika-na-wanafamilia-viongozi-wa-serikali-katika-dua-maalum-ya-kumuombea-rais-wa-awamu-ya-pili-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-hayati-mzee-ali-hassan-mwinyi#When:11:02:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na wanafamilia, viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi mbalimbali katika dua maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-05T11:02:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt.Mwinyi amesema umoja wa Wananchi ni nguzo ya Amani na utulivu wa Taifa.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amesema-umoja-wa-wananchi-ni-nguzo-ya-amani-na-utulivu-wa-taifa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt.mwinyi-amesema-umoja-wa-wananchi-ni-nguzo-ya-amani-na-utulivu-wa-taifa#When:13:56:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kulinda na kudumisha amani, umoja na mshikamano nchini, akihimiza wananchi kuondoa ubaguzi na kuimarisha upendo katika jamii. Amesema umoja wa wananchi ni msingi muhimu wa utulivu wa Taifa, na kila mmoja ana wajibu wa kulinda tunu hizo kwa vitendo.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-03T13:56:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Watanzania  wana Wajibu muhimu wa kuhakikisha Muungano wa Tanzania Amani, Utulivu na Umoja wa kitaifa vinalindwa kuimarishwa</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-watanzania-wana-wajibu-muhimu-wa-kuhakikisha-muungano-wa-tanzania-amani-utulivu-na-umoja-wa-kitaifa-vinalindwa-kuimarishwa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-watanzania-wana-wajibu-muhimu-wa-kuhakikisha-muungano-wa-tanzania-amani-utulivu-na-umoja-wa-kitaifa-vinalindwa-kuimarishwa#When:14:46:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Watanzania  wana Wajibu muhimu wa kuhakikisha Muungano wa Tanzania  Amani, Utulivu na Umoja wa kitaifa vinalindwa ,Kuimarishwa na Kudumishwa. Rais Dķt, ameyasema hayo leo tarehe 2 Aprili 2026  katika Uzinduzi wa Kitaifa wa Mbio  za Mwenge wa Uhuru uliofanyika Uwanja wa  Gombani,  Mkoa wa Kusini ,Pemba. Rais Dķt Mwinyi amefahamisha kuwa  Serikali zote mbili ,Taasisi za Dini,Asasi za kiraia ,Vyombo vya Habari na Wananchi wana Wajibu wa kulinda Misingi ya Utu na kuheshimu Utawala wa Sheria ili kuwa na Taifa  linalosimamia Haki,Usawa ,Umoja, ,Utulivu na Mshikamano wa kitaifa.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-02T14:46:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza uhifadhi wa Maeneo ya Kihistoria na kukaribisha uwekezaji Zanzibar</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-asisitiza-uhifadhi-wa-maeneo-ya-kihistoria-na-kukaribisha-uwekezaji-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/rais-dkt-mwinyi-asisitiza-uhifadhi-wa-maeneo-ya-kihistoria-na-kukaribisha-uwekezaji-zanzibar#When:12:35:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali imeweka kipaumbele katika kuimarisha na kuhifadhi maeneo ya kihistoria kutokana na mchango wake katika uchumi na utamaduni wa Zanzibar. Akizungumza Ikulu Zanzibar leo tarehe 01 Aprili,2026 alipokutana na Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Mhe. Marjo Crompvoets, Rais Dkt. Mwinyi amesema juhudi hizo ni pamoja na ukarabati wa jengo la kihistoria la Sinema ya Majestic, unaofanyika kwa ushirikiano na Serikali ya Japan, ili kulibakisha katika muonekano wake wa asili na kuongeza matumizi yake kiutamaduni.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-04-01T12:35:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kilimo cha mwani kinaongezewa thamani na kuwanufaisha wakulima wa zao hilo</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-serikali-inaendelea-na-mikakati-mbalimbali-ya-kuhakikisha-kilimo-cha-mwani-kinaongezewa-thamani-na-kuwanufaisha-wakulima-wa-zao-hilo</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/media/view/mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amesema-serikali-inaendelea-na-mikakati-mbalimbali-ya-kuhakikisha-kilimo-cha-mwani-kinaongezewa-thamani-na-kuwanufaisha-wakulima-wa-zao-hilo#When:12:06:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kilimo cha mwani kinaongezewa thamani na kuwanufaisha wakulima wa zao hilo. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 30 Machi 2026, alipokutana na Mwenyekiti wa Kampuni ya TSC Purple Limited ya India pamoja na ujumbe wake waliofika Ikulu, Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject>News and Events,</dc:subject>
	  <dc:date>2026-03-30T12:06:00+00:00</dc:date>
	</item>

	<item>
	  <title>Hotuba ya Waziri wa Nchi Afisi ya Rais &#45; Ikulu &amp;nbsp; Mheshimiwa Dkt. Saada Mkuya Salum (MBM) kuhusu makadirio ya mapato na matumizi &amp;nbsp; kwa mwaka wa Fedha 2026/2027.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-kwa-mwaka-wa-fedha-2026-2027</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-kwa-mwaka-wa-fedha-2026-2027#When:15:55:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[YALIYOMO ORODHA YA VIAMBATANISHO .......................................................iv <br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO ................................................................vi <br />
<br />
UTANGULIZI .........................................................................................1 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YARAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ..............................................7 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU A01). ....................................................................................7 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Kusimamia na Kuratibu Shughuli na Huduma za Mheshimiwa Rais na Kuimarisha Mawasiliano Ikulu. ........8 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Kuratibu Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. .............11<br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Afisi ya Rais – Ikulu. ...............................................................................14 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MIRADI YA MAENDELEO .............17 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU A02) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. .....................18 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Majukumu ya Kikatiba na Kisheria ya BLM. ......................................................................19 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utumishi na Uendeshaji wa Ofisi ya Baraza la Mapinduzi .............................................................20 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI ZANZIBAR (FUNGU A09) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ……………………….....20 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA ZPDB (FUNGU A09) .........21<br />
<br />
 i. Programu Kuu ya Usimamizi na Uratibu wa Huduma za Serikali .......................................................................................21 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Mipango ya Miradi ya Kipaumbele na Uendeshaji. ............................................................................23 <br />
<br />
UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAENDELEO KWA FUNGU A09 ……………......24 <br />
<br />
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU ZANZIBAR (FUNGU A10) KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. ....................................25 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027<br />
<br />
ii i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Nyaraka na Kumbukumbu kwa matumizi ya Serikali na Umma. ............25<br />
<br />
 ii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu. ..............................................27 <br />
<br />
MWELEKEO WA BAJETI YA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ......................................................................27.<br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO NA MAKISIO YA FEDHA ZINAZOHITAJIKA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ...............29 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU 001) .................................................................................................30 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Shughuli za Mheshimiwa Rais na Uimarishaji wa Mawasiliano. ...................................30 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Uratibu wa Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. ................31 <br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji. ...........................32 <br />
<br />
MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOTEKELEZWA NA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027 ..................................33 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU 040). ...................................................................................34<br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Majukumu ya Kikatiba na Kisheria ya BLM. ................................................................34 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utumishi na Uendeshaji wa Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi. ..............................................................35 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU (FUNGU 057) ..........................................................36 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi wa Nyaraka na Kumbukumbu kwa Matumizi ya Serikali na Umma. .....................................36 <br />
<br />
ii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji .........................37 <br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO ZA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI (FUNGU 058) …….....38 <br />
<br />
i. Programu Kuu ya Usimamizi na Uratibu wa Miradi ya Serikali. ..................................................................................................38 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 iii ii. Programu Kuu ya Mipango ya Miradi ya Kipaumbele na Uendeshaji. ..............................................................................39 <br />
<br />
MAOMBI YA FEDHA YA KAZI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027. .....................................................40 <br />
<br />
HITIMISHO ........................................................................................40 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
iv ORODHA YA VIAMBATANISHO KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
01. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGU 001) ..44 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
02. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA OFISI YA BARAZA LA MAPINDUZI (FUNGU 040) ....................................................................................47 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.<br />
<br />
03. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI – MACHI) KWA MWAKA 2025 – 2026 KWA TAASISI YA AFISI YA RAIS YA UFUATILIAJI NA USIMAMIZI WA UTENDAJI SERIKALINI (FUNGU 058) ...............48 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 04. MUHTASARI WA MATUMIZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA MIEZI 9 (JULAI - MACHI) KWA 2025 – 2026 KWA TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU (FUNGU 057) ....................................................................................49 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 05. ORODHA YA ZIARA ZA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO. ........................................50 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 06. ORODHA YA ZIARA ZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO. ........................................51 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. 07. ORODHA YA MIKUTANO YA KIKANDA NA KIMATAIFA AMBAYO RAIS WA ZANZIBAR AMESHIRIKI......................53 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
08. ORODHA YA VIKAO VYA MHESHIMIWA RAIS WIZARA ZA KISEKTA ZA SERIKALI ...................54 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
09. ORODHA YA MABALOZI NA WAGENI MASHUHURI WA NCHI ZA NJE WALIOMTEMBELEA MHESHIMIWA RAIS....................................................56 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
10. ORODHA YA IDADI YA SHEHIA ZILZOTEMBELEWA NA WANANCHI WALIOFIKIWA KATIKA MAFUNZO YA SNR..................................................... 58 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI. <br />
<br />
11. USHIRIKI WA IDARA KATIKA MIKUTANO NA VIKAO ZA JUMUIYA ZA KIKANDA NA KIMATAIFA………………60 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.<br />
<br />
12. ORODHA YA MIKUTANO NA VIKAO YA URATIBU WA SHUGHULI ZA DIASPORA ZANZBAR. ......63 <br />
<br />
KIAMBATANISHO NAMBARI.13. <br />
<br />
ORODHA YA WATUMISHI WALIOPATIWA MAFUNZO. ............................................................. 64 <br />
<br />
v HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO <br />
<br />
AfCFTA BLM CAN CCM EAC ECDP GSO ITV IORA NTBs PAC RAMIS SADC SNR TADIO TBC TOKTEN UAE UNDP UNFPA ZASO ZBC ZCTV ZNCC ZPDB Eneo huru la Biashara Barani Afrika Baraza la Mapinduzi Climate Action Network Tanzania Chama cha Mapinduzi Jumuiya ya Afrika Mashariki Early Childhood Development Programme Afisi ya Usalama wa Serikali Independent Television Indian Ocean Rim Association Non-Tariff Barriers Kamati ya Bajeti, na Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Hesabu za Serikali Mfumo wa kielektroniki wa uhifadhi na matumizi ya nyaraka na kumbumbuku Jumiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika Sema na Rais Mwinyi Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Oman Shirika la Utangazaji la Tanzania Transfer of knowlegde through expartriete Nationals Umoja wa Falme za Kiarabu United Nations Development Programme United Nations Population Fund Zanzibar Association of Sports Officers Shirika la Utangazaji la Zanzibar Zanzibar Cable Television Zanzibar National Chamber of Commerce Taasisi ya Afisi ya Rais ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini Zanzibar. <br />
<br />
vi HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 UTANGULIZI 1. 2. 3. 4. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Naomba kutoa hoja kwamba Baraza lako lipokee na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Afisi ya Rais - Ikulu na Taasisi zake kwa Mwaka 2025/2026 na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Afisi ya Rais - Ikulu (Fungu A01), Baraza la Mapinduzi (Fungu A02), Taasisi ya Afisi ya Rais ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa utendaji Serikalini (Fungu A09), na Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu (Fungu A10) kwa mwaka 2025/2026. Mheshimiwa Spika, Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima, siha njema, amani na utulivu vinavyotuwezesha kuendelea kutekeleza majukumu yetu yanayochangia kuleta maendeleo na kujenga ustawi wa Taifa. <br />
<br />
Pia, tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana katika kipindi hiki cha Mkutano wa 03 wa Baraza la 11 kwa ajili ya kupokea utekelezaji wa Afisi ya Rais - Ikulu pamoja na kutafakari mipango ijayo katika kufikia malengo ya Nchi. Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imetekeleza jukumu lake la kikatiba kwa kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Napenda kuwapongeza wananchi wote wa Zanzibar kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo muhimu la kidemokrasia, wakitumia haki yao ya msingi kwa amani na utulivu. Vilevile, napenda kuvipongeza vyama vyote vya siasa vilivyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu, jambo linaloonesha kuimarika kwa misingi ya demokrasia nchini na ukomavu wa kisiasa miongoni mwa Watanzania. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kipekee napenda kutumia fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa imani yake kwangu na kuendelea kunipa dhamana ya kusimamia Afisi ya Rais - Ikulu, yenye jukumu kubwa la kusimamia na kuratibu utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali, kuhakikisha nidhamu na utendaji bora wa watumishi wa umma na kukuza maendeleo endelevu ya kijamii, kiuchumi 1 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 na kiutawala kwa wananchi na hatimae kuwa na Serikali yenye ufanisi na uwajibikaji kwa ustawi wa Taifa. 5. 6. 7. 8. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kwa heshima na adhama ya kipekee, napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kufuatia ushindi wa kishindo alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa Vyama Vingi uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025. Ushindi huu ni kielelezo cha imani kubwa ya wananchi kwake, pamoja na uimara wa mikakati ya kisiasa iliyosimamiwa kwa umakini na maono ya muda mrefu. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kampeni za Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi zilijengwa juu ya msingi unaogusa uhalisia wa maisha ya wananchi, kuimarisha umoja wa kitaifa, kuchochea mageuzi ya kiuchumi na kudumisha misingi ya utawala bora. Ujumbe huu uliwasilishwa kwa utulivu, umakini na mwelekeo ulioeleweka kwa urahisi, hali iliyochangia kuimarisha uungwaji mkono kutoka kwa sekta mbalimbali za jamii. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Katika kipindi chote cha kampeni, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi aliendelea kujijengea taswira ya kuwa kiongozi makini, mwenye dira iliyo wazi na anayethamini maoni ya wananchi. Uwezo wake wa kusikiliza, kuelewa na kujibu changamoto za wananchi kwa vitendo uliimarisha zaidi uhusiano wa kuaminiana kati ya uongozi na jamii. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Ushindi wake katika uchaguzi huo na hatimaye kuapishwa kwake rasmi tarehe 02 Novemba 2025, ni matokeo ya mchakato uliotekelezwa kwa nidhamu na ufanisi, ukihusisha mikakati madhubuti ya kisiasa, mawasiliano yenye ushawishi chanya, pamoja na mshikamano wa dhati kati ya chama na wananchi. Kwa ujumla, kampeni za Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi zilionesha kiwango cha juu cha ubora wa kisiasa na kimkakati. Ziliweka msingi imara wa ushindi huo na kuendelea kipindi cha pili cha awamu ya uongozi wake unaolenga kuharakisha maendeleo 2 <br />
<br />
HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 endelevu ya Zanzibar, kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na mustakabali wa taifa kwa ujumla.<br />
<br />
9. Mheshimiwa Spika, Natoa wito kwa wananchi na wadau wote kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha juhudi za maendeleo ya taifa letu. Aidha, ninawakumbusha viongozi wote waliochaguliwa kuendelea kuweka mbele maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, uwazi na kujituma katika kila nafasi waliyopewa. <br />
<br />
10. Mheshimiwa Spika, Mwaka mmoja ni kipindi kirefu katika maisha ya binadamu na mara nyingi huambatana na matukio na changamoto za maisha. Napenda kuwapa pole wananchi wote walioathiriwa na majanga yaliyotokea katika kipindi cha harakati zao za kujitafutia kipato na maisha. <br />
<br />
11. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuwa karibu na wananchi hao na itaendelea kushirikiana nao katika kukabiliana na changamoto hizo, kwa lengo la kuhakikisha wanapata msaada unaostahiki na kurejesha hali ya ustawi katika maisha yao. <br />
<br />
12. Mheshimiwa Spika, Naomba kuliahidi Baraza lako Tukufu na wananchi wote kuwa nitaendelea kutekeleza majukumu yangu kwa uadilifu, bidii na weledi mkubwa, ili kuendeleza mafanikio yaliyofikiwa na kuhakikisha kwamba Bajeti hii inasimamiwa kwa ufanisi na kutekelezwa ipasavyo. Hakika, mafanikio makuu yaliyopatikana Zanzibar yametokana na maono ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, katika kuwaletea Wazanzibari maendeleo endelevu. <br />
<br />
Tunajivunia na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kiongozi mwenye maono chanya kwa mustakabali wa Taifa letu. Naomba tuendelee kumuombea Mwenyezi Mungu amjalie afya njema, hekima, busara, na ustahimilivu katika kuliongoza Taifa letu. <br />
<br />
3 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
