Mgombea wa kiti cha Rais wa Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuweka mkazo zaidi kuwasaidia Wakulima ili waweze kunufaika na Kuendesha Kilimo chenye tija.Rais Dkt, Mwinyi ameyasema hayo katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika Uwanja wa Michezo Uzini, Wilaya Kati ,Mkoa wa Kusini Unguja.           

Amefahamisha kuwa Serikali katika Awamu ijayo itaongeza fungu ili kuwawezesha Wananchi kiuchumi ikiwemo Makundi ya Wakulima na Wafugaji waweze kuzalisha zaidi kwa kuwapatia Pembejeo ,Mbegu bora ,Mbolea na Masoko ya bidhaa zao kwa wakati. 

Hatua hiyo itaenda sambamba na kuwapatia mikopo midogo isio na riba ili kuendesha shughuli zao. 

Akizungumzia Sekta ya Ufugaji na tatizo la kukosa soko la Uhakika la Bidhaa wanazozalisha Wafugaji   amesema Serikali ijayo itawawezesha kwa mikopo na kuwatafutia Masoko ya Uhakika .     

Rais Dkt, Mwinyi anaewania kwa kipindi cha Pili kuiongoza Zanzibar amewaomba Wana CCM na Wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kukichagua Chama cha Mapinduzi ili kiendelee kuleta Maendeleo.