Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua Dkt. Maua Abeid Daftari kuwa Kamishna wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora.Dkt. Maua alikuwa Mshauri wa Rais katika Awamu ya Saba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.