13. Mheshimiwa Spika, Nalikumbusha Baraza lako Tukufu kuwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameweka wazi mwelekeo mpya wa Serikali katika kipindi chake cha pili, ukiangazia mageuzi ya kiuchumi na ustawi wa wananchi. Katika hotuba yake ya uzinduzi wa Baraza la kumi na moja la Wawakilishi tarehe 10 Novemba 2025, Mheshimiwa Rais alisisitiza kuwa Serikali itajikita katika kukuza ukuaji wa uchumi kwa kutumia nguvu za uzalishaji, kuongeza uwekezaji, na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika biashara na viwanda. <br />
<br />
14. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais Mwinyi pia alibainisha umuhimu wa kuimarisha utendaji wa sekta zinazochangia ukuaji wa uchumi, kuimarisha mazingira ya kupata mtaji, na kuendeleza fursa za uwekezaji zinazovutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Mwelekeo huu mpya unalenga kuhakikisha maendeleo yanayojumuisha kila kona ya jamii; wakulima, wafanyabiashara wadogo na wakubwa, na vijana katika masuala ya ajira na ubunifu. <br />
<br />
15. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amesisitiza usalama, amani, umoja wa kitaifa, na nidhamu ya kitaalamu kama misingi ya utekelezaji wa sera za uchumi na maendeleo endelevu katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake. Serikali inalenga kujenga uchumi imara, wa kisasa, na wenye mshikamano, utakaowawezesha Wazanzibari kushindana vyema katika mazingira ya kimataifa ya kibiashara na kupata faida za moja kwa moja. <br />
<br />
16. Mheshimiwa Spika, Napenda kutoa shukrani zangu za dhati na pongezi kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake madhubuti na wa kimkakati. Ameongoza jitihada za kukuza uchumi na kuimarisha maisha ya Watanzania, akiwahusisha wakulima, wafanyabiashara, na vijana katika maendeleo. Uongozi wake umeimarisha mazingira ya uwekezaji, kuimarisha miundombinu, na kuendeleza mshikamano wa kitaifa. Aidha, juhudi za Serikali zimepanua fursa za mikopo 4 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 kwa wakulima, wavuvi, na wafugaji, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa kipato kwa wananchi. Mwelekeo huu unaonesha dhamira ya kujenga uchumi imara, wa kisasa, na unaotoa faida kwa kila mwananchi. <br />
<br />
17. Mheshimiwa Spika, Kwa moyo wa dhati napenda kumshukuru Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, kwa juhudi zake kubwa katika kuhakikisha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatekeleza majukumu yake kwa umakini. Ushirikiano wake na Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi umeimarisha ufanisi wa Serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kutoa huduma bora kwa wananchi. <br />
<br />
18. Mheshimiwa Spika, Naomba nikupongeze wewe binafsi pamoja na Naibu Spika kwa kuliongoza Baraza letu Tukufu kwa umahiri mkubwa uliodhihirika katika kufikia maamuzi yenye manufaa kwa ustawi wa wananchi, hakika mmesimama imara kuongoza Muhimili huu muhimu kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya Taifa na Mwenyezi Mungu aendelee kuwatia nguvu zaidi. Niwapongeze pia Wenyeviti wa Baraza kwa kukusaidia wewe kuongoza vyema vikao vya Baraza letu, ni dhahiri kuwa muhimili huu umetoa mchango mkubwa kwenye maamuzi ya nchi yetu. <br />
<br />
19. Mheshimiwa Spika, Nichukue nafasi hii pia kuwapongeza Mawaziri wenzangu wote wa Serikali ya Awamu ya Nane kwa kuendelea kupewa dhamana ya kuwatumikia Wazanzibari na kwa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025/2030 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050. <br />
<br />
20. Mheshimiwa Spika, Nikiwa miongoni mwa watekelezaji wa Ilani ya CCM nichukue fursa hii kuwapongeza viongozi wote walioteuliwa kushika nafasi za kumsaidia Mwenyekiti kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM. Tuendelee kushirikiana kutekeleza Ilani na miongozo mingine ya kitaifa ili kujenga Taifa letu. 5 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
21. Mheshimiwa Spika, Napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa Balozi Mhandisi Zena Ahmed Said, aliyekuwa Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha utendaji wa Serikali na kuhakikisha malengo yanafikiwa kwa ufanisi. Uongozi wake mahiri katika kusimamia watendaji wa Serikali umeacha alama muhimu ya mafanikio tunayojivunia leo. Aidha, tunampongeza kwa kuteuliwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Saudi Arabia na tunamtakia kila la kheri katika kuendelea kulitumikia Taifa katika nafasi hiyo mpya. <br />
<br />
22. Mheshimiwa Spika, Vile vile, nawashukuru kwa dhati Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi, hususan Kamati ya Kusimamia Afisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Machano Othman Said, Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini na Makamu wake Mheshimiwa Azza Januari Joseph, Mwakilishi wa Kuteuliwa kupitia nafasi Maalum za Wanawake pamoja na wajumbe wa kamati kwa ushirikiano, maelekezo na ushauri mzuri wanaotupatia ambao umetuwezesha kufanikisha utendaji wa kazi zetu. Aidha, nazishukuru Kamati ya Bajeti na Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Hesabu za Serikali (PAC), Ushirikiano, busara na maelekezo yao yamekuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha utendaji wa Serikali. <br />
<br />
23. Mheshimiwa Spika, Nichukue fursa adhimu ya kumshukuru na kumpongeza Ndugu Raya Issa Mselem, Katibu wa Baraza la Wawakilishi kwa Utendaji wake bora na mashirikiano anayonipa yeye binafsi na watendaji wengine wote wa Baraza la Wawakilishi. <br />
<br />
24. Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa kila mmoja wetu kuendelea kuiunga mkono Serikali, kudumisha mshikamano wa kitaifa, na kushiriki kikamilifu katika juhudi za kujenga Zanzibar imara yenye maendeleo jumuishi kwa ustawi wa wananchi. Ushirikiano huu ni nguzo muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo na kuhakikisha kuwa 6 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 rasilimali za taifa zinatumika kwa ufanisi na kwa manufaa ya wananchi wote. <br />
<br />
25. Mheshimiwa Spika, Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 Afisi ya Rais - Ikulu iliwasilisha mbele ya Baraza lako Tukufu, Mpango na Bajeti ya Afisi na kuomba fedha ili kutekeleza majukumu yake. Ninayo heshima kusimama tena mbele ya Baraza lako Tukufu ili niweze kutoa taarifa ya utekelezaji wa Mpango ulioombewa fedha kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 na kuwasilisha Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. <br />
<br />
26. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais - Ikulu, kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 ilijipangia kutekeleza Programu Kuu tisa (09) zenye Programu ndogo kumi na tano (15). Kiambatanisho nambari 01, 02, 03 na 04 vina maelezo ya ziada kuhusu Programu Kuu na Programu Ndogo. UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU (FUNGUA01). <br />
<br />
27. Mheshimiwa Spika, Fungu A01 limejumuisha Programu Kuu tatu na Programu Ndogo nane. Kwa kipindi cha Julai, 2025 hadi Machi 2026, fungu hili limetumia TZS. 7.94.Bilioni sawa na asilimia 51.87 ya makadirio ya TZS.15.30 Bilioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 39.52 ya makadirio ya kutumia TZS. 20.09 Bilioni kwa mwaka. Mchanganuo wa matumizi hayo ni kama ifuatavyo: a) Malipo ya Mishahara TZS. 5.06 Bilioni sawa na asilimia 98.78 ya makadirio ya TZS, 5.12 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. b) Matumizi Mengineyo TZS. 1.51 Bilioni sawa na asilimia 43.34 ya makadirio ya TZS. 3.49 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. 7 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 c) Matumizi ya Mradi wa Maendeleo TZS.1.37 Bilioni sawa na asilimia 20.46 ya makadirio ya TZS. 6.70 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
28. Mheshimiwa Spika, Fedha hizo zimetumika kutekeleza programu kuu zifuatazo: i. Programu Kuu ya Kusimamia na Kuratibu Shughuli na Huduma za Mheshimiwa Rais na Kuimarisha Mawasiliano Ikulu. <br />
<br />
29. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 3.88 Bilioni sawa na asilimia 85.67 ya makadirio ya TZS. 4.53 Bilioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 64.81 ya makadirio ya TZS. 5.99 Bilioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo mbili zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu wa Huduma za Mheshimiwa Rais imetumia TZS. 3.39 Bilioni sawa na asilimia 91.60 ya makadirio ya kutumia TZS.3.70 Bilioni kwa kipindi cha tathmini; na b) Programu ndogo ya Kuimarisha Mawasiliano baina ya Serikali na Wananchi imetumia TZS. 492.89 Milioni sawa na asilimia 59.27 ya makadirio ya kutumia TZS. 831.63 Milioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
30. Mheshimiwa Spika, kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: i. Kutoa ushauri kwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika masuala ya siasa, uchumi, jamii, sheria, diplomasia, mawasiliano na habari, pamoja na uhusiano wa kikanda na kimataifa, na masuala mengine muhimu. <br />
<br />
ii. Kusimamia ratiba ya kila siku ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kuhakikisha kwamba shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa mipango iliyowekwa na kwa ufanisi unaotarajiwa. 8 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
iii. Ziara nane (08) za ukaguzi wa miradi ya maendeleo ndani ya visiwa vya Zanzibar zimefanyika. Ziara hizi zimehusu ukaguzi wa miradi katika sekta ya elimu, afya, michezo, maji, miundombinu na kilimo, kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji wake unakidhi viwango vinavyotarajiwa, kutumia rasilimali kwa ufanisi na kutoa mapendekezo ya kuimarisha miradi hii ili kufanikisha maendeleo endelevu kwa wananchi. Kiambatanisho nambari 05 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
iv. Kuratibu uzinduzi wa miradi kumi na nane (18) mikubwa, miradi ambayo ina faida za moja kwa moja kwa wananchi katika sekta ya elimu, afya, maji, nishati na miundombinu. Miradi hii inalenga kuimarisha huduma za jamii, kuongeza fursa za kiuchumi, na kuhakikisha maendeleo endelevu yanayogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Kiambatanisho nambari 06 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
v. Kuratibu ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika mikutano minne (04) ya kikanda na kimataifa yenye lengo la kukuza ushirikiano wa kibiashara, uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi. Mikutano hii imejumuisha Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika, Mkutano wa Usajili Barani Afrika na Mkutano wa Uhakiki wa Rasimu ya Mkakati wa kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji. Ushiriki huu umehusisha mazungumzo na wadau mbalimbali, kutafuta fursa za uwekezaji, kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kushirikiana katika miradi ya maendeleo, ili kuhakikisha Zanzibar inapata faida za kiuchumi na kimaendeleo. Kiambatanisho nambari 07 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
vi. Kuratibu na kuendesha vikao 22 vya kiserikali. Vikao hivi vilitumika kutoa maelekezo ya kiutendaji kwa wizara na taasisi 17 za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kupitia vikao hivi, Mheshimiwa Rais amesisitiza uwajibikaji na nidhamu katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali. Kiambatanisho nambari 08 kina taarifa zaidi. 9 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 vii.Kuratibu na kufanikisha shughuli ya kutunuku Nishani ya Mapinduzi na Nishani ya Utumishi Uliotukuka kwa viongozi na wananchi 18 wenye sifa maalum, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika historia, maendeleo na ustawi wa Zanzibar. viii.Kuratibu hafla ya utiaji saini wa mikataba ya miradi mitatu mikubwa ya kimkakati iliyofanyika Ikulu Zanzibar, ikiwemo mradi wa Mfumo Jumuishi wa Usimamizi na Usajili wa Huduma za Ardhi, Mradi wa Usambazaji Maji Kusini Unguja na ujenzi wa Kituo cha Huduma za Saratani Binguni. Miradi hii inalenga kutatua changamoto za muda mrefu katika sekta za ardhi, maji na afya pamoja na kuimarisha upatikanaji wa huduma muhimu kwa wananchi. <br />
<br />
ix. Kuratibu na kutekeleza itifaki ya mikutano ya Mheshimiwa Rais na mabalozi na wajumbe kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Marekani, Saudi Arabia, Ufaransa, Oman, Canada, India na Brazil, kwa lengo la kukuza ushirikiano wa kimkakati na kuvutia uwekezaji. Katika mikutano hii, majadiliano yamelenga sekta za kipaumbele zikiwemo miundombinu, utalii, afya, elimu, uchumi wa buluu na biashara. Majadiliano hayo yalisisitiza upatikanaji wa fursa za uwekezaji, misaada ya maendeleo na uhamishaji wa teknolojia. Aidha, mikutano hiyo imeimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kuongeza imani ya washirika wa kimataifa na kufungua fursa mpya za maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa Zanzibar. Kiambatanisho nambari 09 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
x. Kusimamia utayarishaji, urushaji na utangazaji wa shughuli za kila siku zinazotekelezwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi kupitia vyombo vya habari vikiwemo ZBC TV na Redio, Channel Ten, ITV, TBC Taifa, ZCTV na Azam TV. 10 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 xi. Kuimarisha mawasiliano kati ya Mheshimiwa Rais na wananchi kupitia mitandao ya kijamii iliyofikia maelfu ya watembeleaji “Followers” (Facebook yenye watembeleaji 114,063, Instagram 378,000 na Whatsapp 47,467). <br />
<br />
xii. Kupitia Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR), Afisi imepokea malalamiko 5,266 kati ya hayo, malalamiko 4,593 sawa na asilimia 87.2 yamepatiwa ufumbuzi, na malalamiko 673 sawa na asilimia 12.8 yakiendelea kufuatiliwa kwa kushirikiana na taasisi husika ili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. xiii. Kuandaa na kurusha hewani vipindi 36 kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar kwa lengo la kuonesha ushuhuda wa utatuzi wa changamoto za wananchi zinazowasilishwa kupitia Mfumo wa Sema na Rais, jambo lililoshajihisha wananchi kutumia mfumo huo. <br />
<br />
xiv.Kutoa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa SNR kwa wananchi 2,518 kutoka shehia 44 za Unguja na Pemba. Kiambatanisho nambari 10 kina taarifa zaidi. ii. Programu Kuu ya Kuratibu Ushirikiano wa Kikanda, Kimataifa na Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi. <br />
<br />
31. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 307.02 Milioni sawa na asilimia 47.81 ya makadirio ya TZS. 642.19 Milioni kwa kipindi cha tathmini na asilimia 37.22 ya makadirio ya TZS. 824.88 Milioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo mbili zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kikanda na kimataifa imetumia TZS. 275.52 Milioni sawa na asilimia 53.59 ya makadirio ya kutumia TZS. 514.15 Milioni kwa kipindi cha tathmini; na b) Programu ndogo ya Uratibu Shughuli za Wazanzibari wanaoishi nje ya nchi imetumia TZS. 31.50 Milioni sawa na 11 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 asilimia 24.60 ya makadirio ya kutumia TZS.128.04 Milioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
32. Mheshimiwa Spika, Kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: <br />
<br />
i. Kuratibu ushiriki wa Zanzibar katika Mikutano ya Jumuiya za Kikanda (EAC, SADC, AfCFTA, IORA) na ushirikiano wa Kimataifa kwa ajili ya utatuzi wa changamoto na upatikanaji wa fursa kwa Zanzibar. <br />
<br />
ii. Afisi imeshiriki Vikao na Mikutano 17 ya Jumuiya za Kikanda za EAC, SADC na AfCFTA ndani na nje ya nchi. Lengo la vikao na mikutano hiyo ni upatikanaji wa fursa na kuwajengea uwezo wadau katika kukuza sekta muhimu za Uchumi ikiwemo Uchumi wa buluu, uwekezaji, Biashara na Ujasiriamali Kiambatanisho nambari 11 kina taarifa zaidi. <br />
<br />
iii. Afisi imetoa mafunzo ya Vikwazo Visivyo vya Kodi (NTBs) kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa wataalamu 32 kutoka Kamati ya NTBs ya Zanzibar, Wafanya Biashara na watendaji kutoka Jumuiya ya Wafanya Biashara Zanzibar. Mafunzo hayo yalilenga kuimarisha uelewa kuhusu dhana na athari za Vikwazo Visivyo vya Kodi katika biashara na kujenga uwezo wa washiriki katika kutambua na kushughulikia vikwazo hivyo kwa ufanisi. iv. Kuratibu shughuli 128 za Itifaki ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na kuratibu safari saba za Viongozi Wakuu wastaafu nje ya nchi. <br />
<br />
v. Kushiriki mikutano mitano (5) inayohusiana na masuala ya Diaspora ikiwemo mikutano ya taarifa za wahamaji (Data Migration), ubidhaishwaji wa lugha ya Kiswahili pamoja na vikao vya mashirikiano baina ya Afisi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kiambatanisho nambari 12 kinataarifa zaidi. 12 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 vi. Uzinduzi wa Mfumo rasmi wa Usajili wa Diaspora wa Zanzibar (mwezi Januari 2026), unaoiwezesha Serikali kupata takwimu halisi za Diaspora wa Zanzibar ikiwemo nchi wanazoishi, taaluma na ujuzi, biashara na uwekezaji kwa lengo la kushirikiana katika maswala ya Uchumi, fursa na maendeleo. Hadi kufikia mwezi Machi, 2026, Afisi imesajili Diaspora 1,360 kutoka mataifa mbali mbali duniani. Aidha, kwa kipindi hicho Disapora 423 Wameshapatiwa vitambulisho vyao (Wanaume 257 na Wanawake 166). <br />
<br />
vii. Afisi imeratibu maombi 17 ya vibali vya kazi na maombi 22 ya vibali vya ukaazi kwa Diaspora ambao wanahitaji kukaa nchini na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi. <br />
<br />
viii. Afisi kwa kushirikiana na Jumuiya ya Diaspora Al Amana Foundation kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), imeratibu utoaji wa sadaka ya futari kwa familia zaidi ya 1200 yenye thamani TZS.100.00 Milioni na kuwalipia faini na fidia yenye thamani ya TZS. 18.4 Milioni kwa Wanafunzi 18 walioachiwa huru na kutoa msaada wa magodoro 170 kwa ajili ya Chuo cha Mafunzo. <br />
<br />
ix. Afisi kwa kushirikiana na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Zanzibar na Chuo cha Mafunzo imeratibu mafunzo ya imani kwa Wanafunzi 18 wa Chuo cha Mafunzo walioachiwa huru. <br />
<br />
x. Afisi iliratibu na kushiriki katika zoezi la utoaji wa misaada ya kijamii kwa familia 600 yenye thamani ya zaidi ya TZS. 43.75 Milioni kisiwani Pemba. Misaada hiyo ilitolewa na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Oman (TADIO), Al Wadood Charitable Group na Taasisi ya Diaspora Charity Organization za nchini Oman. <br />
<br />
xi. Afisi kwa kushirikiana na Afisi ya Mufti wa Zanzibar imeratibu uingizwaji wa kontena la sadaka liloletwa na Jumuiya ya Diaspora Ifraj Zanzibar Foundation iliyopo Umoja wa 13 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 Falme za Kiarabu (UAE). Sadaka hio iliwanufaisha familia (668 - Unguja na 5,350 – Pemba) na yenye thamani ya TZS. 377.16 Milioni. <br />
<br />
xii. Afisi ilifanikiwa kukusanya TZS. 13.15 Milioni kutoka Diaspora wa Zanzibar Duniani kwa ajili ya utoaji wa Sadaka katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Sadaka hio walipatiwa watoto 382 ikiwemo mayatima na wenye mahitaji maalum kwa Unguja na Pemba. xiii. Afisi imeratibu programu ya TOKTEN (Tranfer of Knowlegde Through Expatriate Nationals) kwa Wizara na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Wataalam wawili (02) kutoka jamii ya Diaspora (Uingereza na Afrika Kusini) walibadilishana ujuzi na uzoefu kwa Wizara na Taasisi za Serikali katika masuala ya ubunifu, Akili Mnemba pamoja na usimamizi wa huduma za maji safi na salama kwa jamii. <br />
<br />
xiv. Afisi imefanya vikao viwili (02) vya majadiliano na Diaspora, vikao hivyo vilikutanisha wanadiaspora na taasisi husika zinazotoa huduma kwa Diaspora ambapo wanadiaspora walipata fursa ya kueleza changamoto zao na kutatuliwa. Lengo la vikao hivyo ni kuweka mfumo endelevu wa mawasiliano na kuimarisha uhusiano wa Diaspora na nchi yao ya asili. <br />
<br />
iii. Programu Kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Afisi ya Rais – Ikulu. 33. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia Machi 2026, programu hii imetumia TZS. 3.75 Bilioni sawa na asilimia 37.00 ya makadirio ya TZS. 10.13 Bilioni Kwa kipindi cha tathmini na asilimia 28.24 ya makadirio ya TZS. 13.27 Bilioni kwa mwaka. Programu kuu hii imejumuisha programu ndogo nne zifuatazo: <br />
<br />
a) Programu ndogo ya Uratibu na Usimamizi wa Afisi ya Rais Ikulu imetumia TZS.1.31 Bilioni sawa na asilimia 76.92 ya makadirio ya kutumia TZS. 1.697 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. 14 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 <br />
<br />
