Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amemuapisha Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Maryam Seif Hemed, kufuatia uteuzi wake katika nafasi hiyo.Hafla ya uapisho imefanyika leo, tarehe 11 Agosti 2026, Ikulu Zanzibar.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla; Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla; Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Dkt. Mwinyi Talib Haji; Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Ndg. Mansura Mosi Kassim, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wengine waliohudhuria ni Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, viongozi wa dini na wageni mbalimbali waalikwa.