b) Programu ndogo ya Uratibu wa shughuli za Mipango, Sera na Utafiti imetumia TZS.1.59 Bilioni sawa na asilimia 22.80 ya makadirio ya kutumia TZS. 6.98 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
c) Programu ndogo ya Uratibu na Usimamizi wa Afisi ya Rais Ikulu Pemba imetumia TZS. 733.81 Milioni sawa na asilimia 64.68 ya makadirio ya kutumia TZS. 1.13 Bilioni kwa kipindi cha tathmini. <br />
<br />
d) Programu ndogo ya Usimamizi wa Usalama wa Serikali imetumia TZS. 117.00 Milioni sawa na asilimia 36.84 ya makadirio ya kutumia TZS. 317.61 Milioni kwa kipindi cha tathmini. 34. Mheshimiwa Spika, kupitia Programu hii, Afisi imetekeleza yafuatayo: <br />
<br />
i. Kuandaa Kanuni za Utoaji wa Tunzo (Nishani) 2025 chini ya Sheria ya mambo ya Rais. Nam. 3 ya mwaka 2020. <br />
<br />
ii. Kuratibu na kusimamia utoaji wa stahiki kwa watumishi kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma kwa lengo la kuongeza hamasa katika utekelezaji wa majukumu ya kazi. <br />
<br />
iii. Kufanya ukaguzi wa kipindi cha robo ya nne ya Mwaka wa Fedha 2024/2025, sambamba na ukaguzi wa robo ya kwanza, ya pili na ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, kwa lengo la kutathmini utekelezaji wa shughuli, ufanisi wa matumizi ya rasilimali, pamoja na kuainisha na kushauri maeneo yanayohitaji kuimarishwa kwa kuzingatia viwango na miongozo ya ukaguzi wa ndani. <br />
<br />
iv. Kuwajengea uwezo watumishi 42 kwa kuwapatia mafunzo ya muda mrefu katika ngazi na fani zinazohitajika za elimu, pamoja na mafunzo ya muda mfupi ikiwemo Programu za kuwajengea ujuzi kazini na maandalizi ya kustaafu utumishi wa umma kwa lengo la kuimarisha 15 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 utendaji kazi. Kiambatanisho nambari 13 kinataarifa zaidi. v. Kuhakiki mali za Afisi ya Rais - Ikulu kwa kuzitambua, kuziweka thamani stahiki na kuzisajili katika Mfumo wa Usimamizi wa Mali wa Serikali. <br />
<br />
vi. Kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Afisi kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 hadi 2025/2026, kwa lengo la kupima kiwango cha utekelezaji wa malengo yaliyowekwa, kubaini mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza, na kuainisha hatua stahiki za kuimarisha utendaji. <br />
<br />
vii. Kufanya tathmini ya utendaji wa Afisi ya Usalama wa Serikali pamoja na hali halisi ya usalama katika Ofisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. viii. Kufanya upekuzi wa kiusalama wa awali na endelevu kwa watumishi 1,739. Hatua hii imeimarisha uadilifu na uaminifu miongoni mwa watumishi wa umma, hususan katika nafasi nyeti, na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa vihatarishi vya kiusalama vinavyoweza kujitokeza. <br />
<br />
ix. Kufanya ukaguzi wa miundombinu na majengo ya Serikali kumi na moja (11), pamoja na mifumo ya TEHAMA katika taasisi tatu (3) za Serikali. Ukaguzi huu umewezesha kutathmini hali ya usalama wa nyaraka, taarifa, maeneo ya kazi na ufanisi wa mifumo ya utoaji huduma. <br />
<br />
x. Kutoa mafunzo maalum ya kiusalama kwa wateule 78. Mafunzo yalilenga kuongeza uelewa wao wa kiusalama, kuimarisha utendaji katika majukumu yao na kudumisha nidhamu. <br />
<br />
xi. Kutoa mafunzo maalumu ya kiusalama katika mifumo ya TEHAMA na vifaa vya kielektroniki kwa taasisi tatu (03) za Serikali, mafunzo yalilenga kuimarisha uelewa 16 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 wa watumishi, utendaji wao na kuhakikisha usalama wa matumizi ya mifumo muhimu ya kiserikali. <br />
<br />
xii. Kutoa mafunzo kwa watumishi wa umma kwa taasisi 32. Mafunzo haya yalilenga kuimarisha uelewa wa watumishi juu dhana ya usalama serikalini. xiii. Kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na uratibu kwa waajiriwa wapya na wateule wa Rais. Shughuli hizi zinaweka msingi mzuri wa kudhibiti rasilimali watu na kuimarisha usalama, huku zikiwa na lengo la kuongeza ufanisi wa GSO katika kipindi kijacho. <br />
<br />
xiv. Kufuatilia ahadi za Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika miradi ya maendeleo kwa upande wa Pemba. Ahadi hizo zimejumuisha Miradi ya Maendeleo ya Ujenzi wa Barabara ya Ukutini – Mtangani, Finya – Kicha, Chuo cha Mwalimu Nyerere Tawi la Pemba, Dahalia ya Skuli ya Sekondari ya Kiwani na Fidel Castro. <br />
<br />
xv. Kutoa mafunzo ya Sera na Sheria ya Diaspora kwa masheha 32 wa Wilaya ya Chake Chake Pemba. Lengo la mafunzo hayo ni kujenga uelewa kwa masheha juu ya namna kufahamu fursa na huduma wanazopewa Diaspora na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. <br />
<br />
xvi. Kuandaa na kurusha vipindi vinne (4) vinavyoonesha uwajibikaji wa Serikali ya awamu ya nane kwa jamii kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii Pemba. UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MIRADI YA MAENDELEO <br />
<br />
35. Mheshimiwa Spika, Kwa kipindi cha miezi tisa, Afisi ya Rais - Ikulu ilipangiwa TZS. 6.70 Bilioni kwa utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Miradi hiyo ni Mradi wa Uimarishaji wa majengo ya Ikulu, Mradi wa Uimarishaji Mawasiliano ya Mfumo wa Sema na Rais na Mradi wa Uimarishaji wa 17 HOTUBA YA BAJETI WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU 2026/2027 Mfumo wa Ulinzi na Usalama katika Majengo ya Ikulu na Makaazi ya Mheshimiwa Rais. Hadi kufikia Machi 2026, Afisi imeingiziwa TZS. 1.37 Bilioni sawa na asilimia 20.46. 36. <br />
<br />
Mheshimiwa Spika, Kupitia shughuli za miradi ya maendeleo, Afisi imetekeleza yafuatayo: i. Kufanya ukarabati wa majengo ya Ikulu Ndogo ya Dodoma na Ikulu Ndogo ya Laibon Dar es salaam ikiwemo uwekaji wa paving stone na curb stone mpya katika maeneo ya ndani ya Ikulu. <br />
<br />
ii. Kuimarisha mifumo ya ulinzi katika Ikulu Ndogo ya Pagali kwa kuweka kamera za uangalizi (CCTV), pamoja na uzio wa umeme, kwa lengo la kuongeza kiwango cha usalama na ulinzi wa eneo hilo. <br />
kuu wa Serikali, kwa lengo la kuimarisha ufanisi, hadhi na weledi katika utekelezaji wa majukumu ya kiutawala<br />
iii. Kuweka lifti katika Ikulu ya Mnazi Mmoja ili kuimarisha upatikanaji wa huduma na kurahisisha ufikiaji wa maeneo ya ofisi, hususan kwa wageni wanaofika kushiriki vikao na mikutano na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hatua inayochangia kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutawala na hadhi ya mazingira ya kikazi. <br />
<br />
iv. Kununua vitendea kazi vinavyohitajika katika kutoa huduma kwa Uongozi, ikiwemo vifaa vya kisasa vya uendeshaji wa mikutano, mifumo ya sauti (PA system), vifaa vya TEHAMA, mifumo ya mawasiliano ya ndani, pamoja na vifaa maalum vya mapokezi na mikutano ya viongozi wa]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-08T15:55:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hotuba ya Waziri wa Nchi Afisi ya Rais &#45; Ikulu &amp;nbsp; Mheshimiwa Dkt. Saada Mkuya Salum (MBM) makadirio ya mapato na matumizi  mwaka wa Fedha 2026/2027.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-mwaka-wa-fedha-2026-2027</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-dkt-saada-mkuya-salum-mbm-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-mwaka-wa-fedha-2026-2027#When:15:15:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-05-08T15:15:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Risala ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Al Haj Dk. Hussein Ali Mwinyi ya Kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa Mwaka 2026 Miladia, sawa na Mwaka 1447 Hijria.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/risala-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-al-haj-dk-hussein-ali-mwinyi-ya-kuukaribisha-mwezi-mtukufu-wa-ramadhani-kwa-mwaka-2026-miladia-sawa-na-mwaka-1447-hijria</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/risala-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-al-haj-dk-hussein-ali-mwinyi-ya-kuukaribisha-mwezi-mtukufu-wa-ramadhani-kwa-mwaka-2026-miladia-sawa-na-mwaka-1447-hijria#When:16:30:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[RISALA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA AL HAJ DK. HUSSEIN ALI MWINYI YA KUUKARIBISHA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI KWA MWAKA 2026 MILADIA, SAWA NA MWAKA 1447 HIJRIA.<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Assalamu Aleikum Warahmatullahi Wabarakatuh<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Subhanahu Wataala kwa kutujaalia neema ya uhai na kwa kutuwezesha kuifikia siku hii tunapoukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa mwaka huu wa 1447 Hijria, sawa na mwaka 2026 Miladia.<br />
<br />
Mwezi wa Ramadhani umetukuzwa na Mwenyezi Mungu kuwa ni mwezi mtukufu kwani amali za waja katika mwezi huu, huwa na fadhila na daraja kubwa. Kwa mnasaba huo,imefaradhishwa kufunga pamoja na kuongeza juhudi katika kutekeleza ibada nyingine za faradhi na sunna kwa wingi ili tunufaike na utukufu wa Mwezi wa Ramadhani. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Ramadhani ni mwezi ulioteremshwa kitabu kitukufu cha Qurani katika usiku ulio bora zaidi wa Lailatul Qadir, kitabu ambacho ndio muongozo wa dini yetu. Tunafundishwa na kuhimizwa kuwa miongoni mwa ibada bora na muhimu katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani tunaoukaribisha ni kukithirisha kusoma Qurani na kuzingatia mafundisho yake ili tuweze kupata mafanikio hapa duniani na kesho mbele ya haki.<br />
<br />
Natumia fursa hii kuwahimiza waislamu kuendeleza utaratibu wa kuwa na darsa mbalimbali za Qurani na mafunzo mengine katika mwezi wa Ramadhani ili kujiongezea maarifa na kukuza imani zetu pamoja na kutuwezesha kutekeleza ibada kwa usahihi zaidi. Aidha, tuendeleze utamaduni wa kuandaa mashindano ya kuhifadhi Qurani ambayo huchangia kuwawezesha watoto na vijana wetu kufuata mwenendo mwema wa kupenda kusoma na kuhifadhi Qurani na huongeza hamasa ya usomaji wa Qurani ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Nitoe wito kwetu sote tujitahidi kuhudhuria na kushiriki katika mashindano hayo.<br />
<br />
Ndugu wananchi,<br />
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa kuchuma fadhila ambazo Mwenyezi Mungu amewaahidi waja wake watakaofanya mema na kujiepusha na makatazo yake. Miongoni mwa mambo mema yanayohimizwa ni kutoa sadaka kwa ndugu zetu wenye uwezo mdogo ili nao waweze kupata mahitaji yao muhimu yakiwemo ya chakula.<br />
<br />
Napenda kutumia fursa hii kuwaomba wafanyabishara kutopandisha bei za bidhaa muhimu hasa zile zinazotumika zaidi katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Mwezi wa Ramadhani ni kipindi cha kuchuma mema kwa kusaidiana na kuhurumiana mambo ambayo huzidisha mapenzi na kuongeza baraka katika jamii. Ni wajibu wetu kuwafikiria na kuwasaidia wenzetu wasio na uwezo wakiwemo wajane na mayatima ili nao waweze kuupokea vema Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.<br />
<br />
Ndugu wananchi,<br />
Serikali kupitia Tume ya Ushindani Halali wa Biashara imefanya ukaguzi kwenye maghala ya kuhifadhia bidhaa muhimu za chakula zikiwemo mchele, unga wa ngano, sukari na mafuta ya kupikia pamoja na kukagua madukani. Tumejiridhisha kuwa kuna chakula cha kutosha kwa mwezi wa Ramadhani na hata baada ya hapo. Hivyo, nazitaka mamlaka husika kusimamia mwenendo wa bei za bidhaa za chakula na kuhakikisha hazipandishwi ovyo ili kufikia malengo ya dhamira njema ya Serikali ya kuondoa ushuru wa bidhaa hizo ili wananchi hasa wa kipato cha chini waweze kumudu kuzinunua.<br />
<br />
Ndugu wananchi,<br />
Suala la kutunza usafi ni moja ya majukumu muhimu katika kujiepusha na maradhi mbalimbali hasa ya kuambukiza na pia kuimarisha haiba na taswira ya miji yetu. Sote ni mashahidi kuwa uzalishaji wa taka huongezeka sana katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kutokana na shughuli mbali mbali katika Manispaa, Miji na Halmashauri zetu.<br />
<br />
Napenda kutumia fursa hii kuzitaka Mamlaka zote zinazosimamia usafi wa mazingira katika Manispaa, Miji na Halmashauri zote Unguja na Pemba kuwa na mipango na mikakati maalum ya kushughulikia usafi katika maeneo yao.<br />
<br />
Aidha, niwaombe wananchi kushirikiana na mamlaka husika kutunza usafi wa mazingira  katika maeneo yote hasa kwenye masoko, maeneo ya huduma za chakula na maeneo ya makaazi.<br />
Ndugu wananchi,<br />
Nahitimisha risala yangu kwa kuhimiza umuhimu wa kuendelea kuishi kwa amani, kuheshimiana na kujiepusha na mambo yote ambayo yanakwenda kinyume na mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kutii sheria, kuepuka mambo yote yanayoweza kusababisha maudhi au karaha kwa  waliofunga. Tuna wajibu wa kuendelea kuishi kwa kuvumiliana ili kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini.<br />
<br />
Tumuombe Mwenyezi Mungu atujaalie kuitekeleza ibada ya saumu na ibada nyengine kwa Ikhlasi ili tuweze kunufaika na fadhila za utukufu wa mwezi huu. Mwenyezi Mungu aizidishie nchi yetu amani, umoja na mshikamano. Atuzidishie Imani, uchamungu na atuwezeshe kupata riziki za halali kwa baraka na utukufu wa mwezi wa Ramadhani ili tuweze kupata mafanikio  hapa Duniani na kesho mbele ya haki. Amina! <br />
<br />
Ramadhan Mubarak.<br />
Wassalamu Aleikum Warahmatullahi Wabarakatu<br />
Ahsanteni kwa kunisikiliza<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-02-18T16:30:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI  KATIKA UFUNGUZI WA JENGO LA HUDUMA ZA MATIBABU YA DHARURA NA MAABARA KWENYE KITUO CHA AFYA MAKUNDUCHI</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-ufunguzi-wa-jengo-la-huduma-za-matibabu-ya-dharura-na-maabara-kwenye-kituo-cha-afya-makunduchi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-ufunguzi-wa-jengo-la-huduma-za-matibabu-ya-dharura-na-maabara-kwenye-kituo-cha-afya-makunduchi#When:13:37:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI<br />
KATIKA UFUNGUZI WA JENGO LA HUDUMA ZA MATIBABU YA DHARURA NA MAABARA KWENYE KITUO CHA AFYA MAKUNDUCHI WILAYA YA KUSINI MKOA WA KUSINI - UNGUJA<br />
17 JANUARI 2024<br />
<br />
Waheshimiwa mawaziri Mliopo<br />
Mheshimiwa Hassan Khamis Hafidh, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar,<br />
Mheshimiwa Ayoub, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,<br />
Mhandisi Zena Ahmed Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, <br />
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja,<br />
Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja,<br />
Dkt Amour Suleiman Mohamed, Kaimu Katibu Mkuu na Mkurugenzi Mkuu Wizara ya Afya<br />
Viongozi wa vikosi vya ulinzi na Usalama mliopo,<br />
Waheshimiwa Wabunge na Wawakilishi mliopo<br />
Wakurugenzi wa Wizara ya Afya na Wizara nyengine mliopo,<br />
Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kusini,<br />
Viongozi wa Vyama na Serikali mliopo,<br />
Ndugu wafanyakazi na waandishi wa habari<br />
Wageni waalikwa, <br />
Ndugu Wananchi,<br />
Mabibi na Mabwana,<br />
<br />
ASSALAM ALAYKUM<br />
<br />
<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai  na afya njema na kutuwezesha kukutana kwa madhumuni ya kulifungua rasmi jengo jipya la Huduma za matibabu ya dharura na Maabara ya kisasa katika kituo chetu cha Afya hapa Makunduchi. Napata faraja kuhudhuria tukio hili kwani wiki chache zilizopita, nilipokuja Makunduchi kwa ajili ya kisomo cha Duwa, niliwaahidi viongozi wakiwemo masheha kuwa penye majaaliwa, nitakuja mwenyewe katika sherehe za ufunguzi wa jengo hili. Namshukuru Mwenyezi Mungu kuniwezesha kufikia dhamira yangu hiyo. Aidha, naishukuru Wizara ya Afya na wafadhili waliondaa shughuli hii ya leo na kwa heshima waliyonipa ya kuwa Mgeni Rasmi. Pia, natoa shukrani zangu za dhati kwenu ndugu wananchi, viongozi na waalikwa wote kwa kuamua kuja kuungana nasi katika tukio hili muhimu la maendeleo ya sekta ya afya. <br />
<br />
Ndugu Wananchi, <br />
Ujenzi wa jengo jipya la huduma za matibabu ya dharura  na maabara ya kisasa hapa Makunduchi ni miongoni mwa  juhudi zinazochukuliwa na  Serikali katika kuimarisha miundombinu ya huduma za Afya ili ziweze kwenda sambamba na mabadiliko ya maendeleo ya huduma za afya duniani. Hatua hii vile vile ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020- 2025 pamoja na ahadi tulizozitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2020. Nyote ni mashahidi wa mafanikio ambayo tumeyapata katika kipindi cha miaka mitatu tu ya uongozi wa Awamu ya Nane katika kuimarisha sekta ya afya kama ilivyo katika sekta nyengine zikiwemo elimu, maji safi na salama, umeme, ujenzi wa barabara na nyenginezo.<br />
<br />
Katika sekta hii ya afya, tunathibitisha utekelezaji  wa ahadi  zetu kwa kumaliza kujenga na kufungua hospitali 10 za wilaya na moja ya mkoa ya Lumumba ambazo zote tumeziwekea vifaa vya kisasa na wataalamu kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi kwa mujibu wa ngazi ya hospitali husika. Leo hii tupo hapa Makunduchi katika tukio jengine la ufunguzi rasmi wa jengo jipya la  huduma za tiba za dharura pamoja  na maabara ya kisasa. Huu ni mwendelezo wa mageuzi makubwa ya maendeleo ya sekta ya afya hapa nchini.<br />
<br />
Ndugu wananchi,<br />
Serikali ya  Awamu ya Nane inaendelea kuchukua hatua mbali mbali za kuimarisha huduma za afya katika ngazi zote. Tumekamilisha ujenzi wa Hospitali katika ngazi ya wilaya na kuanza ngazi ya mkoa. Tutaendelea kujenga hospitali za mikoa katika mikoa iliyobaki ikiwemo Mkoa huu wa Kusini Unguja ambapo taarifa njema ni kuwa mfadhili ameshapatikana. Eneo lipo tayari na mfadhili ameshawasilisha michoro ya awali ya hospitali hiyo itakavyokuwa. Kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali pia inaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za Afya kwa ngazi ya msingi. Hatua hiyo ni utekelezaji wa mpango mpya wa serikali katika utoaji wa huduma za Afya ngazi ya msingi ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu kwa kujenga majengo mapya na kutanua  baadhi ya vituo vya afya nchi nzima, kuweka vifaa vya kisasa kwa lengo la kutoa huduma bora za afya ikiwemo za dharura na uchunguzi wa awali katika ngazi ya msingi ili kupunguza vifo visivyotarajiwa. <br />
<br />
Ndugu wananchi, <br />
Serikali imepata mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mipango na mikakati ya kuendeleza sekta ya afya nchini kupitia programu mbali mbali zinazoendeshwa kwa ushirikiano na Washirika wa Maendeleo. Jambo hilo limesaidia kuimarisha huduma za afya katika ngazi ya msingi. Vile vile ujenzi wa miundombinu kama hii na utoaji wa elimu ya afya na uibuaji wa wananchi wenye matatizo mbali mbali ya kiafya mapema kupitia programu hizi ikiwemo ya wafanyakazi wetu katika ngazi ya jamii (CHW) tuliyoizindua rasmi tarehe 16 Disemba 2023 pale Maisara mjini Zanzibar na Afya Call Center. Huduma ambayo mwananchi sasa anaweza kupiga simu kupitia namba 190 bure na kupata ushauri wa kiafya. Serikali ina lengo la kuunganisha kituo hiki muhimu na huduma za dharura nchi nzima. Jambo hili linaisaidia serikali kuimarisha afya ya jamii, mfumo wa rufaa, kupunguza vifo pamoja na kupunguza gharama za matibabu kwani wagonjwa hupatiwa matibabu mapema na kupewa ushauri unaofaa ili kupambana na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari, presha na saratani.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-17T13:37:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI, KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 60 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-kuadhimisha-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-kuadhimisha-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar#When:18:09:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI, KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 60 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR<br />
TAREHE: 11 JANUARI, 2024<br />
Assalamu Aleikum<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kutupa uhai na afya njema na kutuwezesha kufikia siku ya leo, tukiwa katika mkesha wa Maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. <br />
<br />
Tunapoadhimisha sherehe za Mapinduzi, tuna wajibu pia wa kuwakumbuka Waasisi wetu chini ya Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, viongozi na wananchi wenzetu waliotangulia mbele ya haki, ambao waliitumikia nchi yetu kwa moyo, ujasiri na uzalendo. Tunamuomba Mwenyezi Mungu awalaze pema peponi. Na wale walio hai, Mola awape afya njema na umri mrefu tuendelee kushirikiana nao katika kujiletea maendeleo. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Nachukua fursa hii kuwashukuru wananchi wote kwa kujitokeza kwa wingi katika matukio mbali mbali yaliyoandaliwa katika Maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi. Ni matarajio yangu kuwa na kesho siku ya kilele, mtajitokeza tena kwa wingi katika uwanja wa Amani ili kufanikisha sherehe zetu. <br />
Tofauti na mara nyengine zote safari hii sherehe yetu itafanyika mchana ili kutoa fursa kwa waumini wa Dini ya Kiislamu kupata nafasi ya kutekeleza ibada ya sala ya Ijumaa.<br />
<br />
Mara hii tulikuwa na miradi iliyozinduliwa 65 na miradi 45 imeekewa mawe ya msingi. Hii ni idadi kubwa sana ya miradi ambayo hatujawahi kuifikia katika kipindi cha sherehe kama hizi. Vile vile, tumeandaa matukio makuu maalum na sherehe za aina yake ambazo kilele chake kitafanyika katika uwanja wa Amani. Kadhalika, tuna ujio wa baadhi ya wageni mashuhuri tutakao kuwa nao katika maadhimisho yetu haya. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Mafanikio tuliyoyapata miaka 60 tokea Mapinduzi ya mwaka 1964, yametokana na uongozi thabiti wa Waasisi wa Taifa letu na viongozi wote wa awamu zilizotangulia kwa ushirikiano na uzalendo kati yao na nyinyi wananchi. Serikali ya Awamu ya Nane tokea ilipoingia madarakani miaka mitatu iliopita, inayaendeleza mafanikio hayo na kufanya juhudi za kuhakikisha Zanzibar inazidi kupiga hatua za maendeleo katika sekta zote na kudumisha amani na umoja wa kitaifa.<br />
<br />
Nilipoingia madarakani mwaka 2020, nilieleza dhamira yangu ya kuunganisha Malengo ya Mapinduzi na uchumi, nikilenga kuimarisha jitihada za kukuza uchumi ili kustawisha maisha ya wananchi wa Zanzibar. Lengo la Serikali ninayoiongoza ni kuendeleza umoja, mshikamano na maridhiano ili kila Mzanzibari apate fursa ya kuchangia maendeleo na kunufaika na matunda ya Mapinduzi kwa misingi ya usawa. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa mafanikio tunayoendelea kuyapata katika kuifikia dhamira hiyo katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Nane.<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Katika kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi na miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Nane, tunafurahia mafanikio tuliyo nayo katika kudumisha na kuendeleza Amani, Umoja na Mshikamano. Misingi hii muhimu imetuwezesha kupiga hatua katika maendeleo ya uchumi, ujenzi wa miundombinu, kuimarisha huduma za jamii, biashara na kuendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.<br />
<br />
Natoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan; Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM kwa ushirikiano mkubwa anaonipa. Vile vile, nawashukuru viongozi wa kisiasa, viongozi wa dini na asasi za kijamii, viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama vya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wote kwa kunipa ushirikiano na kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini kwa faida ya kizazi cha sasa cha baadae.<br />
 Nawahakikishia wananchi na wageni wote wanaotutembelea kwamba nchi yetu ipo salama na kwamba Serikali zetu zote mbili zitaendelea kutekeleza wajibu wake wa kikatiba na kisheria katika kulinda amani, utulivu na usalama wa mali zao.<br />
<br />
Ndugu Wananchi. <br />
Katika hotuba yangu hii ya kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na miaka mitatu Serikali ya Awamu ya Nane, nitaelezea kwa muhtasari mafanikio, changamoto na mipango yetu ya utekelezaji wa majukumu ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar. Serikali iliwapa jukumu mawaziri wote kuelezea kwa kina kupitia vyombo vya habari, mafanikio, changamoto na mipango ya kila wizara ili wananchi wafahamu utendaji wa Serikali yao. Nawashukuru Waheshimiwa Mawaziri kwa kutekeleza kwa mafanikio agizo hilo.<br />
<br />
Ndugu Wananchi<br />
Juhudi zinazochukuliwa na Serikali zimewezesha uchumi wetu kuzidi kuimarika. Thamani ya Pato halisi la Taifa (GDP at constant Price) imeongezeka kutoka TZS. Trilioni 3.116 kwa mwaka 2020 na kufikia thamani ya TZS. Trilioni 3.499 mwaka 2022. Vile vile ukusanyaji wa mapato umeongezeka kufikia TZS. Trilioni 1.4 mwaka 2022/2023 kutoka TZS. Bilioni 790.48 mwaka 2020/2021, sawa na ongezeko la asimilia 56.4. Aidha, kasi ya ukuaji wa uchumi mwaka 2022 imefikia wastani wa asilimi 6.8 ikilinganishwa na asilimia 1.3 ya mwaka 2020. Kiwango cha ukuaji wa uchumi wetu ni kikubwa ikilinganishwa na nchi nyingi zinazoendelea. <br />
<br />
Kukuwa kwa uchumi wetu kumetokana na kuongezeka kwa uwekezaji kwa kutekelezwa miradi ya Maendeleo ya kipaumbele ikiwemo miundombinu ya barabara, bandari, viwanja vya ndege, huduma za maji safi na salama, uimarishaji wa huduma za nishati ya umeme, masoko na kuimarika kwa sekta ya huduma kwa kuongezeka kwa idadi ya watalii. Pato la mtu binafsi nalo limeongezeka kutoka USD 1,099 sawa na TZS. Milioni 2.5 mwaka 2020 na kufikia USD 1,230 sawa na TZS. Milioni 2.8 mwaka 2022. Aidha, jitihada zilizochukuliwa na Serikali zimeweza kudhibiti kasi ya mfumko wa bei na kuendelea kuwa katika tarakimu moja. Kwa mwaka 2023 mfumko wa bei ulikuwa ni wa wastani wa asilimia 6.8 hali inayomuhakikishia mwananchi kupata mahitaji ya lazima.<br />
<br />
Ndugu Wananchi<br />
Serikali za awamu zote zilizopita baada ya Mapinduzi zilichukuwa juhudi za uwekezaji kwa ujenzi wa miundombinu, majengo ya Ofisi, huduma na maakazi, viwanda na kuwakaribisha wawekezaji kuzitumia fursa na rasilimali zilizopo nchini katika kuchangia ukuaji wa uchumi. Tunapoadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi na Miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Nane tumeshuhudia mafanikio makubwa katika jitihada zetu za kuvutia wawekezaji.  Kasi ya uwekezaji nchini imeongezeka ambapo jumla ya miradi 296 yenye thamani ya USD. Bilioni 4.5 imeidhinishwa. Miradi hiyo inakadiriwa kutoa ajira zipatazo 17,479 ikihusisha uwekezaji katika visiwa vidogo 16 wenye thamani ya USD. Milioni 377.5, ujenzi wa hoteli za kitalii 112, viwanda 36, biashara ya majengo 56 na miradi mingine ya kiuchumi. <br />
<br />
Mafanikio haya yametokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa na Serikali ikiwemo uimarishaji wa huduma zinazotolewa na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) ambapo sasa wawekezaji wanaweza kupata huduma zote za uwekezaji katika kituo kimoja (One Stop Center) ndani ya masaa 24. Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuvutia wawekezaji ikiwa ni pamoja na kutangaza fursa zilizopo katika maeneo ya bandari jumuishi ya Mangapwani na ujenzi wa miundombinu ikiwemo barabara, maji na umeme katika maeneo ya uwekezaji.<br />
<br />
Ndugu Wananchi<br />
Kwa kuzingatia umuhimu wa biashara kwa Zanzibar, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua hatua mbali mbali kuimarisha mazingira ya ufanyaji wa biashara. Tunapoadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi na mitatu ya Serikali ya Awamu ya Nane, sekta ya biashara ya usafirishaji na uingizaji bidhaa kwa ujumla inaendelea kuimarika ambapo kwa mwaka 2022 Zanzibar imefanya biashara yenye thamani ya TZS. Trilioni 1.4 ukilinganisha na TZS. Bilioni 913.1 kwa mwaka 2020, sawa na ongezeko la asilimia 57.6.<br />
 <br />
Zanzibar imesafirisha nje bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 180.4 kwa mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 174.7 ikilinganishwa na usafirishaji wa bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 65.7 kwa mwaka 2020. Kwa mwaka 2022, Zanzibar imesafirisha tani 6,452.8 za karafuu yenye thamani ya TZS. Bilioni 118.3 ikilinganishwa na tani 3,506.8 zilizosafirishwa mwaka 2020, zenye thamani ya TZS. Bilioni 38.37 sawa na ongezeka la fedha la asilimia 208.1. Kwa upande wa mwani Zanzibar imesafirisha Tani 13,972.5 zenye thamani ya TZS. Bilioni 16.0 kwa mwaka 2022 ukilinganisha na tani 11,382.6 wenye thamani ya TZS. Bilioni 11.7 kwa mwaka 2020, sawa na ongezeko la asilimia 36.8.  <br />
<br />
 Kuhusu biashara baina ya Zanzibar na Tanzania Bara, mwaka 2022, Zanzibar imesafirisha bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 37.64 ikilinganishwa na bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 15.03 zilizosafirishwa mwaka 2020. Kwa upande wa uagiziaji katika kipindi cha mwaka 2022, Zanzibar imeagizia bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 375.80 kutoka Tanzania Bara ikilinganishwa na uagiziaji wa bidhaa zenye thamani ya TZS. Bilioni 243.81 kwa mwaka 2020.<br />
<br />
Ndugu Wananchi<br />
Kwa madhumuni ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi, Serikali imechukua hatua za kuimarisha uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na kupambana na umaskini. Serikali imepata mafanikio katika uimarishaji wa vikundi vya ushirika ambapo jumla ya vikundi 1,546 vya ushirika vimesajiliwa. Idadi hiyo imewezesha kufikia vikundi 3,662 vya ushirika vilivyosajiliwa nchini. Kupitia fedha za Ahuweni ya UVIKO - 19, Serikali imetoa jumla ya TZS Bilioni 60. Fedha hizi zinajumuisha TZS. Bilioni 29 zilizotolewa kwa ajili ya sekta za Uchumi wa Buluu, TZS Bilioni 16 kwa ajili ya ujenzi wa Masoko na TZS. Bilioni 15 kwa ajili ya Programu ya Inuka yenye lengo la kutoa mikopo kwa wajasiriamali na wafanyabiashara.<br />
<br />
Programu ya Inuka ilianza na mtaji wa TZS. Bilioni 15.0. Hadi sasa mikopo yenye thamani ya TZS. Bilioni 22.4 imeshatolewa kupitia programu hii. Ongezeko la thamani la mikopo hiyo limetokana na fedha za marejesho ambazo zinaendelea kutolewa mikopo mipya (Revolving Fund). Mikopo hiyo imewezesha kuzalisha ajira za moja kwa moja (direct employment) kwa Wananchi 43,360. Aidha, programu ya Khalifa Fund imetoa mikopo yenye thamani ya TZS. Bilioni 2.10 kwa miradi 18 ya wananchi. Kadhalika, kupitia Mfuko wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi jumla ya TZS Milioni 852.17 zimetolewa kwa wananchi.<br />
<br />
Kupitia Programu ya Mikopo kwa Makundi Maalum, hadi sasa Serikali imefanikiwa kukusanya jumla ya TZS. Bilioni 1.9 kutoka Halmashauri za Wilaya. Fedha hizi zimelengwa kutumika kwa ajili ya kutoa mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. <br />
<br />
Ndugu Wananchi<br />
Katika kuhakikisha suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi linapata mafanikio, Ujenzi wa miundombinu umezingatiwa ambapo vituo viwili vya kusarifu asali vinavyogharimu TZS. Milioni 529.29 vimejengwa Unguja na Pemba.  Aidha, ujenzi wa kituo cha mafunzo ya usarifu mazao utakaogharimu USD. Milioni 1.29 umeanza kwa matayarisho ya awali.<br />
Kadhalika, wajasiriamali wamepatiwa vifaa vya uzalishaji wa asali ikiwemo Mizinga yenye thamani ya TZS. Milioni 459.98, vifaa vya nyuki vyenye thamani ya TZS Milioni 194.34, Vifaa vya maabara vyenye thamani ya TZS Milioni 34.40 na Pikipiki 9 zenye thamani ya TZS Milioni 35.91.<br />
<br />
Serikali pia, imeanzisha Wakala ili kuimarisha usimamizi wa utoaji wa Mikopo kwa kushirikiana na Benki ya CRDB. Vile vile, mafunzo yanaendelea kutolewa kwa wajasiriamali ili kuwajengea uwezo zaidi ambapo wajasiriamali 2,225 wameshapatiwa mafunzo hayo kwa kipindi hiki.Jitihada hizi za Serikali ya Awamu ya Nane katika kipindi cha miaka mitatu, zimewezesha kupatikana kwa jumla ya ajira 187,651. Idadi hiyo imevuka malengo ya ajira 180,000 kwa miaka mitatu, sawa na ongezeko la asilimia 104.3<br />
<br />
 Ndugu Wananchi,<br />
Serikali imezingatia haja ya kuwapatia wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo mazingira bora ya kufanyia kazi zao. Ujenzi wa vituo 14 vya wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo vilivyogharimu TZS Bilioni 16.03 vimejengwa Unguja na Pemba ambapo baadhi yake vimeanza kutumika. Vile vile, jumla ya masoko 10 yamejengwa kwenye Wilaya 6 yenye thamani ya TZS. Bilioni 4.93. Aidha, ujenzi wa masoko makubwa ya kisasa unaogharimu TZS. Bilioni 102.41 unaendelea katika maeneo ya Mwanakwerekwe, Jumbi na Chuini. Ni matumaini yetu kuwa masoko haya yatakamilika mwaka huu 2024 na kuanza kutumika. <br />
<br />
Hadi kufikia tarehe 20 Disemba, 2023 jumla ya wajasiriamali 7,227 wamesajiliwa na kupatiwa vitambulisho katika Serikali za Mitaa Unguja na Pemba. Vile vile, mafanikio yamepatikana katika ukusanyaji wa mapato kwa Serikali za Mitaa, ambapo ukusanyaji wa mapato umeongezeka kwa asilimia 26 kutoka TZS Bilioni 15.24 zilizokusanywa mwaka 2020 hadi kufikia TZS Bilioni 20.71 mwaka 2023.  ]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-11T18:09:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>RISALA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK HUSSEIN ALI MWINYI YA KUUAGA MWAKA 2023 NA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA WA 2024</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/risala-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-ya-kuuaga-mwaka-2023-na-kuukaribisha-mwaka-mpya-wa-2024</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/risala-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-ya-kuuaga-mwaka-2023-na-kuukaribisha-mwaka-mpya-wa-2024#When:18:08:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[RISALA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK HUSSEIN ALI MWINYI YA KUUAGA MWAKA 2023 NA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA WA 2024<br />
<br />
Ndugu Wananchi;<br />
Assalamu Aleikum Warahamatullah Wabarakatuh,<br />
<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na afya njema na kutuwezesha kuifikia siku ya leo ya kuuaga mwaka 2023 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2024.<br />
<br />
Ndugu Wananchi;<br />
Ni utaratibu tuliojiwekea katika nchi yetu inapofika siku kama hii kutoa risala ya kuuaga mwaka unaomalizika na kuukaribisha mwaka mpya kwa kueleza muhtasari na tathmini ya utendaji wetu, sambamba na mwelekeo wa nchi yetu kwa mwaka ujao. Kwa hakika, tuna wajibu wa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuukamilisha mwaka wa 2023 kwa amani na mafanikio. Katika mwaka tunaoumaliza, tumefanikiwa katika kudumisha amani,umoja na mshikamano wa kitaifa hapa nchini.<br />
<br />
Viongozi wa Serikali, viongozi wa kisiasa, asasi za kiraia tumeweza kushirikiana na wananchi  katika masuala mbali mbali ya maendeleo, hatua ambayo imetuwezesha kutekeleza kwa mafanikio mipango yetu ya kukuza uchumi na kuimairisha huduma za jamii. Aidha, hali hiyo imewavutia na kupelekea kuungwa mkono na washirika wetu wa maendeleo yakiwemo mashirika ya Kimataifa, Taasisi, mbali mbali, Balozi za nje na nchi marafiki.<br />
<br />
Ndugu Wananchi;<br />
Katika mwaka tunaoukamilisha tumepata mafanikio katika kuimarisha ukuaji wa uchumi, uimarishaji wa miundombinu, biashara na uwekezaji, huduma za jamii zikiwemo elimu, afya, maji safi na salama, umeme na uimarishaji wa demokrasia na utawala bora. Kwa jumla sekta zote zimeweza kupiga hatua kubwa za mafanikio kwa kuzingatia mipango yetu mikuu ya maendeleo; Ilani ya uchaguzi ya CCM 2020/2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar na Malengo mengine ya Kikanda na Kimataifa kama ambavyo imeelezwa kwa kina kupitia majukwaa mbali mbali na vyombo vya habari mwezi uliopita wakati nchi yetu inaadhimisha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Nane.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-31T18:08:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI KATIKA HAFLA YA KILELE CHA SHEREHE ZA MWEZI WA SHUKURANI NA FURAHA KWA WALIPA KODI KATIKA UKUMBI WA HO</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-hafla-ya-kilele-cha-sherehe-za-mwezi-wa-shukurani-na-furaha-kwa-walipa-kodi-katika-ukumbi-wa-ho</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-hafla-ya-kilele-cha-sherehe-za-mwezi-wa-shukurani-na-furaha-kwa-walipa-kodi-katika-ukumbi-wa-ho#When:11:46:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI KATIKA HAFLA YA KILELE CHA SHEREHE ZA MWEZI WA SHUKURANI NA FURAHA KWA WALIPA KODI KATIKA UKUMBI WA HOTELI YA GOLDEN TULIP ZANZIBAR<br />
TAREHE: 29 DISEMBA,2023<br />
Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla; <br />
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,<br />
<br />
Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid; <br />
Spika wa Baraza la Wawakilishi,<br />
<br />
Mheshimiwa Khamis Ramadhan Abdalla; <br />
Jaji Mkuu wa Zanzibar,<br />
<br />
Mheshimiwa Saada Mkuya Salum; <br />
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Fedha na Mipango,<br />
<br />
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri Mliopo,<br />
<br />
Mhandisi Zena Ahmed Said; <br />
Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi,<br />
<br />
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya <br />
Makatibu Wakuu na Wakurugenzi wa Taasisi <br />
mbali mbali za Serikali,<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA),<br />
<br />
Viongozi mbali mbali wa Vyama vya Siasa na Sekta binafsi <br />
<br />
Walipakodi na Wageni waalikwa,<br />
<br />
Waandishi wa Habari,<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
<br />
Mabibi na Mabwana<br />
Assalamu Aleikum<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu, Mwingi wa rehema kwa kutujaalia uhai na afya njema na kutuwezesha kukutana katika hafla hii ya siku ya kilele cha Sherehe za Mwezi wa shukurani kwa walipakodi ambayo huandaliwa maalum kwa madhumuni ya kutambua mchango wa walipa kodi wetu.<br />
<br />
Natoa shukrani zangu za dhati kwa uongozi wa Afisi ya Rais Fedha na Mipango na Mamlaka ya Mapato Zanzibar kwa maandalizi mazuri ya shughuli hii na kwa kunialika kuwa Mgeni Rasmi. Shukrani zangu za pekee nazitoa kwenu ndugu wafanyabiashara na walipakodi nyote kwa ushirikiano wenu na kwa kutimiza wajibu wenu wa kisheria wa kulipa kodi kwa hiari ili kuiwezesha Serikali kukusanya mapato ya kuendesha shughuli zake za kuwatumikia wananchi.<br />
<br />
<br />
Ndugu Wananchi na Walipa kodi,<br />
Nimepata faraja kujumuika pamoja nanyi katika sherehe inayoandaliwa kila mwaka na Mamlaka ya Mapato ya Zanzibar katika mwezi wa Disemba ambayo lengo lake kuu ni kujenga uhusiano mwema baina ya ZRA na walipa kodi, kusikiliza mahitaji yao, kuhamasisha ulipaji kodi wa hiari na kupokea maoni juu ya namna bora zaidi ya kuimarisha ulipaji kodi. Kwa msingi huo, hafla hii ina umuhimu wa kipekee kwa ZRA kupata wasaa wa kukaa pamoja na wateja wake ambao ni nyinyi walipa kodi kusikiliza maoni yenu ili kuiwezesha Mamlaka ya Mapato Zanzibar kupata ufanisi katika kutimiza majukumu yake ya usimamizi na ukusanyaji wa mapato Zanzibar.<br />
Idadi kubwa ya washiriki wa shughuli hii na mafanikio ambayo nchi yetu inaendelea kuyapata katika kuongezeka kwa mapato yanayokusanywa na ZRA kila mwaka, yananipa faraja kuona kuwa mwamko wa ulipaji wa kodi kwa hiari hapa Zanzibar umazidi kuimarika.<br />
<br />
Hali hii inanipa matumaini kwamba walipakodi mnajua wajibu wenu huo na kuamini kuwa hakuna nchi duniani ikiwemo Zanzibar inayoweza kupiga hatua za maendeleo bila ya kukusanya kodi zake kwa ufanisi. Mapato yanayotokana na kodi ni njia kuu na ya uhakika ya kuipatia fedha Serikali na kuiwezesha kutoa huduma ipasavyo kwa wananchi. Kwa hivyo, nachukua fursa hii kukupongezeni walipakodi wetu kwa kulitambua hilo na kutimiza wajibu wenu. Hongereni sana<br />
<br />
<br />
Ndugu Wananchi na Walipa kodi <br />
Nimefurahi kusikia kuwa katika kipindi hiki cha mwezi mmoja, ZRA imekitumia katika   kuimarisha matumizi ya mifumo ya kieleketroniki katika  ukusanyaji wa mapato kwa kusimamia vyema mfumo wa utoaji wa risiti za kielektroniki (VFMS), na kutoa mafunzo yanayohusiana na jinsi ya kurekebisha risiti za kielektroniki zinazokosewa badala ya kuandika barua ZRA ili kuomba kufanyiwa marekebisho. Hii ni hatua nzuri na muhimu kwani inaondoa usumbufu na ina mchango muhimu katika kurahisisha ufanyaji wa biashara hapa Zanzibar. <br />
<br />
Nawapongeza ZRA kwa jitihada zao za kuimarisha matumizi ya mifumo kwani nimeelezwa kuwa hivi sasa wanakamilisha utengenezaji wa mfumo mpya wa kusimamia ukusanyaji wa mapato ya kodi ZIDRAS unaoitwa (Zanzibar Integrated Domestic Revenue Administration System). Mfumo huu ambao nimeuzindua karibuni, umeanza kutumika mwezi wa Aprili, 2023 kwa kuwasajili walipakodi 2,340 wakiwemo walipa kodi wakubwa 186. Huu ndio mfumo utakaotumika badala ya mfumo wa ZITAS ulioanza kutumika tokea mwaka 2012 na kubainika kuwa na changamoto nyingi. Nimeelezwa kuwa mfumo huu  wa  ZIDRAS una manufaa mengi ambayo naamini mtapatiwa maelezo ya kina kuhusu faida zake. Napenda nikuahidini kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika mifumo ya uendeshaji <br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-30T11:46:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI,&amp;nbsp; KATIKA  HAFLA YA UZINDUZI WA VIWANJA VYA MICHEZO MATUMBAKU,&amp;nbsp; TAREHE: 30 DISEMBA, 2023</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-hafla-ya-uzinduzi-wa-viwanja-vya-michezo-matumbaku-tarehe-30-disemba-2023</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-katika-hafla-ya-uzinduzi-wa-viwanja-vya-michezo-matumbaku-tarehe-30-disemba-2023#When:11:41:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI,  KATIKA  HAFLA YA UZINDUZI WA VIWANJA VYA MICHEZO MATUMBAKU, <br />
TAREHE: 30 DISEMBA, 2023<br />
<br />
Mheshimiwa Dkt. Saada Mkuya Salum; <br />
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Fedha na Mipango,<br />
<br />
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri mliopo<br />
katika hafla hii,<br />
<br />
Mheshimiwa Mhandisi Zena Ahmed Said; <br />
Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi,<br />
<br />
Dkt. Moh’d Said Moh’d (Dimwa) <br />
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar,<br />
<br />
Mheshimiwa  Idrissa Kitwana Mustafa; <br />
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja,<br />
<br />
Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu <br />
wa Wizara mliopo katika hafla hii,<br />
<br />
Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama,<br />
<br />
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Mfuko wa <br />
Hifadhi ya Jamii Zanzibar,<br />
<br />
Mkurugenzi Mwendeshaji Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar,<br />
<br />
Viongozi  mbali mbali wa Serikali na Vyama vya Siasa,<br />
<br />
Ndugu Waandishi wa Habari,<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
<br />
Mabibi na Mabwana.<br />
<br />
Assalam Aleikum.<br />
<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema kwa kutujaalia neema ya uhai na afya njema na kutuwezesha kukutana hapa kwa lengo la kushiriki hafla ya Uzinduzi wa Viwanja vya Michezo vya Kisasa katika eneo la Matumbaku hapa Miembeni Zanzibar.<br />
<br />
Natoa shukrani zangu za dhati kwako Mheshimiwa Saada Mkuya Salum Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha na Mipango pamoja na wote walioshiriki kunialika niwe mgeni rasmi katika shughuli hii muhimu kwa maendeleo ya sekta ya michezo katika nchi yetu. Shukrani zangu maalum nazitoa kwenu viongozi nyote mliopo hapa, waalikwa na wananchi wote mliojitokeza kwa wingi katika kufanikisha shughuli hii. Nakushukuruni sana.<br />
<br />
Ndugu Wananchi, <br />
Tunakutana tena katika viwanja hivi kwa mara ya pili, ambapo siku ya tarehe 09 Januari,2023  tulikuwa hapa kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa viwanja vitatu vya mpira wa miguu. Nachukua fursa hii kutoa pongezi kwa Wizara ya Habari, vijana, Utamaduni na Michezo na Afisi ya Rais Fedha na Mipango pamoja na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar kwa <br />
<br />
<br />
kuyasimamia vyema maagizo niliyoyatoa siku ya uwekaji wa jiwe la msingi. Mtakumbuka niliagiza kuwa viwanja hivi ni lazima viwe vya kisasa vyenye muonekano mzuri kwa kujenga uzio na maegesho ya gari pamoja na kuweka sakafu maeneo yote. Pia nikaagiza kujengwa kwa viwanja vyengine kwa ajili ya michezo mingine ya mpira wa wavu (volleyball), mpira wa kikapu (basketball) na mpira wa kikapu (netball). <br />
<br />
Katika hotuba yangu niliyoitoa siku hiyo niliahidi ya kuwa katika sherehe za miaka 60 ya Mapinduzi, tutarudi tena kufungua viwanja hivi baada ya kukamilika. Leo hii tupo hapa, nafarajika kuona kuwa kauli niliyoitoa siku ile na vyote nilivyoagiza vimezingatiwa na viwanja vimekamilika. Shukrani zangu ziende kwa watu wote waliofanikisha  kukamilisha ujenzi wa viwanja hivi. Kwa hakika tuna haki ya kujivunia mafanikio makubwa ambayo nchi yetu imeyapata kwa ujenzi wa viwanja vya michezo vya kisasa ikizingatiwa kuwa juzi tu tumeufungua uwanja mpya wa Amaan uliofanyiwa matengenezo makubwa na hivi sasa umepata haiba mpya na kukidhi viwango vya michezo vya kimataifa.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-30T11:41:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA MKUU WA CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR AMBAE PIA NI RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK.HUSSEIN ALI MWINYI KATIKA MAHAFALI YA 19 YA CHUO KIKUU CHA TAIFA C</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-mkuu-wa-chuo-kikuu-cha-taifa-cha-zanzibar-ambae-pia-ni-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk.hussein-ali-mwinyi-katika-mahafali-ya-19-ya-chuo-kikuu-cha-taifa-c</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-mkuu-wa-chuo-kikuu-cha-taifa-cha-zanzibar-ambae-pia-ni-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk.hussein-ali-mwinyi-katika-mahafali-ya-19-ya-chuo-kikuu-cha-taifa-c#When:12:51:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA MKUU WA CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR AMBAE PIA NI RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK.HUSSEIN ALI MWINYI KATIKA MAHAFALI YA 19 YA CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR (SUZA) <br />
TAREHE: 28 DISEMBA, 2023<br />
Mheshimiwa Othman Masoud Othman; <br />
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar; <br />
<br />
Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdullah; <br />
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar;  <br />
<br />
Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid; <br />
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar;<br />
<br />
Mheshimiwa Khamis Ramadhan Abdalla; <br />
Jaji Mkuu wa Zanzibar;<br />
<br />
Mheshimiwa Lela Moh’d Mussa; <br />
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali,<br />
<br />
Waheshimiwa Mawaziri wote Mliohudhuria;<br />
<br />
Mhandisi Zena Ahmed Said: <br />
Katibu Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi;<br />
<br />
Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud; <br />
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja;<br />
<br />
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar;<br />
<br />
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar;<br />
<br />
Manaibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar;<br />
Waheshimiwa Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,<br />
<br />
Viongozi na Watendaji mbali mbali wa Serikali mliopo;<br />
<br />
Ndugu Wahadhiri na Wafanyakazi wa SUZA;<br />
<br />
Ndugu Wahitimu na Wageni Waalikwa;<br />
<br />
Ndugu waandishi wa habari;<br />
<br />
Mabibi na Mabwana,  <br />
<br />
Assalamu Alaikum<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema kwa kutujaalia uhai na afya njema nakutuwezesha kukutana katika Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.  Pili, natoa shukrani zangu za dhati kwa Uongozi na jumuiya yote ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kwa maandalizi mazuri ya  Mafahali haya ya 19.<br />
<br />
Napenda fursa hii kuwakaribisha waalikwa nyote katika Mahafali haya ya 19 ya Chuo Kikuu Cha Taifa Cha Zanzibar. Natoa shukrani zangu kwa mahudhurio makubwa ya waalikwa kutoka taasisi za Serikali, taasisi binafsi na wanajamii kuja kuungana na jumuiya ya chuo katika shughuli hii ya mahafali ikiwa ni kuunga mkono jitihada za maendeleo za Chuo chetu katika kuandaa wataalamu wa fani mbali mbali ambao leo tumekuja kushuhudia wakihitimu. <br />
<br />
Ndugu Wananchi na Wageni Waalikwa.<br />
Tukiwa katika mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha SUZA, tunajivunia mafanikio ambayo chuo hiki kinaendelea kuyapata kila mwaka hususan ongezeko la wahitimu katika kozi zinazofundishwa na chuo hiki. Tumeelezwa kuwa kwa mwaka wa masomo 2022/2023, jumla ya wahitimu 2,102 wanatarajiwa kutunukiwa shahada mbali mbali leo hii. Idadi hii ni sawa na ongezeko la asilimia 9 ukilinganisha na idadi ya wahitimu 1,913 wa mwaka jana. Napenda niupongeze uongozi wa chuo, wahadhiri,  wafanyakazi na uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mafanikio ambayo Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kinaendelea kuyapata katika kuundaa wataalamu wa  kusuma mbele maendeleo ya nchi yetu. Sina shaka kwamba wahitimu hawa 2,102  wameandaliwa vizuri.  <br />
<br />
Chuo chetu kinaendelea kuwa bora kwa kuwaandaa vijana wetu kuwa mahiri na wenye weledi kitaaluma, wenye uzalendo na raia wema watakaotoa mchango muhimu katika sekta mbali mbali za maendeleo pamoja na kuhimili ushindani katika soko la ajira. <br />
<br />
Ndugu Wananchi na Wageni Waalikwa.<br />
Serikali zetu zote mbili; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tumejiandaa kuhakikisha kuwa vijana wote wenye sifa za kujiunga na vyuo vikuu, wanapatiwa mikopo ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao. Nachukua fursa hii kuzipongeza Bodi  zetu mbili za Mikopo ya Wanafunzi. Bodi Mikopo ya Elimu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ya Zanzibar kwa kushirikiana na kuhakikisha  vijana wote waliodahiliwa katika vyuo vikuu, na wanaohitaji mikopo wanapatiwa. <br />
<br />
Ndugu Wananchi na Wageni Waalikwa<br />
Katika kutathmini maendeleo ya Chuo chetu cha SUZA, nakupongezeni kwa kuona umuhimu wa kuongeza wigo wa ushirikiano na taasisi za kiserikali pamoja na taasisi binafsi. Nafahamu kuwa SUZA imekuwa ikishiriki katika maonesho, makongamo na warsha mbali mbali za kijamii na kitaaluma. Hatua hiyo ni muhimu kwani inatoa fursa ya kujifunza, kuendeleza uhusiano mwema na kutoa faraja kwa wananchi wa Zanzibar kwa kuona Chuo Kikuu cha Taifa kinatoa mchango wake kwa jamii. Napenda nikuhimizeni kuendelea kutekeleza wajibu wetu wa kufanya tafiti zenye lengo la kupata ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili jamii na kutoa ushauri wa kitaalam.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-28T12:51:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh  Idris Abdul Wakil Kikwajuni</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mhe.dk.hussein-ali-akizungumza-katika-maadhimisho-ya-siku-ya-maadili-na-haki-za-binadamu-zanzibar-katika-ukumbi-wa-sheikh-idriss-abdul-wakil-kikw</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mhe.dk.hussein-ali-akizungumza-katika-maadhimisho-ya-siku-ya-maadili-na-haki-za-binadamu-zanzibar-katika-ukumbi-wa-sheikh-idriss-abdul-wakil-kikw#When:11:24:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK. HUSSEIN ALI MWINYI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU KWENYE UKUMBI WA SHEIKH  IDRIS ABDUL WAKIL<br />
TAREHE: 18 DISEMBA, 2023<br />
<br />
Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdullah; <br />
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,<br />
<br />
Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid; <br />
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar,<br />
<br />
Mheshimiwa Khamis Ramadhan Abdulla; <br />
Jaji Mkuu wa  Zanzibar,<br />
<br />
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Maziri,<br />
<br />
Mheshimiwa Idrisa Kitwana Mustafa; <br />
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi,<br />
<br />
Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,<br />
<br />
Viongozi wa Serikali mliohudhuria,<br />
<br />
Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia,<br />
<br />
Wakuu  wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama,<br />
<br />
Wageni Waalikwa,<br />
<br />
Mabibi na Mabwana.    <br />
<br />
Assalamu Aleykum,<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu, mwingi wa Rehema, kwa kutujaalia uzima na afya njema na kutuwezesha ya kukutana hapa katika Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binaadamu.<br />
<br />
Natoa shukrani zangu za dhati kwa uongozi wa Wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora kwa matayarisho mazuri na kwa kunialika kuwa mgeni rasmi katika shughuli hii.<br />
<br />
Nawashukuru watendaji wote wa taasisi za Serikali, Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia na wananchi kwa jumla kwa kuja kujumuika pamoja na sisi kwa ajili ya kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binaadamu ambayo huadhimishwa kila mwaka. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Maadhimisho haya yanatupa fursa ya kujadili mustakabali wa nchi yetu na kutafakari namna bora ya kuimarisha utawala bora na misingi yake ikiwemo utawala wa sheria, uwajibikaji, uwazi, uadilifu, haki za binaadamu na kupiga vita rushwa.<br />
<br />
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zimekubaliana kwa pamoja kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binaadamu Kitaifa kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka. <br />
<br />
Maadhimisho haya yanatokana na maadhimisho ya Siku ya Kupambana na Rushwa Duniani kila ifikapo tarehe 9 Disemba pamoja na maadhimisho ya Siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika tarehe 10 Disemba ya kila mwaka. Kwa kuwa siku ya tarehe 9 Disemba ya kila mwaka, ni Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara, hivyo Siku ya Maadili na Haki za Binaadamu huadhimishwa baada ya Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara. Uamuzi huu umekusudia kutoa nafasi kwa wananchi kuungana na mataifa mengine Duniani katika harakati za mapambano dhidi ya Rushwa na kulinda Haki za Binaadamu. Kwa upande mwengine kutoa nafasi ya kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania Bara. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Historia inaeleza kuwa haki za Binaadamu zinatokana na tamko la kimataifa lililoidhinishwa na kupitishwa na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Disemba mwaka 1948. Madhumuni ya Tamko hilo ni kukuza na kuimarisha misingi ya Haki za Binaadamu Duniani. Barani Afrika masuala ya haki za binadamu yamo katika tamko la Afrika la Haki za Binadamu na Watu (African Charter on Human and People’s Rights). Kwa Tanzania masuala ya Haki za Binadamu yameingizwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Sura ya Kwanza Sehemu ya Tatu na hapa Zanzibar masuala haya yameingizwa katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 Sura ya Tatu.<br />
<br />
Katika kukuza, kulinda na kutetea haki za binaadamu na misingi ya utawala bora nchini, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianzisha Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na baadae Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikaridhia Tume hiyo kutekeleza majukumu yake hapa Zanzibar kupitia Sheria Na. 12 ya 2003. Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume huandaa na kutoa ripoti ya kila mwaka yenye mapendekezo kwa Serikali zote mbili kuhusiana na hali ya Haki za Binaadamu na Utawala bora nchini.<br />
<br />
Aidha, Msingi wa Siku ya Kupambana na Rushwa Duniani unatokana na Azimio la Umoja wa Mataifa lililosainiwa tarehe 9/12/2003 pamoja na Mkataba wa Umoja wa Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa na mwaka 2003 ambao ulianza kutumika rasmi Barani Afrika mwaka 2005. Lengo la Azimio na Mkataba huo ni kupinga rushwa Kimataifa, Kikanda na Kitaifa. Kwa hapa Zanzibar masuala ya kupambana na Rushwa yameingizwa katika Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 na kupewa umuhimu wake kwa kutungwa kwa Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi. Sheria hiyo imetoa fursa kwa wananchi wote kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa. <br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Maadhimisho haya ya Siku ya Maadili na Haki za Binaadamu nchini yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo:-<br />
“Tuimarishe Utawala Bora na Haki za Binaadamu kwa Kuondoa Ubadhirifu na Kukuza Maadili kwa Ustawi wa Jamii”.<br />
<br />
Ni Dhahiri kuwa Kaulimbiu hii imelenga katika kusisitiza umuhimu wa kuimarisha misingi ya Utawala Bora na Haki za Binaadamu, kudhibiti ubadhirifu na kukuza maadili ili wananchi waweze kupata maendeleo yaliyokusudiwa.<br />
<br />
Kwa kiasi kikubwa tumefanikiwa kutekeleza kwa ufanisi lengo la Serikali yetu la kufikisha maendeleo kwa wananchi wake. Maendeleo haya yanayoonekana na yanayokuja yanatokana na kuwa na misingi imara ya utawala bora ikiwemo kusimamia utawala wa sheria, haki, uwajibikaji, uwazi, usawa, uadilifu, kuzuia rushwa na ubadhirifu wa mali za umma. Hivyo kila taasisi ya Serikali, Binafsi, Asasi za Kiraia, Asasi za Kidini na kila mwananchi kwa nafasi yake, ana wajibu wa kusimamia na kutekeleza misingi ya utawala bora kwa manufaa ya maendeleo yetu.<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Suala la kuimarisha misingi ya Utawala Bora si la Serikali na taasisi zake pekee bali ni la wote likijumuisha Jumuiya za Kimataifa, Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi, Viongozi wa Dini, Vyombo vya Habari na Wananchi kwa ujumla. Hivyo Serikali pamoja na makundi hayo yote kwa umoja wao yana mchango mkubwa katika kuheshimu na kuimarisha maadili, haki za binadamu, uwajibikaji, uwazi na kupiga vita rushwa. Kwa mantiki hiyo, Serikali imeanzisha taasisi mbalimbali zinazosimamia masuala ya Utawala Bora nchini. Miongoni mwa Taasisi hizo ni pamoja na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi, Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora pamoja na Idara ya Utawala Bora. Kila Taasisi imeanzishwa na kupewa jukumu lake maalum katika kuimarisha na kusimamia misingi ya Utawala Bora nchini.<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma imepewa jukumu la kusimamia maadili ya viongozi wa umma nchini, kupitia Sheria Na. 4 ya 2015 kwa lengo la kuimarisha misingi ya utawala bora ikiwemo uwazi na uwajibikaji. Miongoni mwa mafanikio ya Tume ya Maadili kwa mwaka wa 2022/2023 imepokea, kusajili na kuhifadhi jumla ya Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Viongozi 2,686 sawa na asilimia 107 ya shabaha iliyopangwa. Kati ya Fomu hizo, Fomu zilizowasilishwa ndani ya muda ni 2,677 na zilizowasilishwa nje ya muda ni 11. Takwimu zinaonesha kwamba idadi ya viongozi wanaochelewa kurejesha Fomu inapungua ukilinganisha na miaka iliyopita. Hali hii inathibitisha kwamba Tume ya Maadili inaendelea kutekeleza kikamilifu jukumu lake la kutoa elimu kila mwaka kwa kukutana na viongozi wote katika Wizara na taasisi zao. Hata hivyo, kwa kuwa kuchelewa kurejesha Fomu kwa wakati bila ya sababu za msingi ni kosa la kimaadili kwa mujibu wa Sheria, hatua zimeendelea kuchukuliwa kwa viongozi waliochelewa kurejesha Fomu kama inavyoelekezwa na Sheria.<br />
<br />
Ndugu Wananchi,<br />
Katika kutekeleza jukumu la msingi la Uhakiki wa Taarifa za Mali na Madeni ya Viongozi wa Umma, kwa mwaka wa 2022/2023 jumla ya viongozi 233 wamehakikiwa taarifa zao za mali na madeni. Idadi hii ni sawa na asilimia 117 ya shabaha ya Viongozi 200 waliopangwa kuhakikiwa. Ni jambo zuri kuona idadi ya Viongozi wanaohakikiwa inaongezeka ukilinganisha na miaka iliyopita. Licha ya Tume ya Maadili kuendelea kutekeleza jukumu hili, bado kuna tatizo la kukosekana kwa nyaraka za umiliki wa mali zilizoorodheshwa kwenye Fomu za Tamko la Mali na Madeni. Viongozi wengi wameorodhesha mali ambazo ama hawajakamilisha taratibu za uhaulishaji wa mali hizo au hawana nyaraka halisi za umiliki. Hivyo, natoa wito kwa viongozi kukamilisha utaratibu wa uhaulishaji wa mali zao ili kurahisisha uwekaji wa kumbukumbu sahihi za taarifa na mali zao katika Daftari la Usajili wa Taarifa za Mali na Madeni za Viongozi wa Umma. Kadhalika, taasisi zinazohusika na uhaulishaji zinapaswa kuchukuwa hatua mahususi za kuharakisha kazi hiyo.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-19T11:24:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa  Dk. Hussein Ali Mwinyi kwenye Ufunguzi wa Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-kwenye-ufunguzi-wa-kikao-cha-77-cha-tume-ya-afrika-ya-haki-za-binadamu-na-watu</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mheshimiwa-dk-hussein-ali-mwinyi-kwenye-ufunguzi-wa-kikao-cha-77-cha-tume-ya-afrika-ya-haki-za-binadamu-na-watu#When:11:16:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa  Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ufunguzi wa Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Tarehe; 20 Oktoba, 2023<br />
<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti wa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu;<br />
<br />
Mheshimiwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu;<br />
<br />
Wahesimiwa Makamishna wa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu;<br />
<br />
Waheshimiwa Wawakilishi wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika,<br />
<br />
Viongozi Mbalimbali wa Nchi na Serikali,<br />
<br />
Waheshimiwa Mabalozi,<br />
<br />
Wadau wa Mbalimbali wa Maendeleo,<br />
<br />
Waheshimiwa Wenyeviti na Makamishna wa Taasisi za Kitaifa za Haki za Binadamu,<br />
<br />
Washiriki Kutoka Taasisi Zisizo za Kiserikali<br />
<br />
Wananchi Mliopo,<br />
<br />
<br />
<br />
Waandishi wa Habari,<br />
<br />
Mabibi na Mabwana,<br />
<br />
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutujaalia  neema ya uhai na kutuwezesha kukutana hapa leo katika hafla ya ufunguzi wa kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).Kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda nikupongeze Mheshimiwa Prof. Remy Ngoy Lumbu, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Watu kwa uongozi wako imara katika kuiongoza taasisi hii muhimu ya Umoja wa Afrika, Taasisi ambayo inalinda, inakuza na kuendeleza haki za binadamu na watu katika Bara la Afrika. <br />
<br />
Pia, niwapongeze Makamishina wote wa Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ambao mnashirikiana pamoja katika kuimarisha haki za binadamu na watu katika bara la Afrika. HONGERENI SANA.<br />
<br />
Ndugu Washiriki,<br />
Kikao hiki ni matokeo ya ziara ya Mwenyekiti wa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu aliyoifanya nchini Tanzania tarehe 30 Januari, 2023, ambapo pamoja na masuala mengine yaliyojadiliwa, pia aliomba mkutano huu ufanyike hapa Tanzania. Hivyo, kwa niaba Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, natumia fursa hii kuwashukuru kwa uamuzi wenu wa kufanya kikao cha 77 cha Kawaida cha Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu hapa nchini Tanzania. <br />
<br />
Ndugu Washiriki,<br />
Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote, napenda kuwakaribisha viongozi na waalikwa wote kutoka nchi mbalimbali wakiwemo; Waheshimiwa Mawaziri; Mabalozi na Viongozi wa Taasisi za Kitaifa za Haki za Binadamu na Asasi za Kiraia (AZAKI); pamoja na wawakilishi wa Serikali na makundi mbalimbali kutoka Bara la Afrika.<br />
<br />
Nimejulishwa kuwa katika mkutano huu, yatajadiliwa masuala mbalimbali ikiwemo hali ya haki za binadamu katika bara la Afrika, taarifa za kazi za Makamishna pamoja na taarifa za mifumo ya ulinzi wa haki za binadamu Afrika. Ni matumaini yangu kuwa taarifa hizi zitatoa tathimini ya hali halisi ya haki za binadamu na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kupata mbinu za kukabiliana na changamoto zitakazoainishwa. Aidha, naamini kwamba washiriki watapata fursa ya kutoa maoni na mapendekezo yao kuhusiana na masuala yatakayojitokeza katika taarifa zitakazo wasilishwa.<br />
<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-10-20T11:16:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>HOTUBA YA BAJET YA WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS &#45;IKULU  MHESHIMIWA JAMAL KASSIM ALI KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA  FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 MEI, 2023</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-jamal-kassim-ali-kuhusu-makadirio-ya-matumizi-ya-fedha-kwa-mwaka-wa-fedha-2023-2024-mei-2023</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-jamal-kassim-ali-kuhusu-makadirio-ya-matumizi-ya-fedha-kwa-mwaka-wa-fedha-2023-2024-mei-2023#When:09:23:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS -IKULU  MHESHIMIWA JAMAL KASSIM ALI KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA  FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA<br />
2023/2024 MEI, 2023<br />
<br />
YALIYOMO	i<br />
<br />
ORODHA YA VIAMBATISHO	ii<br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO	iv<br />
<br />
UTANGULIZI	1<br />
<br />
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS – IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023	5<br />
<br />
MAFANIKIO YA FUNGU A01	5<br />
<br />
MAFANIKIO YA FUNGU A02 BARAZA LA MAPINDUZI	44<br />
<br />
MWELEKEO WA BAJETI YA AFISI RAIS IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024	46<br />
<br />
PROGRAMU KUU NA NDOGO NA MAKISIO YA FEDHA ZINAZOHITAJIKA KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024       47<br />
<br />
PROGRAMU KUBWA NA NDOGO ZA FUNGU A01	49<br />
<br />
PROGRAMU KUBWA NA NDOGO ZA FUNGU A02	53<br />
<br />
PROGRAMU KUBWA NA NDOGO ZA FUNGU A09	56<br />
<br />
PROGRAMU KUBWA NA NDOGO ZA FUNGU A10.	58<br />
<br />
MAMBO MAKUU YATAKAYOTEKELEZWA NA AFISI YA RAIS -IKULU KWA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA WA 2023/2024	60<br />
<br />
MAOMBI YA FEDHA YA KAZI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024	61<br />
<br />
HITIMISHO	61<br />
<br />
ORODHA YA VIAMBATISHO <br />
<br />
Kiambatisho 1. Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Bajeti ya mwaka 2023/2024	63<br />
<br />
Kiambatisho 2. Malalamiko yaliyowasilishwa na Wananchi kwa Taasisi 59 za Serikali zilizounganishwa katika Mfumo wa Sema na Rais kwa Julai – Machi 2022/2023	<br />
70<br />
<br />
Kiambatisho 3. Orodha ya Malalamiko yaliyowasilishwa na Wananchi kwa Kipindi cha Miezi 9 Julai - Machi 2022/2023............................................. 74<br />
<br />
Kiambatisho 4. Mchanganuo wa Takwimu za Malalamiko kwa Mwezi katika kipindi cha Julai – Machi 2022/2023 kupitia Mfumo wa Sema na Rais	75<br />
<br />
Kiambatisho 5. Idadi ya Watumishi Waliopekuliwa kwa Wizara/Taasisi	90<br />
<br />
Kiambatisho 6. Idadi ya Watumishi Waliopatiwa Mafunzo kwa Wizara/Taasisi.	93<br />
<br />
Kiambatisho 7. Idadi ya Majengo ya Serikali yaliyofanyiwa Ukaguzi wa Kiusalama	94<br />
<br />
Kiambatisho 8. Orodha ya Wizara, Idara na Taasisi zilizofanyiwa Ukaguzi kwa kipindi cha Julai-Machi, 2023     96 Kiambatisho 9. Idadi ya Watafiti wa Ndani na kutoka Nje ya Nchi walaiotembelea Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu kwa kipindi cha Julai-Machi 2023	100<br />
<br />
Kiambatisho 10. Wageni wa ndani ya Nchi	101<br />
<br />
<br />
VIFUPISHO VYA MANENO<br />
<br />
<br />
AfCFTA	African Continental Free Trade Area (Eneo huru la Biashara Barani Afrika)<br />
AFD	Jumuiya ya Maendeleo ya Ufaransa<br />
CCM	Chama cha Mapinduzi<br />
EAC	East Africa Community (Jumuiya ya Afrika Mashariki)<br />
GCC	Global Cooperation Committee<br />
IORA	Indian Ocean Rim Association (Jumuiya ya Nchi zilizopakana na Bahari ya Hindi<br />
JPC	Joint Permanent Commission (Tume ya kudumu ya Pamoja)<br />
PDB	Presidential Delivery Beaureu<br />
SADC<br />
TADIO                 	Southern African Development Community (Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika)<br />
Tanzania Diaspora in Oman (Jumuiya ya Wanadiapora wa Tanzania Nchini Omani).<br />
UNFPA	Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu<br />
UNHIF	Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya<br />
WTTC	World Travel and Tourism Council Global Summit<br />
<br />
ZACADIA	Jumuiya ya Wazanzibari Wanaoishi Nchini Canada (ZACADIA)<br />
ZADEP	Zanzibar Development Plan<br />
ZAWA	Mamlaka ya Maji (Zanzibar Water Authority)<br />
ZBA	Wakala wa Ujenzi Zanzibar<br />
ZBC	Shirika la Utangazaji Zanzibar (Zanzibar Broadcasting Corporation)<br />
ZCTV	Zanzibar Cable Televishion<br />
ZEMA	Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar<br />
ZIPA	Mamlaka ya Ukuzaji Vitega Uchumi Zanzibar<br />
ZPDC	Zanzibar Petroleum Development company<br />
ZPRA	Zanzibar Petroleum Regulatory Authority<br />
<br />
UTANGULIZI<br />
1.Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwa Baraza lako tukufu kujadili na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Afisi ya Rais–Ikulu kwa kazi za kawaida na Maendeleo kwa mwaka  wa fedha 2023/2024.<br />
<br />
2.Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kutujaalia mazingira ya amani na utulivu ambayo yametupa nguvu, mshikamano na imani ya kuendelea kumsaidia Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kutekeleza majukumu ya kuongoza Zanzibar. <br />
<br />
3.Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee napenda kumshukuru Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa imani yake kubwa kwangu kwa kuendelea kuniamini kusimamia Afisi                       ya Rais–Ikulu Zanzibar. Vile vile namshukuru Mheshimiwa Rais kwa safu nzuri ya Watendaji wa Afisi yangu ambao amewaidhinisha.<br />
<br />
4.Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii, kumpongeza Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutimiza miaka miwili (2) na kupata mafanikio makubwa ya utendaji wa kazi yanayoonekana katika sekta mbali mbali nchini. Aidha kipekee nampongeza kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Zanzibar. Mheshimiwa Rais wetu amedhihirisha kuwa yeye ni kiongozi bora, muadilifu, mzalendo, mchapa kazi, mpenda mashirikiano na mwenye nia ya kweli katika kuleta  maendeleo nchini.<br />
<br />
5.Mheshimwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumpongeza Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake bora, uliojaa uzalendo na maono ambao umechochea kuimarika kwa diplomasia hususani diplomasia ya uchumi baina ya nchi yetu na nchi yengine na mashirika ya kimataifa.<br />
<br />
<br />
6.Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Othman Masoud Othman  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Mhe Hemed Suleiman Abdallah Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa kuendelea kumsaidia  Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa                             Baraza la Mapinduzi katika kufanikisha majukumu yake ya kuiletea nchi yetu maendeleo.<br />
<br />
<br />
<br />
7.Mheshimiwa Spika, naomba pia kuwapongeza Mawaziri wenzangu wote wa Serikali ya Awamu ya nane kwa kuendelea kupewa nafasi ya kuwatumikia Wananchi na kutekeleza Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.<br />
<br />
8.Mheshimiwa Spika, namshukuru Mhandisi Zena Ahmed Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi kwa kazi nzuri anazozifanya katika kutekeleza majukumu yanayoiwezesha Serikali kufikia malengo yake, ikiwa ni pamoja na kuwasimamia Makatibu Wakuu kwa                                    ufanisi.<br />
<br />
9.Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naishukuru Kamati ya Kudumu ya kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Machano Othman Said, Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini na Makamu wake Mheshimiwa Mtumwa Peya Yussuf, Mwakilishi wa Jimbo la Bumbwini, pamoja na Wajumbe wa Kamati kwa ushirikiano, maelekezo na ushauri mzuri wanao tupatia ambao umetuwezesha kuimarisha utendaji wetu wa kazi.<br />
<br />
10.Mheshimiwa Spika, aidha, naishukuru Kamati ya Bajeti ya Baraza lako tukufu chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Abdullah Hussein Kombo Mwakilishi wa Jimbo la Mkoani pamoja na Makamu wake Mhe. Asha Abdallah Mussa Mwakilishi wa   Jimbo la Mahonda pamoja na wajumbe wa kamati kwa michango na miongozo waliotupatia tulipopata bahati ya kuwasilisha Taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Uimarishaji wa Nyumba za Viongozi kwa mwaka 2022/2023 sambamba na kufanya ziara katika maeneo ya mradi.<br />
<br />
Mheshimiwa Spika, naomba nikamilishe pongezi zangu kwa namna ya pekee kwako wewe binafsi Mhe. Spika, naibu wako na wenyeviti wa Baraza kwa kuendelea kuliongoza Baraza letu kwa umahiri na mafanikio makubwa. Pili wawakilishi wote kwa kazi nzuri wanazozifanya na ushirikiano wanaonipatia katika utekelezaji wa majukumu ya yangu. Tatu na mwisho napenda kuipongeza na kuishukuru familia yangu  na wapiga kura wa jimbo la Magomeni ambao wameendelea kunipatia upendo, ushirikiano na uvumilivu mkubwa hata pale ninapokuwa nimebanwa na majukumu ya kitaifa nje ya Jimbo langu la uchaguzi. Naahidi kuendelea kushirikiana nanyi katika kuliletea maendeleo jimbo letu na nchi yetu kwa ujumla.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-05-15T09:23:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>MHESHIMIWA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK. HUSSEIN ALI MWINYI AMEKUTANA NA UONGOZI WA SHIRIKA LA NYUMBA TAREHE 27 FEBRURI,2023  NA KUSIKILIZA  CHANGAMOTO ZA WANANCHI ZILIZOWA</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/mheshimiwa-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-dk-hussein-ali-mwinyi-amekutana-na-uongozi-wa-shirika-la-nyumba-tarehe-27-februri2023-na-kusikiliza-changamoto-za-wananchi-zilizowa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/mheshimiwa-rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-dk-hussein-ali-mwinyi-amekutana-na-uongozi-wa-shirika-la-nyumba-tarehe-27-februri2023-na-kusikiliza-changamoto-za-wananchi-zilizowa#When:13:10:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[MHESHIMIWA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK. HUSSEIN ALI MWINYI AMEKUTANA NA UONGOZI WA SHIRIKA LA NYUMBA TAREHE 27 FEBRURI,2023  NA KUSIKILIZA  CHANGAMOTO ZA WANANCHI ZILIZOWASILISHWA  KUPITIA MFUMO WA SEMA NA RAIS KUHUSU WANANCHI WALIOPANGISHWA<br />
 <br />
NYUMBA NA SHIRIKA LA NYUMBA<br />
<br />
1.Ndugu Maosud Mussa Masoud ambae amemlalamikia Ndugu Abdulkarim Omar Salum kwenye nyumba Namba 10/99 iliyopo Michenzani. Mheshimiwa Rais baada kupitia vielelezo vya pande zote ametoa uamuzi wa kila mmoja apewe chumba kimoja katika nyumba hiyo.<br />
<br />
2.Ndugu Eshe Ali Salim amemlalamikia Ndugu Abbas Abdalla Mohamed kwenye nyumba Namba 6/10 iliyopo Michenzani Mheshimiwa Rais baada ya kupitia vielelezo vya pande zote ameamua kufuatwa kwa sheria na kutokuzingatiwa matatizo yao binafsi. Kwa hivyo Nyumba No 6/10 iliyopo Michenzani amepewa Ndugu Eshe Ali Salim kwa vile ndiye aliyetambulika kwenye Mkataba wa Ukodishaji kwa sasa.<br />
<br />
3.Feisal Ali Said amelilalamikia Shirika la Nyumba kumtoa katika nyumba Namba 239 iliyopo Hurumzi ambayo alipangishwa na Shirika hilo Mheshimiwa Rais baada kupitia vielelezo vya pande zote ametoa uamuzi wa kurejeshewa Nyumba hiyo. Ndugu Feisal Ali Said. Aidha amelitaka Shirika la Nyumba kuwatafutia nyumba nyengine wapangaji waliomo ndani ya nyumba hiyo.<br />
<br />
4.Ndugu Imam Ali Makame amelilalamikia Shirika la Nyumba malalamiko yafuatayo kuhusiana na Nyumba Namba 781 iliyopo Hurumzi. Kuongezewa kodi kutoka Shs 250,000 mpaka shs 2,000,000 kwa mwezi kutokana na kubadilisha matumizi ya makaazi ya nyumba na kuwa ya biashara.<br />
<br />
Kutokufidiwa gharama zake za matengenezo aliyofanya katika nyumba hiyo.<br />
<br />
Kutokujibiwa barua yake ya maombi ya kupatiwa mkataba wa muda mrefu, Mheshimiwa Rais ametoa maamuzi na kulitaka Shirika la nyumba lifanye mawasiliano nae na wajibu barua zake kwa kufuatilia anacho kilalamikia. <br />
<br />
5.Ndugu Gharib Ali  Issa amelalamikia  Shirika la Nyumba kwa kumtoa katika nyumba Namba 213 iliyopo Hurumzi aliyokuwa akiishi, Mheshimiwa Rais ametoa agizo kwa Shirika la Nyumba kuwasilisha barua walizomwandikia Ndugu Gharib zinazomtaka kulipa deni na akakataa kulipa deni hilo.Kutokana na kikao hicho Mheshimiwa Rais amesema hatua nyengine zitafuata. ]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-03-01T13:10:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa-mkurugenzi-mkuu-wa-mamlaka-ya-kuzuia-rushwa-na-uhujumu-uchumi-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa-mkurugenzi-mkuu-wa-mamlaka-ya-kuzuia-rushwa-na-uhujumu-uchumi-zanzibar#When:16:48:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi amemteua Ndugu Ali Abdalla Ali kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar katika Ofisi ya Rais Katiba Sheria,Utumishi na Utawala Bora.<br />
<br />
Kabla ya Uteuzi Ndugu Ali Abdalla Ali alikua Afisa Mwandamizi Ofisi ya Rais.<br />
<br />
Uteuzi huo Umeanza leo tarehe 05 Septemba 2022<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-09-05T16:48:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waameifariji Familia ya Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk-ali-mohamed-shein-pamoja-na-makamo-wa-rais-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-waameifariji-familia-ya-rais-mstaafu-alhaj-ali-hassan-mwinyi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk-ali-mohamed-shein-pamoja-na-makamo-wa-rais-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-waameifariji-familia-ya-rais-mstaafu-alhaj-ali-hassan-mwinyi#When:10:52:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[RAIS Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.  Philip Isdori Mpango kwa nyakati tofauti waameifariji Familia ya Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi kutokana na kifo cha mtoto wake Hassan Ali Hassan  kilichotokea Jumatano wiki hii katika Hospitali Kuu ya Mnazi mmoja, Mkoa wa Mjini Magharibi.<br />
<br />
<br />
Hafla  hiyo ilyioambatana na Dua ilifanyika nyumbani kwa Marehemu Chukwani Mkoa Mjini Magharibi ambapo Viongozi hao  pia walipata fursa ya kutoa mkono wa pole kwa  Rais mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, Mama Siti Mwinyi, Mke wa marehemu Fauzia Salim Hilali pamoja na wanafamilia.<br />
<br />
Walimuomba Mwenyezi Mungu amsamehe Marehemu madhambi yake na kuwataka wafiwa kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wao.<br />
<br />
Wakati huo huo; Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi alishiriki katika Mkutano Mkuu  wa Uchaguzi wa CCM ngazi ya Jimbo, uliofanyika Ofisi za  Jimbo la Mpendae, Mkoa wa Mjini Magharibi.<br />
<br />
Akitoa nasaha kwa wajumbe wa Mkutano huo, Dk. Mwinyi aliwataka kutumia vyema Demokrasi  kwa kuchagua Viongozi kwa busara kubwa na kuzingatia wanachama wenye uwezo, uadilifu na wanaokataa rushwa.<br />
<br />
Katika mkutano huo wajumbe walipata fursa ya kupiga kura na kuchagua Viongozi  mbali mbali katika nafasi ya Mwenyekiti wa Jimbo, Katibu wa Jimbo pamoja na Katibu wa Siasa na Uenezi wa Jimbo hilo.Nafasi nyengine zilizogombewa ni pamoja na Wajumbe watatu (3) wa Mkutano Mkuu wa Mkoa, wajumbe watano (5) wa Halmashauri Kuu ya Wilaya pamoja na Wajumbe watano (5) wa Halmashauri kuu ya jimbo.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-09-04T10:52:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi wa Kamishna wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-kamishna-wa-tume-ya-maadili-ya-viongozi-wa-umma</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-kamishna-wa-tume-ya-maadili-ya-viongozi-wa-umma#When:14:51:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua Dlt. Maua Abeid Daftari kuwa Kamishna wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora.Dkt. Maua alikuwa Mshauri wa Rais katika Awamu ya Saba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-07-08T14:51:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Hotuba ya Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Ikulu Mheshimiwa Jamal Kassim Ali Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi  ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 Aprili,2022.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-jamal-kassim-ali-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-ya-fedha-kwa-mwaka-wa-fedha-2022-2023-aprili2022</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/hotuba-ya-waziri-wa-nchi-afisi-ya-rais-ikulu-mheshimiwa-jamal-kassim-ali-kuhusu-makadirio-ya-mapato-na-matumizi-ya-fedha-kwa-mwaka-wa-fedha-2022-2023-aprili2022#When:12:29:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[YALIYOMO<br />
1. ORODHA YA VIAMBATISHO ...................................... iii<br />
2. VIFUPISHO VYA MANENO ........................................ iv<br />
3. UTANGULIZI ................................................................ 1<br />
4. MAJUKUMU YA AFISI YA RAIS IKULU ........................ 3<br />
5 MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS IKULU KWA KIPINDI CHA JULAI – MACHI 2021/2022 ................................ 7<br />
6. MWELEKEO WA BAJETI YA AFISI YA RAIS IKULU KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 ....................... 39<br />
7. PROGRAMU KUU NA NDOGO NA MAKISIO YA FEDHA ZINAZOHITAJIKA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 .............................................. 40<br />
8. MAMBO MAKUU YATAKAYOTEKELEZWA NA AFISI YA RAIS IKULU KWA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA WA 2022/2023 ............................................50<br />
9. MAOMBI YA FEDHA KWA KAZI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 ................................................................... 50<br />
10. HITIMISHO ................................................................. 51<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
iii ORODHA YA VIAMBATISHO<br />
Kiambatisho Nam.1. Mchanganuo wa Maagizo kwa kila Mkoa. .................................................................... 53<br />
Kiambatisho Nam. 2. Orodha ya Mada zilizojadiliwa kupitia Televisheni na Redio katika kipindi cha “Unatekelezaje? kwa kipindi cha Julai 2021 - Machi 2022...54<br />
Kiambatisho Nam. 3. Idadi ya taarifa zilizorushwa na waliotembelea Tovuti ya Ikulu kwa Kipindi cha Miezi Tisa 2021 – 2022 ..................................60<br />
Kiambatisho Nam. 4. Taarifa zilizorushwa Kupitia Mitandao ya Kijamii ya Ikulu kwa Kipindi cha Miezi Tisa 2021 – 022.........................................61<br />
Kiambatisho Nam. 5. Orodha ya Malalamiko yaliyowasilishwa na Wananchi kwa Kipindi cha Miezi 9 kutoka Julai mpaka Machi 2021/2022. ......................... 63<br />
Kiambatisho Nam. 6. Takwimu za Malalamiko yaliyowasilishwa na Wananchi kwa Taasisi 45 za Serikali zilizounganishwa katika Mfumo wa Sema na Rais kwa Kipindi Julai – Machi 2021/2022. .......................64<br />
Kiambatisho Nam. 7. Idadi ya Taasisi na Watumishi waliopatiwa Semina ya Utunzaji Nyaraka na Udhibiti wa Siri za Serikali................................... 68<br />
Kiambatisho Nam. 8. Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti ya Kazi za Kawaida kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 na Makadirio ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023. ............69<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
iv VIFUPISHO VYA MANENO<br />
AfCFTA Afirca Continental Free Trade Area (Soko huru la Biashara la Nchi za Afrika)<br />
AMREF African Medical and Research Foundation (Shirika la Utafiti wa Madawa Afrika)<br />
AU African Union (Umoja wa Nchi za Afrika)<br />
BLM Baraza la Mapinduzi<br />
CCM Chama Cha Mapinduzi<br />
COMESA Common Market for Eastern and Southern<br />
Africa (Soko la Pamoja za Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika)<br />
DRC Democratic Repulic of Congo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo)<br />
EAC East Africa Community (Jumuiya ya Afrika Mashariki)<br />
GSO Government Security Office (Afisi ya Usalama wa Serikali)<br />
IORA Indian Ocean Rim Association (Jumuiya za Nchi zilizopakana na Bahari ya Hindi)<br />
JCC Joint Commission for Cooperation (Tume ya Pamoja ya Ushirikiano)<br />
JPC Joint Permanent Commission (Tume za Kudumu za Pamoja)<br />
KBLM/KMK Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi<br />
NTB’s Non-Tariff Barriers (Vikwazo vya Biashara Visivyo vya Kiushuru)<br />
SADC Southern Africa Development Community (Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika)<br />
SDG’s Sustainable Development Goals (Malengo ya Maendeleo ya Melenia)<br />
BAJETI IKULU<br />
v SMT Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania<br />
SMZ Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar<br />
SNR Sema na Rais<br />
TEHAMA Teknolojia ya Habari na Mawasiliano<br />
TZS Tanzania Shiling (Shilingi ya Kitanzania<br />
UAE United Arab Emirates (Umoja wa Falme za Kiarabu)<br />
UNDP United Nations Development Programme<br />
UNICEF United Nations International Children’s<br />
Emergency Fund (Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto)<br />
USD United State Dollar (Fedha ya Marekani)<br />
UWEMAJO Umoja wa Wenye Mashamba Jozani <br />
VVU/UKIMWI Ukosefu wa Kinga Mwilini<br />
ZADEP Zanzibar Development Plan 2021 - 2026 (Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar)<br />
ZAWA Zanzibar Water Authority (Mamlaka ya Maji Zanzibar)<br />
ZBC Zanzibar Broadcasting Cooperation (Shirika la Utangazaji la Zanzibar)<br />
ZCTV Zanzibar Cable Television<br />
BAJETI IKULU<br />
<br />
1 UTANGULIZI<br />
1.Mheshimiwa Spika, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema kwa kutujaalia uzima na afya njema na kuweza kukutana hapa katika kikao hiki muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu. Aidha, kwa namna ya pekee namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kwa mara nyengine tena na kunipa jukumu la kuhudumu katika Afisi yake. Vile vile, nachukua fursa hii adhimu kumpongeza Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutuongoza, kutuelekeza na kusimamia ipasavyo utekelezaji wa majukumu ya Serikali kama ilivyoainishwa katika Katiba, Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025, Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar 2021-2026 (ZADEP) na Mipango mikuu ya Maendeleo kwa Taifa letu.<br />
<br />
2. Mheshimiwa Spika, napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi anavyoiongoza Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa weledi na kusimamia vyema Miradi mikubwa ya kimkakati katika kipinbdi cha mwaka mmoja cha uongozi wake.Aidha sisi sote ni mashahidi tunaona namna anavyoifungua nchi katika diplomasia ya uchumi.<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
2<br />
3. Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza Mheshimiwa Othman Masoud Othman, Makamu wa Kwanza wa Rais na Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdalla, Makamu wa Pili wa Rais kwa namna ambavyo wanamsaidia Mheshimiwa Rais katika kutekeleza majuku yake ya kila siku ya kuongoza na kusimamia shughuli za serikali.<br />
4. Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kukupongeza wewe binafsi, Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid na naibu wako Mheshimiwa Mgeni Hassan Juma na Mwenyekiti wa Baraza lako Tukufu Mheshimiwa Mwanaasha Khamis Juma kwa kuliongoza vyema Taifa hili. Katika uongozi wako tumeshuhudia uendeshaji wa mijadala iliyo wazi na yenye nidhamu ya hali ya juu ya waheshimiwa wajumbe wa Baraza lako.<br />
5. Mheshimiwa Spika, natoa shukran maalum kwa Mwenyekiti wa kamati ya kusimamia Afisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa, Mheshimiwa Machano Othman Said Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mheshimiwa Mtumwa Peya Yussuf, Mwakilishi wa Jimbo la Bumbwini pamoja na Wajumbe wote wa Kamati kwa mashirikiano na miongozo wanayotupatia.<br />
6. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais Ikulu imeanzishwa kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa Mheshimiwa Rais katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu namba 50(04). Afisi ya Rais Ikulu ni matokeo ya mabadiliko ya Miundo ya<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
3 Wizara yaliyofanyika mara tu baada ya kuanza kwa Awamu ya Nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Awali Afisi hii ilikuwa ni sehemu ya Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji na mnamo tarehe 10 Julai, 2021 ilianzishwa Afisi ya Rais Ikulu.<br />
7. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais Ikulu katika Awamu hii ya Nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeundwa upya na kuongezewa majukumu ya kushughulikia Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar. Kwa sasa, Afisi ya Rais Ikulu ina jukumu la kusimamima Afisi ya Faragha ya Mheshimiwa Rais, Afisi ya Baraza la Mapinduzi,Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Idara ya Utumishi na Uendeshaji, Idara ya Mawasiliano na Habari, Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Uratibu wa Shughuli za Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi, Afisi ya Usalama wa Serikali (GSO),Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu na Afisi ya Rais Ikulu - Pemba.<br />
<br />
MAJUKUMU YA AFISI YA RAIS IKULU<br />
<br />
8. Mheshimiwa Spika, Kutokana na mabadiliko yaliyofanyika Serikalini, Afisi ya Rais Ikulu itatekeleza majukumu yafuatayo:<br />
i. Kusimamia shughuli za Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.<br />
ii. Kuhakikisha kuwa jamii inapata habari juu ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo na Sera zinazotekelezwa na Mheshimiwa Rais<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
4 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.<br />
iii. Kusimamia majukumu ya kikatiba na kisheria ya Baraza la Mapinduzi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi.<br />
iv. Kusaidia uchambuzi wa Nyaraka na Sheria zinazotarajiwa kuwasilishwa serikalini pamoja na kufuatilia utekelezaji wake.<br />
v. Kuratibu na kusimamia shughuli za Wazanzibari wanaoishi Nje ya Nchi (Diaspora).<br />
vi. Kuratibu na kuandaa shughuli za Mipango,Sera na Utafiti katika Afisi ya Rais Ikulu.<br />
vii. Kusimamia Nyaraka na Kumbukumbu zote za Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) kwa zile Taasisi zake zilizopo Zanzibar.<br />
viii. Kupanga na kusimamia utekelezaji wa shughuli za Afisi ya Usalama wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (GSO).<br />
9. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi sasa naomba uniruhusu niwasilishe kwa ufupi Utekelezaji wa Programu za Afisi ya Rais Ikulu kwa kipindi cha Julai 2021 – Machi 2022.<br />
10. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais Ikulu kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ilitekeleza Programu kuu tano na ndogo 14 chini ya Mafungu mawili ambayo ni A01 na A02. Utekelezaji wa Programu hizi, ulizingatia Mipango Mikuu ya Kitaifa ikiwemo Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 - 2025, ZADEP, Hotuba ya Rais wa Zanzibar<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
5 Rais na Mwenyekiti wa Bararaza la Mapinduzi aliyoitoa katika ufunguzi wa Baraza la Kumi la Wawakilishi pamoja na miongozo, maelekezo na maagizo aliyoyatoa. Kupitia Programu zake, Afisi iliandaa Mpango Kazi wa mwaka 2021/2022 na kuweka vipaumbele katika mambo yafuatayo:-<br />
a) Kuimarisha utendaji na umakini katika matumizi ya rasilimali za Serikali<br />
11. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuhimiza umakini katika nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na kupiga vita vitendo vya rushwa na uhujumu wa uchumi. Ni imani yetu kuwa, umma na wadau wa<br />
maendeleo wameshuhudia utumishi unaofuata sheria na uadilifu katika kuhudumia jamii pamoja na kuimarika kwa nidhamu za watendaji wa Serikali. Aidha, pamoja na mabadiliko hayo,Serikali inaendelea kuwahimiza watendaji wa Wizara, Idara na Taasisi zake kuzingati sheria na uwadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao ili<br />
kupata matokeo ya utumishi wenye ufanisi.<br />
b) Kudumisha Amani na Utulivu Nchini <br />
12. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kupitia ziara na mikutano yake na makundi mbali mbali ya kijamii,ameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
6 Amani na utulivu. Kwa kutolea mfano tarehe 25 Machi, 2022 wakati alipokuwa akizungumza na waumini wa dini ya kiislamu katika Masjid Arafa Mombasa Wilaya ya Magharibi “B” aliwasisitiza wananchi kuendelea kuhubiri amani.<br />
c) Kuimarika kwa Ushiriki wa Zanzibar katika masuala ya Mtangamano wa Kikanda na Jumuiya za Kimataifa<br />
13. Mheshimiwa Spika, Afisi kupitia Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Uratibu wa Wazanzibari wanaoishi Nje ya Nchi, imehakikisha kuwa Zanzibar inanufaika na uhusiano wa Jumuiya za Kikanda na Kimataifa. Katika kufikia hatua hii, wataalamu wamewezeshwa kushiriki katika vikao vya mtangamano wa kikanda na kimataifa,pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa na faida zinazotokana na Jumuiya hizo.<br />
Aidha, Serikali inaendelea kuzihamasisha balozi na jumuiya za kimataifa kufungua Afisi ndogo za uwakilishi Zanzibar ili ziweze kiungo muhimu cha kukuza uwekezaji na upatikanaji wa masoko ya bidhaa katika nchi zao na kuvutia uwekezaji Zanzibar.<br />
d) Uratibu wa Wazanzibari Wanaoishi Nje ya Nchi.<br />
14. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais Ikulu imeweka mazingira wezeshi na kuendelea kuratibu na kuhamasisha ushiriki wa Wazanzibari wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) ili waweze kuzitangaza<br />
<br />
BAJETI IKULU<br />
7 Fursa zinazopatikana nchini na kushiriki kikamilifu katika kuchangia maendeleo ya kiuchumi ya nchi yetu. Afisi imehakikisha kuwa, kupitia sheria namba 4 ya 2020, inayosimamia utekelezaji wa Sera ya Diaspora kwa mujibu wa miongozo iliyopo imewezesha wanadiaspora wa Zanzibar kushiriki ipasavyo katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii.<br />
e) Kusimamia na Kutunza Nyaraka na Kumbukumbu.<br />
15. Mheshimiwa Spika, Afisi ya Rais Ikulu, kupitia Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu imeendelea kufanya ukaguzi wa kumbukumbu na nyaraka kwa Wizara na Taasisi za Serikali. Aidha, imeweza kutoa huduma za utafiti kwa Watafiti wa ndani na Watafiti nje ya nchi. Vile vile Afisi imetangaza na kutoa taaluma kuhusu kazi, majukumu na umuhimu wa nyaraka zinazohifadhiwa na Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar kupitia Maonesho ya Biashara ya kuadhimisha Sherehe za Miaka 58 ya Mapinduzi ya Zanzibar.<br />
<br />
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA AFISI YA RAIS IKULU KWA KIPINDI CHA JULAI – MACHI 2021/2022<br />
16. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Afisi ya Rais Ikulu kupitia Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu ilipangiwa kukusanya TZS. 15.0 Milioni.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-05-27T12:29:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>THE STATE UNIVERSITY OF ZANZIBAR (SUZA)&amp;nbsp; JOB OPPORTUNITIES</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/the-state-university-of-zanzibar-suza-job-opportunities</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/the-state-university-of-zanzibar-suza-job-opportunities#When:12:07:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-05-20T12:07:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametuma salamu za pole kwa wanafunzi pamoja na walimu wa skuli ya Sekondari ya Kengeja Ufundi kiswani Pemba</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-dk-hussein-ali-mwinyi-ametuma-salamu-za-pole-kwa-wanafunzi-pamoja-na-walimu-wa-skuli-ya-sekondari-ya-kengeja-ufundi-kiswani-pemba</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-dk-hussein-ali-mwinyi-ametuma-salamu-za-pole-kwa-wanafunzi-pamoja-na-walimu-wa-skuli-ya-sekondari-ya-kengeja-ufundi-kiswani-pemba#When:11:37:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametuma salamu za pole kwa wanafunzi pamoja na walimu wa skuli ya Sekondari ya Kengeja Ufundi kiswani Pemba kufuatia kuungua moto kwa daghalia ya wanawake katika skuli hiyo.<br />
<br />
Katika salamu hizo za pole, Rais Dk. Mwinyi alieleza jinsi alivyopokea kwa mshituko na huzuni kubwa tukio hilo lililotokea hapo jana lililosababisha uharibifu wa jengo hilo, vitanda, vifaa vya kusomea vya wanafunzi pamoja na vifaa vyengine vya matumzi ya wanafunzi.<br />
<br />
Salamu hizo za pole zilieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itachukua juhudi za makusudi katika kuhakikisha inawawekea mazingira mazuri mbadala kwa wakati huu wanafunzi hao pamoja na kuhakikisha hali ya daghalia hiyo inarejea kama ilivyokuwa mwanzo ili waweze kuendelea na masomo yao kama kawaida.<br />
<br />
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuzitaka taasisi husika kufanya uchunguzi wa kina juu ya ajali hiyo ya moto ili majanga kama hayo yasiendelee kutokea kwa mara nyengine tena hasa ikizingatiwa kwamba tayari matukio kama hayo yamesharipotiwa hivi karibuni katika skuli ya Utaani na Madungu kisiwani humo.<br />
<br />
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud viashiria vya mwanzo vya tukio hilo la moto vinaonesha kwamba  linatokea na hitilafu ya umeme lakini hakuna mwanafunzi aliyepata majeraha ya moto huo na wanafunzi wote wako salama.<br />
<br />
Alisema kuwa athari zaidi imetokea kwa kuungua jengo pamoja na vifaa vyote vya wanafunzi vilivyokuwemo ndani huku akisema kwamba Serikali ya Mkoa inaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo sambamba kuwasilisha  misaada mbali mbali kwa ajili ya wanafunzi hao ili waweze kuendelea na masomo yao ipasavyo<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-05-17T11:37:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dk.Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia ajali ya basi lililogongana na lori  huko katika eneo la Melea, Kibaoni, Mkoani Morogoro.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk.hussein-ali-mwinyi-ametoa-salamu-za-rambirambi-kwa-familia-za-marehemu-waliofariki-kufuatia-ajali-ya-basi-lililogongana-na-lori-huko-katika-eneo-la-melea-kibaoni-mkoani-morogoro</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk.hussein-ali-mwinyi-ametoa-salamu-za-rambirambi-kwa-familia-za-marehemu-waliofariki-kufuatia-ajali-ya-basi-lililogongana-na-lori-huko-katika-eneo-la-melea-kibaoni-mkoani-morogoro#When:09:26:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia ajali ya basi lililogongana na lori  huko katika eneo la Melea, Kibaoni, Mkoani Morogoro.<br />
<br />
Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi alieleza kusikitishwa na vifo vilivyotokana na ajali hiyo na kuzinasihi familia za marehemu kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha misiba hiyo.<br />
<br />
“Kwa niaba yangu binafsi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wake tunatoa mkono wa pole kufuatia vifo hivyo vilivyotokana na ajali hiyo na tunaungana na ndugu, jamaa na marafiki katika maombolezi”, ilieleza sehemu ya salamu hizo za rambirambi za Rais Dk. Mwinyi.<br />
<br />
Rais Dk. Mwinyi alimuomba Mwenyezi Mungu awalaze Marehemu wote mahala pema peponi,  Amin.<br />
<br />
Aidha, Rais Dk. Mwinyi aliwaombea kwa Mwenyezi Mungu majeruhi wote wa ajali hiyo kupona kwa haraka ili waweze kuendelea na shughuli zao za kimaisha.<br />
<br />
Ajali hiyo ilitokea jana jioni Machi 18 ambapo watu 22 walifariki dunia huku zaidi ya 30 wakijeruhiwa baada ya basi lenye namba za usajili T732 ATH mali ya Kampuni ya AHMEED linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Tanga kugongana uso kwa uso na lori lenye namba IT 2816 katika eneo la Melea, Kibaoni barabara ya Iringa-Morogoro.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-03-19T09:26:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Dk. Hussein Ali Mwinyi amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk-hussein-ali-mwinyi-amemtumia-salamu-za-pongezi-rais-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-samia-suluhu-hassan</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/dk-hussein-ali-mwinyi-amemtumia-salamu-za-pongezi-rais-wa-jamhuri-ya-muungano-wa-tanzania-samia-suluhu-hassan#When:09:24:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kushika madaraka ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.<br />
<br />
Katika salamu hizo,  Rais Dk. Mwinyi alieleza kuwa kwa niaba yake na kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanziba na wananchi wake wote wanamtakia kila la kheri Rais Samia katika uongozi wake uliotukuka na kuahidi kuendelea kumuunga mkono ili maendeleo zaidi yaendelee kupatikana hapa nchini.<br />
<br />
Rais Dk. Mwinyi  alieleza kuwa uongozi wa Rais Samia utaendelea kuwa Dira ya Maendeleo hasa kwa kuzingatia kauli mbiu yake aliyokuja nayo na “KAZI IENDELEE”, akimaanisha kwamba yale mazuri yote aliyoyaacha mtangulizi wake Hayati Rais Dk. John Pombe Magufuli anayaendeleza kwa vitendo na kwa ustadi mkubwa.<br />
<br />
Hivyo, alisisitiza kwamba wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wana kila sababu ya kuendelea kumuunga mkono sambamba na kuiunga mkono kauli mbiu hiyo ili yale maono ya Rais Samia aweze kuyafikia na kuyatekeleza.<br />
<br />
Aidha, alieleza imani kubwa waliyonayo wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Rais wao mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan kwani wanathamini jitihada zake kubwa anazozichukua katika kuhakikisha maendeleo endelevu yanapatikana hapa nchini. <br />
<br />
Sambamba na hayo, Rais Dk. Mwinyi amemuombea kwa MwenyeziMungu kumpa maisha marefu yenye afya na nguvu Rais Samia ili aendelee kuiongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watu wake<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-03-19T09:24:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi wa Makatibu Tawala wa Wilaya</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa-makatibu-tawala-wa-wilaya</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa-makatibu-tawala-wa-wilaya#When:13:15:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dkt.Hussein Ali Mwinyi amewateua wafuatao kuwa Makatibu Tawala wa Wilaya katika Wilaya mbali mbali za Zanzibar.<br />
1. Ndugu Said Haji Mrisho ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mjini katika   <br />
   Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.<br />
2. Ndugu Juma Abdalla Hamad ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Magharibi "A" <br />
   katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.<br />
3. Ndugu Sahim Harun Haji ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Magharibi "B" <br />
   katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.<br />
4. Ndugu Mariam Said Khamis ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini "A" <br />
   katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.  <br />
5. Ndugu Hassan Abdallah Rashid ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini <br />
   "B"katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.<br />
6. Ndugu Hamza Mahmoud Juma ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kati katika  <br />
   Mkoa wa Kusini Unguja.<br />
7  Ndugu Mbaraka Omar Kasongo ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kusini <br />
   katika Mkoa wa Kusini Unguja.<br />
8. Ndugu Miza Hassan Faki ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya Mkoani katika Mkoa <br />
   wa Kusini Pemba.<br />
<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-03-16T13:15:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi mpya wa Mawaziri na Manaibu Mawaziri  wa Serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-mpya</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-mpya#When:19:19:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi leo tarehe 08 Machi,2022 amefanya mabadiliko katika Baraza la Mapinduzi kwa kuigawa iliyokuwa Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto kuwa Wizara mbili na kuwabadilisha Wizara baadhi ya Mawaziri.Aidha Mhe.Rais pia amewateua Mawaziri wapya wanne na Naibu Mawaziri wapya saba.Kufuatia mabadiliko hayo,Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa itakuwa na Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-<br />
<br />
<br />
1. OFISI YA RAIS<br />
   i. Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais - Ikulu<br />
      Mhe:Jamali Kassim Ali.Kabla ya uteuzi huo Mhe.Jamal alikuuwa Waziri wa    <br />
      Nchi,Ofisi ya Fedha na Mipango]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-03-08T19:19:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi  ZRB</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-zrb</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-zrb#When:12:05:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua NDUGU YUSUPH JUMA MWENDA kuwa KAMISHNA WA BODI YA MAPATO ZANZIBAR (ZRB). Kabla ya Uteuzi huo ndugu Yusuph Juma Mwenda alikuwa mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)<br />
Uteuzi huo unaanzia leo tarehe 01 Machi,2022]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-03-01T12:05:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi Kamishna</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-kamishna</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-kamishna#When:15:32:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua KANAL BURHAN ZUBERI NASSOR kuwa KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA ZANZIBAR.<br />
Uteuzi huo unaanzia leo tarehe 22 Februari,2022]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-22T15:32:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-wa#When:11:36:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua BALOZI MOHAMMED MWINYI MZALE kuwa KAMISHNA WA TUME YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA katika Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria Utumishi na Utawala BVora.<br />
Uteuzi huo unaanza leo tarehe 18 Februari,2022]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-18T11:36:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Utenguzi ZRB</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/utenguzi-002</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/utenguzi-002#When:11:23:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi ametengua uteuzi wa KAMISHNA WA BODI YA MAPATO ZANZIBAR (ZRB) NGUGU SALUM YUSSUF ALI kuanzia leo tarehe 17 Februari,2022]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-17T11:23:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Salam za rambirambi kwa Mzee  Malecela.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/salam-za-rambirambi-kwa-mzee-malecela</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/salam-za-rambirambi-kwa-mzee-malecela#When:15:31:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Mzee John Malecela kufuatia kifo cha mpendwa wao Mwelentuli Malecela.<br />
<br />
Aidha, Rais Dk. Mwinyi ametoa salamu hizo za pole kwa ndugu jamaa na marafiki pamoja na uongozi wote wa Shirika la Afya Duniani (WHO), ambapo marehemu  hadi umauti unamfika alikuwa ni Mkurugenzi  wa Udhibiti wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele.<br />
<br />
Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi alieleza kusikitishwa na kifo hicho na kuwanasihi ndugu, jamaa na marafiki pamoja na uongozi wote wa (WHO) kuwa na subira na ustahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo.<br />
<br />
Rais Dk. Mwinyi amemuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi,  Amin.<br />
<br />
Marehemu Mwelentuli alizaliwa Machi 26, 1963  ambapo katika uhai wake aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tafiti za kiafya Tanzania (NIMRI) ambapo pia, aliwahi kuwania nafasi ya mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.<br />
]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-12T15:31:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Utenguzi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/utenguzi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/utenguzi#When:11:56:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi ametengua uteuzi wa viongozi wafuatao kuanzia leo tarehe 03 Februari,2022:-<br />
1. Ndugu Omar Ali Omar  - Mkurugenzi wa Idara ya Utumishi na Uendeshaji katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.<br />
2. Ndugu Suleiman Yahya Ame - Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.<br />
3. Ndugu Fatma Ali Iddi - Kamisna wa Kazi katika Ofisi ya Rais,Kazi,Uchumi na Uwekezaji.<br />
4. Salum Ubwa Nassor - Afisa Mdhamini Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Pemba.<br />
5. Ndugu Nasima Haji Chum - Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia na Watoto katika Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-03T11:56:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uteuzi</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-0004</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/publications/uteuzi-0004#When:12:21:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi amemteua NDUGU ILYASA PAKACHA HAJI kuwa MKURUGENZI WA MIPANGO,SERA NA UTAFITI katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi,Zanziba.Kabla ya Uteuzi huo Ndugu Ilyasa alikuwa Afisa Mipango katika Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Zanzibar.<br />
Uteuzi huo unaanza leo 02 Februari,2022.]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2022-02-02T12:21:00+00:00</dc:date>
	</item>
	<item>
	  <title>Dkt.Hussein Ali Mwinyi  ameshiriki katika Ibada ya Sala ya Ijumaa Fuoni Chunga.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/dkt.hussein-ali-mwinyi-ameshiriki-katika-ibada-ya-sala-ya-ijumaa-fuoni-chunga</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/dkt.hussein-ali-mwinyi-ameshiriki-katika-ibada-ya-sala-ya-ijumaa-fuoni-chunga#When:13:41:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2026-02-20T13:41:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amelizindua baraza la Wawakilishi leo</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amelizindua-baraza-la-wawakilishi-leo</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-na-mwenyekiti-wa-baraza-la-mapinduzi-mhe-dkt-hussein-ali-mwinyi-amelizindua-baraza-la-wawakilishi-leo#When:15:43:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2025-11-10T15:43:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya CCM Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amechukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/mgombea-urais-wa-zanzibar-kwa-tiketi-ya-ccm-mhe.dk.hussein-mwinyi-amechukua-fomu-ya-kugombea-urais-wa-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/mgombea-urais-wa-zanzibar-kwa-tiketi-ya-ccm-mhe.dk.hussein-mwinyi-amechukua-fomu-ya-kugombea-urais-wa-zanzibar#When:14:06:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-30T14:06:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzbar Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi ameifungua Hoteli ya Kitalii ya Zanbreeze Beach Resort &amp;amp; Spa Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzbar-mhe.dk.hussein-ali-mwinyi-ameifungua-hoteli-ya-kitalii-ya-zanbreeze-beach-resort-spa-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzbar-mhe.dk.hussein-ali-mwinyi-ameifungua-hoteli-ya-kitalii-ya-zanbreeze-beach-resort-spa-zanzibar#When:16:54:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-16T16:54:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Alhajj Dk.Hussein Mwinyi amezungumza na Uongozi wa Al Madrasat Swifat Nabawiyatil Msolopa Ikulu Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-alhajj-dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-uongozi-wa-al-madrasat-swifat-nabawiyatil-msolopa-ikulu-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-alhajj-dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-uongozi-wa-al-madrasat-swifat-nabawiyatil-msolopa-ikulu-zanzibar#When:17:27:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-15T17:27:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Alhajj Dk.Hussein Mwinyi amejumuiya na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa na Dua Maalumu ya Kuimombea Nchi Amani na Viongozi Wakuu wa Serikali</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-alhajj-dk.hussein-mwinyi-amejumuiya-na-waumini-wa-dini-ya-kiislamu-katika-sala-ya-ijumaa-na-dua-maalumu-ya-kuimombea-nchi-amani-na-viongozi-wakuu-wa-serikali</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-alhajj-dk.hussein-mwinyi-amejumuiya-na-waumini-wa-dini-ya-kiislamu-katika-sala-ya-ijumaa-na-dua-maalumu-ya-kuimombea-nchi-amani-na-viongozi-wakuu-wa-serikali#When:17:18:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2025-08-15T17:18:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Taarab Rasmi na Chakula Ikulu.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/taarab-rasmi-na-chakula-ikulu</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/taarab-rasmi-na-chakula-ikulu#When:20:35:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-12T20:35:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/kilele-cha-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/kilele-cha-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-zanzibar#When:17:04:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-12T17:04:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Dkt.Hussein Ali Mwimyi ametunuku Nishani</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-dkt.hussein-ali-mwimyi-ametunuku-nishani</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-dkt.hussein-ali-mwimyi-ametunuku-nishani#When:15:22:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-11T15:22:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Ufunguzi wa Eneo la Maonesho ya Biashara na Tamasha la 10 la Biashara Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-eneo-la-maonesho-ya-biashara-na-tamasha-la-10-la-biashara-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-eneo-la-maonesho-ya-biashara-na-tamasha-la-10-la-biashara-zanzibar#When:16:43:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-10T16:43:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Utiaji saini Makubaliano Ujenzi wa Bandari ya Abiria Mpiga Duri.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/utiaji-saini-makubaliano-ujenzi-wa-bandari-ya-abiria-mpiga-duri</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/utiaji-saini-makubaliano-ujenzi-wa-bandari-ya-abiria-mpiga-duri#When:05:45:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-10T05:45:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amefungua Skuli ya Sekondari ya Tumekuja ikiwa ni Shamrashara za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amefungua-skuli-ya-sekondari-ya-tumekuja-ikiwa-ni-shamrashara-za-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amefungua-skuli-ya-sekondari-ya-tumekuja-ikiwa-ni-shamrashara-za-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar#When:14:50:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-09T14:50:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>UFUNGUZI WA BANDARI YA FUMBA</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-bandari-ya-fumba</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-bandari-ya-fumba#When:16:02:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-08T16:02:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOTELI YA ZANZIBAR CROWN AND RESORT LIMITED.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/jiwe-la-msingi-ujenzi-wa-hoteli-ya-zanzibar-crown-and-resort-limited</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/jiwe-la-msingi-ujenzi-wa-hoteli-ya-zanzibar-crown-and-resort-limited#When:14:56:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-07T14:56:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>JIWE LA MSINGI SOKO LA MWANAKWEREKWE</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/jiwe-la-msingi-soko-la-mwanakwerekwe</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/jiwe-la-msingi-soko-la-mwanakwerekwe#When:15:38:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-06T15:38:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>MATEMBEZI NA MAZOEZI YA VIUNGO</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/matembezi-na-mazoezi-ya-viungo</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/matembezi-na-mazoezi-ya-viungo#When:09:52:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2024-01-01T09:52:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA KITUO CHA MABASI KIJANGWANI ,IKIWA NI SHAMRASHAMRA ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ameweka-jiwe-la-msingi-mradi-wa-ujenzi-wa-kituo-cha-mabasi-kijangwani-ikiwa-ni-shamrashamra-za-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ameweka-jiwe-la-msingi-mradi-wa-ujenzi-wa-kituo-cha-mabasi-kijangwani-ikiwa-ni-shamrashamra-za-maadhimisho-ya-miaka-60-ya-mapinduzi-ya-zanzibar#When:17:26:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-31T17:26:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amefungua Viwanja vya Michezo vya Matumbaku Spotrs Complex Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amefungua-viwanja-vya-michezo-vya-matumbaku-spotrs-complex-miembeni-wilaya-ya-mjini-unguja</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amefungua-viwanja-vya-michezo-vya-matumbaku-spotrs-complex-miembeni-wilaya-ya-mjini-unguja#When:13:49:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-30T13:49:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Ufunguzi wa Viwanja vya Matumbaku Sports Complex</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-viwanja-vya-matumbaku-sports-complex</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/ufunguzi-wa-viwanja-vya-matumbaku-sports-complex#When:10:01:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-30T10:01:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>MAHFALI YA 19 CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR (SUZA).</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/mahfali-ya-19-chuo-kikuu-cha-taifa-cha-zanzibar-suza</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/mahfali-ya-19-chuo-kikuu-cha-taifa-cha-zanzibar-suza#When:14:43:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-28T14:43:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AHUTUBIA NA KUUFUNGUA UWANJA WA MAAN ZANZIBAR IKIWA NI SHAMRASHAMRA ZA MIAKA 60 YA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ahutubia-na-kuufungua-uwanja-wa-maan-zanzibar-ikiwa-ni-shamrashamra-za-miaka-60-ya-mapinduzi-matukufu-ya-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ahutubia-na-kuufungua-uwanja-wa-maan-zanzibar-ikiwa-ni-shamrashamra-za-miaka-60-ya-mapinduzi-matukufu-ya-zanzibar#When:11:15:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-28T11:15:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Uwekaji wa Jiwe la msingi maegesho ya magari,Malindi.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/uwekaji-wa-jiwe-la-msingi-maegesho-ya-magarimalindi</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/uwekaji-wa-jiwe-la-msingi-maegesho-ya-magarimalindi#When:13:30:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-21T13:30:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>CHAMA CHA WAJANE AFRICA</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/chama-cha-wajane-africa</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/chama-cha-wajane-africa#When:05:35:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-20T05:35:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Maadhimisho ya Siku ya Maadili na haki za Binadamu tarehe 19 Disemba,2023</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/maadhimisho-ya-siku-ya-maadili-na-haki-za-binadamu-tarehe-19-disemba2023</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/maadhimisho-ya-siku-ya-maadili-na-haki-za-binadamu-tarehe-19-disemba2023#When:11:47:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-19T11:47:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amezindua Mpango wa Kitaifa wa wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii Zanzibar Viwanja vya Maisara Suleiman</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezindua-mpango-wa-kitaifa-wa-wahudumu-wa-afya-ngazi-ya-jamii-zanzibar-viwanja-vya-maisara-suleiman</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezindua-mpango-wa-kitaifa-wa-wahudumu-wa-afya-ngazi-ya-jamii-zanzibar-viwanja-vya-maisara-suleiman#When:15:59:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-16T15:59:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>DUA MAALUM YA KUOMBEWA RAIS WA ZANZIBAR,MASJID MUSHAWWAR MJINI ZANZIBAR</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/dua-maalum-ya-kuombewa-rais-wa-zanzibarmasjid-mushawwar-mjini-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/dua-maalum-ya-kuombewa-rais-wa-zanzibarmasjid-mushawwar-mjini-zanzibar#When:12:44:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-15T12:44:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA VIWANJA VYA NJE YA UWANJA WA AMAAN ZANZIBAR</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ameweka-jiwe-la-msingi-la-ujenzi-wa-viwanja-vya-nje-ya-uwanja-wa-amaan-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-ameweka-jiwe-la-msingi-la-ujenzi-wa-viwanja-vya-nje-ya-uwanja-wa-amaan-zanzibar#When:15:55:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-14T15:55:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amezungumza na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Nchini Bw.Shigeki Ikulu Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-mwakilishi-mkazi-wa-undp-nchini-bw.shigeki-ikulu-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-mwakilishi-mkazi-wa-undp-nchini-bw.shigeki-ikulu-zanzibar#When:15:16:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-14T15:16:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amezungumza na Rais wa Taasisi ya YTB ya Uturuki.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-rais-wa-taasisi-ya-ytb-ya-uturuki</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-rais-wa-taasisi-ya-ytb-ya-uturuki#When:12:48:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-07T12:48:00+00:00</dc:date>
	</item>	<item>
	  <title>Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi amezungumza na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania Ikulu Zanzibar.</title>
	  <link>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-naibu-mkurugenzi-mkuu-wa-umoja-wa-ulaya-nchini-tanzania-ikulu-zanzibar</link>
	  <guid>https://www.ikuluzanzibar.go.tz/blog/rais-wa-zanzibar-mhe.dk.hussein-mwinyi-amezungumza-na-naibu-mkurugenzi-mkuu-wa-umoja-wa-ulaya-nchini-tanzania-ikulu-zanzibar#When:12:43:00Z</guid>
	  <description><![CDATA[]]></description> 
	  <dc:subject></dc:subject>
	  <dc:date>2023-12-07T12:43:00+00:00</dc:date>
	</item>
	</channel>
</rss>